Baada ya bandari kubinafisishwa kwa miaka 100, ninamuomba radhi chifu Mangungo

Aje dp world au mwingine wakati tayari mshasainishana na dp world. Hio wizi unaousema haupo kwenye utendaji kwa wafanyakazi wa bandari tu hata kupata hao wawekezaji nao ni wizi. Unajua mchakato hadi kapatikanaa huyo dp world?

Pia Kama tatizo wote sisi ni wezi na wala rushwa unaamini vipi kwenye kupata hao wawekezaji hakuna rushwa?
CV yao inaonyesha, japo ni suala la bahati nasibu. Bandari yetu imelalamikiwa mpaka Rais Kagame, bandari yetu imetukosesha pesa nyingi pale wateja wa mataifa mengine wanapoamua kuikimbia na kwenda Kenya au Msumbiji. Tunarudia makosa yale yale kila mwaka na yanatugharimu kudorora kwa uchumi wetu.

Msikilize Msigwa ataongea leo usiku katika hii mitandao ya kisasa.
 
Swali dogo tu" je ninyi ndiyo mliowachagua wawe pale "? Si kuna mtu aliweka falisafa kuwa wakiwa peke yao mjengoni, ndipo mtaishi kama muko peponi? Na nchi itakua kama Newyork kuanzia chatu mpaka zenzi,na kuanzia kiaka mpaka mbaba bay?? Siku zijazo mjifunze kuweka wenu ili wakiwa palee juu walinde maslahi yenu.Ni hayo tu kwa leo !!
Hawakuchaguliwa kuwa pale .
 
Hii nchi ni kutafuta uraia wa binadamu wanaojitambuwa na si chadema wanaotetea washalamba asali
 
Nchi hii hakuna tunachoweza labda ufisadi. Nitajie kitu kimoja tu ambacho kama Mtanzania unaweza kusimama mbele ya dunia ukajipiga kifua kuwa tumeweza kukiendesha kwa ufanisi. Nipo nimekaa paleeee!

Yakianzishwa mashindano ya ufisadi tunaibuka videdea bila kupingwa hata Wanaija safari hii tunawakalisha dadeki!
Kichepuka na kulea michepuko
 
We are very sorry our ancestors, Chief Mangungo and your fellows. For sure today we have shown that we are extremely Bogus than you all. Our leaders are the most Bogus Ones
 
NATAMANI KUWAOMBA MSAMAHA KINA CHIEF MANGUNGO
____________________
Kuna nyakati huwa Natamani Sisi Watanzania Kuwaomba Msamaha mababu zetu akiwemo Chief Mangungo kwa KUWACHEKA na Kuwa na HASIRA nao kwa kuingia Mkataba wa Ulaghai na Dr. Carl Peters wa Ujerumani ambao ndio uliidhinisha mwanzo wa utawala wa Kikoloni Karne ya 19.

Ni wazi kabisa kizazi chetu cha sasa kila kinaporejea kusoma namna mababu zetu walivyoingizwa Kingi kwenye mikataba ya ulaghai hasa kwa kumrejea Chief Mangungo wa Msowero hucheka na kuona walikuwa wajinga kiasi gani mpaka wakubali?

Lakini mababu hawa kina Chief Mangungo hawakuwa na elimu yoyote, hawakuwa wametembea sehemu mbalimbali yaani hawakuwa na exposure, mababu hawa walidanganywa kwasababu hawakuwa na elimu yoyote ya darasani na hata kutia saini walitumia dole gumba huku wakiwa hawaelewi kilichoandikwa.

Kizazi hikihiki cha baada ya Ukoloni, kizazi chenye elimu, kizazi kinachojua lugha zote rasmi duniani, kizazi cha kidigitali, kinashindwa kujiuliza na kuhoji na kuwacheka viongozi wake ambao wamekuwa wakisaini mikataba ya miaka ya zaidi ya 100 ambayo ndani yake kuna athari za kizazi na kizazi. Mikataba inayokuwa inamnufaisha mwekezaji zaidi na kuwanyonya wazawa.

Mikataba inasainiwa na viongozi waliosoma na kusomeshwa kwa fedha za umma na wana Degree, Masters na PhD, mikataba wanayosaini ni ya kinyonyaji na ya hovyo lakini mikataba inatetewa kwamba wawekezaji hawa wataongeza ajira na kizazi cha Kisomi kinafurahia na kushangilia, hakuna kuhoji, hakuna kuuliza. Ajira zinazoongezwa ni za Malipo ya bora mkono uende kinywani. Ajira zisizo za ukombozi wa kiuchumi.

Nimebahatika kuona mahali kwa macho yangu, Kiwanda ambacho kipo Tanzania eneo kilipo kuna makubaliano ya kimkataba miaka 100 kinazalisha nguo ambazo zinakwenda kuuzwa nje. Nguo zimeandikwa Made in China ila zinatengenezwa hapa kwetu. Kina wafanyakazi zaidi ya 400 (Mia nne) Mishahara wanayolipwa take home Yaani baada ya makato yote ni Sh. 90,000TZS na masaa ya kufanya kazi ni saa mbili asubuhi hadi saa moja usiku, Jumatatu hadi Ijumaa na Jumamosi ni mwisho saa nane mchana. Makontena na makontena huingia na kutoka kila wiki. Je, huyu mwekezaji ana Faida gani kwa nchi yetu kama sio unyonyaji ni nini?
Hivi mbele ya kizazi chenye wasomi lukuki viongozi wanathubutu kusaini mkataba wa kuuza bandari ya Dares salaam kwa miaka mia moja?
Je, mkataba kama huu, ulisainiwa na Mangungo? Kwanini tuwacheke wazee wetu ambao hawakuwa na elimu yoyote?

Natamani Kuwaomba msamaha kina Chief Mangungo.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.View attachment 2648183
Kwa TAARIFA yako hapa inatafutwa pesa kuvunja legancy ya jiwe.
 
da inatia uchungu watu wana angalia masilahi yao binafsi badala ya kuangalia masilahi ya watanzania walio wengi.r.i.p mwenda zake john pombe magufuri.
Unamsifia aliyetuletea dhahama? Bila kuiba kura tungekuwa na bunge Bora sana sasa hivi!
 


"Makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Falme ya Dubai kama yalivyo kwenye mkataba huu hayakubaliki kwa sababu zifuatatazo:

(1) Makubaliano yataleta mgogoro kati ya wananchi wa Tanganyika na wa Zanzibar na hivyo kuendelea kuhatarisha Muungano.

(a) Wakati mkataba umetiwa ..saini na Waziri Makame Mnyaa Mbarawa, Mzanzibari, kwa mamlaka aliyokasimiwa na Rais Samia Suluh Hassan, Mzanzibari pia, mkataba wenyewe unahusu bandari zote zilizopo upande wa Tanganyika peke yake.

(b) Bandari zote za Zanzibar hazihusiki na mkataba, licha ya ukweli kwamba ..bandari ni mojawapo ya Mambo ya Muungano kwa mujibu wa Katiba ya sasa.

(c) Swali la wazi hapa ni, je, kama kweli mkataba huu una manufaa makubwa kwa nchi yetu kama inavyodaiwa na serikali na CCM na wapambe, kwa nini bandari za Zanzibar hazimo kwenye mkataba huu?

(d) Katika mazingira haya, Watanganyika wana haki ya kuhisi kwamba Wazanzibari hawa wawili wanagawa mali za Tanganyika kwa wageni kwa faida zao binafsi, wakati wakilinda mali zao wenyewe.

(e) Kuuruhusu mkataba huu kuendelea ni kuruhusu chuki dhidi ya Wazanzibari kuanza kujengeka miongoni mwa Watanganyika. Huku ni kuhatarisha mahusiano katika ya Wazanzibari na Watanganyika jambo ambalo linahatarisha Muungano moja kwa moja.

2. Mkataba huu unahatarisha usalama na uhuru wa nchi yetu moja kwa moja.

(a) Mkataba unakabidhi bandari zote za Tanganyika kwa DP World na washirika wao wa kibiashara kwa muda usiojulikana na kwa manufaa ambayo hayajaelezwa wazi wazi;

(b) DP World sio tu ni kampuni ya kibiashara, bali pia ni kampuni inayomilikiwa moja kwa moja na Serikali ya Falme ya Dubai na inawakilisha maslahi ya kibiashara na ya kisiasa ya Serikali hiyo.

(c) Endapo kutatokea kutoelewana kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ...ya Falme ya Dubai au Falme ya Nchi za Kiarabu (UAE), ambayo Dubai ni mojawapo ya nchi washirika maslahi ya Tanzania yatakuwa kwenye hatari kubwa na ya wazi.

(d) Mkataba unabadilisha au kukiuka sio tu Katiba na sheria za Tanzania, unaweza pia kupelekea kuvunja mikataba na ..sheria za kimataifa na hivyo kupelekea Tanzania kuwa na mahusiano mabaya na jumuiya ya kimataifa.

3. Mkataba utapelekea unyang'anyi mkubwa wa ardhi za wananchi utakaofanywa na serikali yetu ili kutekeleza masharti ya mkataba huu.

(a) Mkataba unataka serikali ya Tanzania kuipatia DP World na washirika wake ardhi yoyote watakayoihitaji kwa ajili ya shughuli zao;

..(b) Mkataba unataka serikali kuhakikisha kwamba ardhi hizo hazina mmiliki au mwenye maslahi mwingine yeyote kwenye ardhi hizo.

(c) Katika mazingira halisi ya nchi yetu ambako serikali imekuwa ndio tishio kubwa la haki za ardhi za wananchi wetu, mkataba huu utachochea ..migogoro mikubwa zaidi ya ardhi na uonevu mkubwa dhidi ya wananchi.

(d) Ardhi ambazo DP World watazikabidhiwa na serikali ya Tanzania chini ya mkataba huu hazina ukomo wa umiliki wake kwa sababu mkataba wenyewe hauna ukomo unaojulikana.

4. Mkataba huu unaendeleza utamaduni wa kuwapa wawekezaji wa nje manufaa makubwa ya kikodi na faida nyingine, ambao umesababisha taifa letu kupoteza utajiri na rasilimali zake asilia, kama vile madini, bila kupata manufaa yoyote ya maana.

(a) Chini ya mkataba huu, misamaha ya kodi na manufaa mengine kwa DP World yamewekewa ulinzi ule ule wa kutobadilishwa wakati wa kipindi chote cha mkataba, kama ilivyokuwa kwenye madini na sekta nyingine za uchumi wetu.

(b) Zaidi ya ahadi za jumla jumla za manufaa kwa nchi yetu, mkataba huu hauonyeshi manufaa ya wazi wazi kwa nchi yetu na kwa uchumi wetu." Mhe. Freeman Mbowe
 

Attachments

  • VID-20230607-WA0116.mp4
    7.8 MB
  • VID-20230607-WA0115.mp4
    4.1 MB


"Makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Falme ya Dubai kama yalivyo kwenye mkataba huu hayakubaliki kwa sababu zifuatatazo:

(1) Makubaliano yataleta mgogoro kati ya wananchi wa Tanganyika na wa Zanzibar na hivyo kuendelea kuhatarisha Muungano.

(a) Wakati mkataba umetiwa ..saini na Waziri Makame Mnyaa Mbarawa, Mzanzibari, kwa mamlaka aliyokasimiwa na Rais Samia Suluh Hassan, Mzanzibari pia, mkataba wenyewe unahusu bandari zote zilizopo upande wa Tanganyika peke yake.

(b) Bandari zote za Zanzibar hazihusiki na mkataba, licha ya ukweli kwamba ..bandari ni mojawapo ya Mambo ya Muungano kwa mujibu wa Katiba ya sasa.

(c) Swali la wazi hapa ni, je, kama kweli mkataba huu una manufaa makubwa kwa nchi yetu kama inavyodaiwa na serikali na CCM na wapambe, kwa nini bandari za Zanzibar hazimo kwenye mkataba huu?

(d) Katika mazingira haya, Watanganyika wana haki ya kuhisi kwamba Wazanzibari hawa wawili wanagawa mali za Tanganyika kwa wageni kwa faida zao binafsi, wakati wakilinda mali zao wenyewe.

(e) Kuuruhusu mkataba huu kuendelea ni kuruhusu chuki dhidi ya Wazanzibari kuanza kujengeka miongoni mwa Watanganyika. Huku ni kuhatarisha mahusiano katika ya Wazanzibari na Watanganyika jambo ambalo linahatarisha Muungano moja kwa moja.

2. Mkataba huu unahatarisha usalama na uhuru wa nchi yetu moja kwa moja.

(a) Mkataba unakabidhi bandari zote za Tanganyika kwa DP World na washirika wao wa kibiashara kwa muda usiojulikana na kwa manufaa ambayo hayajaelezwa wazi wazi;

(b) DP World sio tu ni kampuni ya kibiashara, bali pia ni kampuni inayomilikiwa moja kwa moja na Serikali ya Falme ya Dubai na inawakilisha maslahi ya kibiashara na ya kisiasa ya Serikali hiyo.

(c) Endapo kutatokea kutoelewana kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ...ya Falme ya Dubai au Falme ya Nchi za Kiarabu (UAE), ambayo Dubai ni mojawapo ya nchi washirika maslahi ya Tanzania yatakuwa kwenye hatari kubwa na ya wazi.

(d) Mkataba unabadilisha au kukiuka sio tu Katiba na sheria za Tanzania, unaweza pia kupelekea kuvunja mikataba na ..sheria za kimataifa na hivyo kupelekea Tanzania kuwa na mahusiano mabaya na jumuiya ya kimataifa.

3. Mkataba utapelekea unyang'anyi mkubwa wa ardhi za wananchi utakaofanywa na serikali yetu ili kutekeleza masharti ya mkataba huu.

(a) Mkataba unataka serikali ya Tanzania kuipatia DP World na washirika wake ardhi yoyote watakayoihitaji kwa ajili ya shughuli zao;

..(b) Mkataba unataka serikali kuhakikisha kwamba ardhi hizo hazina mmiliki au mwenye maslahi mwingine yeyote kwenye ardhi hizo.

(c) Katika mazingira halisi ya nchi yetu ambako serikali imekuwa ndio tishio kubwa la haki za ardhi za wananchi wetu, mkataba huu utachochea ..migogoro mikubwa zaidi ya ardhi na uonevu mkubwa dhidi ya wananchi.

(d) Ardhi ambazo DP World watazikabidhiwa na serikali ya Tanzania chini ya mkataba huu hazina ukomo wa umiliki wake kwa sababu mkataba wenyewe hauna ukomo unaojulikana.

4. Mkataba huu unaendeleza utamaduni wa kuwapa wawekezaji wa nje manufaa makubwa ya kikodi na faida nyingine, ambao umesababisha taifa letu kupoteza utajiri na rasilimali zake asilia, kama vile madini, bila kupata manufaa yoyote ya maana.

(a) Chini ya mkataba huu, misamaha ya kodi na manufaa mengine kwa DP World yamewekewa ulinzi ule ule wa kutobadilishwa wakati wa kipindi chote cha mkataba, kama ilivyokuwa kwenye madini na sekta nyingine za uchumi wetu.

(b) Zaidi ya ahadi za jumla jumla za manufaa kwa nchi yetu, mkataba huu hauonyeshi manufaa ya wazi wazi kwa nchi yetu na kwa uchumi wetu." Mhe. Freeman Mbowe
Naomba radhi
Screenshot_20230609-081153.jpg
IMG-20230609-WA0000.jpg
 
Sultan Mangungo anakumbukwa daima kwa kuuza nchi iliyokiuwa chini ya himaya yake kwa wakoloni wajerumani kwa mkataba wa maandishi!!

Wabunge wetu pia wameridhia mkataba wa maandishi wa kukabidhi bandari zetu zote ziwe chini ya waarabu jumla ili wazisimamie, waziendeshe na kuziongoza jumla. Kwa kuwa jambo hili liko kinyume na sheria za nchi yetu, wabunge wanataka kubadilisha sheria ili ziruhusu mgeni kuuziwa jumla rasilimali za nchi yetu!!

Kwa walichokifanya wabunge, kwa nini tuisiwabatize jina la MANGUNGOS wa kizazi kipya!!

Mkataba wa Mangungo na Wajerumani huu hapa:

1688979833481.png
 
Back
Top Bottom