Kuna siku moja nilikwenda Banki ambayo ipo karibu sana hapa ofisi zetu zilipo eneo la Kibaha jina lake linaanzia na herufi "N". Nilikwenda kuchukua shilingi laki moja tu, kupitia dirishani yaani kwa Teller.Cha ajabu nilipokwenda siku nyingine si nikakuta eti Statement ya Account yangu inaonesha siku ile nilitoa milioni moja.
Yaani nimehangaika kumuona Bank Manager wa tawi lile lakini wapi, mpaka sasa sijapata pesa zangu. Jamani huu si wizi lakini ? Je nifanyeje kupata pesa zangu ?
Yaani nimehangaika kumuona Bank Manager wa tawi lile lakini wapi, mpaka sasa sijapata pesa zangu. Jamani huu si wizi lakini ? Je nifanyeje kupata pesa zangu ?