Sijui jina halisi la watu wenye hulka ya maneno kama ya kwako.!Mngekuwa basi wapole, wastaarabu, wafuata sheria, watetea haki za binadamu, wafuata ushauri, sio kwa huo ubabe wenu wa kishamba, misifa kujikweza, kujifanya kila kitu mnajua, watesaji, na wauwaji, mkafie mbali
Wahaya mnataka muwe marais mara ngapi?. Mtafute Britanicca akueleze Katto ni nani?.Yaani unataka wasukuma muwe maraisi tuu na sisi wahaya tubaki kuwaangalia
Paskali wewe ni mwandishi mzuri unayeandika taarifa ambazo ni researched na uandishi wako ni wa mpangilio. Ila, sasa naona unaanza kupotoka. Si lazima uandike kila wazo linalokuja kwenye kichwa chako. Utajiharibia sasa hivi. Kumbuka ni kazi ngumu sana kujijenga na kufikia level ambayo umefika, lakini ni kazi rahisi sana ambayo haichukui muda wa mwezi kuharibu sifa yako nzuri na kusahaulika kabisa. Ukishaharibu kazi ya kurudisha heshima yako itakuwa ngumu na almost impossibleWanabodi,
Kabla Magufuli hajawa rais wetu, sisi wengine wenu tulijua tangu mwaka 2014 na tukasema humu!.Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli
Miongoni mwa sifa zilizomuibua Magufuli ni sifa inayoitwa "uthubutu" unreasonably ambayo wengine huita ni udikiteta. Yaani kuachana na mambo ya kufuata sheria, taratibu na kanuni, ndiyo yametufikisha hapa, hawa viongozi wenye "uthubutu" hawahitaji kujua sheria, taratibu na kanuni, zinataka nini, bali hufanya lile linalowezekana,
Ndio maana tukasema humu, japo Magufuli kweli ni dikiteta, Tanzania mahali ilipofika ilimhitaji mtu kama Magufuli na Mwenyeenzi Mungu akaisikia sala yetu, akatupatia Magufuli!.
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Tukija kwa Makonda, muda mfupi baada ya kuteuliwa DC wa Kinondoni, akaonyesha uwezo, hivyo kama ilivyokuwa kwa Magufuli, mwaka 2014 tulisema ni Magufuli, na mwaka 2015 kweli akawa yeye. Vivyo hivyo kwa Makonda akiwa DC, akina sisi tukasema hivi Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
Na kweli haukupita muda akawa!.
Hivyo kwa hii kazi nzuri yote anayoifanya Magufuli, atakapoondoka ile 2025, kama hatamuachia nchi mtu mwenye kufuata nyayo zake, hii kazi nzuri yote ya Magufuli itakuwa ni kazi bure! . Hivyo nimeshauri Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?
Kwa vile katiba sio Msahafu, 2025 tuibadili katiba Magufuli aendelee indefinitely kama Mugabe, mpaka atakapo choka kabisa na kuwa hawezi tena kwa incapacitation, au tumsubirie Mungu, au Tanzania sasa na sisi tuanze mtindo wa spotting na headhunting na kumfantia grooming huyo headhunted.
Kwa maoni yangu Makonda atatufaa sana kumpokea Magufuli, maana kiukweli huyu Jamaa atatufaa sana kwa sababu ana uthubutu mkubwa zaidi kuliko hata Magufuli. Makonda akimpokea kiukweli kabisa Tanzania itanyooka.
Magufuli pamoja na mazuri yake, naye kama binadamu pia ana madhaifu na mapungufu yake, Vivyo hivyo Makonda pia sio malaika naye ana mapungufu yake, moja ya mapungufu makubwa ya Makonda ni inferiority complex inayopelekea ku practice superiority complex na kujikuta ana over do bila kujijua.
Mfano ni jinsi anavyojikomba komba kwa rais Magufuli mpaka kupindukia, karibu kila jambo lazima amtaje Magufuli tena kwa majina yake yote manne na sifa zake zote nne "Rais Wetu Mpendwa Mheshimiwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli" (si mnajua watu wa Kanda yetu kwa kupenda masifa). Makonda lazima afike mahali aonyeshe anaweza kusimama on his own na sio kila wakati kutegemea apron strings za Magufuli.
2025 atatufaa sana. Kwa kuanzia 2020 akalichukue lile jimbo la yule mama pale, au akampumzishe Musukuma na kumshikisha adabu. Atashinda na kupewa moja ya portfolio zenye impact, ili 2025 ampokee Magufuli. Kitendo cha Magufuli kushika nchi, ni dalili ya Tanzania kutenda haki ya wengi wape, yaani wenye haki na uhalali wa kutawala nchi ni wale walio wengi. Baada ya Magufuli aje Makonda, na baada ya hapo kule kule mpaka na wengine wawe ni walio wengi! .
Makonda konyesha uwezo wa uthubutu, jee mnalionaje hili la kwanini asiwe Makonda kumpokea Magufuli?.
Kwa kwa wale mashabiki wa upinzani mtanisamehe bure, kwenye urais upinzani ni bado sana.
Paskali.
Uongozi ni kipawa toka kwa mungu...uongozi sio madarasa.Paskali ni wewe unayeongea haya au nani? Wana Dar sasa hivi wanaongozwa na darasa la saba unataka Nchi nzima iongozwe na Mtu wa aina hii tena. Huyo mwache ifike 2020 baba yake akitoka tu madarakani atakiona cha moto kwa makosa aliyofanya
KwlNimeipenda hii na mimi niliitaja hapa.
P
kusini mwa jangwa la saharaMayalla huwa ni watu wa asili ya mkoa gani?
Badala ya kujib hoja unakimbilia kujb vihojaSijui jina halisi la watu wenye hulka ya maneno kama ya kwako.!
Lakini nadhani huwa wana asili ya kuwa na chuki binafsi au hasira za kuathiriwa ama kuingiliwa kwa maslahi yao.
na mitandao ya kijamii ndio mahali pekee wanapoweza kutoa hasira zao kwa kujificha nyuma ya kibodi.!
Mbaya ya watu wa aina hii anaweza hata kuwa mkeo au sekretari wako!
SIJUI KWA NINI NIMEKIELEWA SANA KIPANDE HIKI.(si mnajua watu wa Kanda yetu kwa kupenda masifa)
Sijaona hoja kwenye bandiko lako zaidi ya kelele za maumivu..!Badala ya kujib hoja unakimbilia kujb vihoja