Baa la njaa: Handeni maembe yawa chakula kikuu

Baa la njaa: Handeni maembe yawa chakula kikuu

Ninamuona DC Gondwe akikanusha Clouds 360 kwa kuuliza "kwenye ukame maembe yanaweza kukomaa".
Lakini ameshindwa kusema alitumia jitihada zipi kwa msimu wa kilimo uliopita katika kujihakikishia wilaya yake haina njaa.Aina hii ya viongozi ni hatari sana.
Anajificha kwenye kivuli chake. Je kipindi hiki si msimu wa maembe? Aache kufananisha maembe na mahindi. Sasa hao wananchi waliosema wanategemea kudra za mwenyezi Mungu walimaanisha nini? Siasa siasa hadi wananchi wanaenda kaburini
 
Ninamuona DC Gondwe akikanusha Clouds 360 kwa kuuliza "kwenye ukame maembe yanaweza kukomaa".
Lakini ameshindwa kusema alitumia jitihada zipi kwa msimu wa kilimo uliopita katika kujihakikishia wilaya yake haina njaa.Aina hii ya viongozi ni hatari sana.
Kati ya wazembe wachache sana wa karne hii. Analia?
 
Wewe ni mpumbavu wala siwezi kufanya argument na wewe, lini umesikia maembe, nanasi, parachichi yamekuwa chakula cha watu kushindia mchana na jioni?. Hivo vitu ni matunda yanayopaswa kuliwa baada ya mtu kula. Matunda kuwepo kwenye makundi ya vyakula vinavyotakiwa kiafya havifanyi viwe vyakula vya mtu kushindia. Inawezekana wewe ni mhaya au mchaga huko watu chakula kikuu ni ndizi, kanda ya ziwa ni ugali na wali kwa shinyanga na mwanza, huko nyanda za juu kusini ni wali, pwani ni wali. Hebu nambie maembe au nanasi ni chakula kikuu cha watu gani hapa tz?. Wewe mama yako amewahi kutenga maembe mezani kama chakula cha mchana na baadaye jioni na kesho ikawa hivyo?. Sipendagi matusi ila wewe naona una kichwa kikubwa kisicho na akili kama sufuria bila maji.

Umejieleza vizuri, umeonesha uwezo wako wa kufikiri na umeonesha pia uzoefu wako na zaidi ya yote umeonesha ugumu wako wa kupokea wazo jipya kutoka katika dunia tofauti ya tafakuri na ile uliyoizoea. Nafahaamu huwezi hata kuamini kuwa kuna jamii chakula chao kikuu ni maziwa kwa kuwa tangu utoto wewe maziwa umepikiwa na mama yako kwenye chai. Dunia hii tuliyomo inatuhitaji tufikirie nje ya box, kufikiri nje ya box nako si kazi ndogo, kunahitaji si kubadili fikra tu bali mpaka baadhi ya mila na desturi. Ikiwepo tabia ya kuvumilia wazo gumu usilokuwa na jibu lake badala ya kutumia matusi kujibu hoja
 
Tangu lini embe ndio chakula kamilifu kwa afya bora? Ni dhahiri uelewa wako wa kanuni za lishe bora ni ndogo. Elemika na wimbo huu mama chakula bora.
Listen and Download Mbaraka Mwinshehe - Mama Chakula Bora Mp3

Usibadili mada! Hatuzungumzii afya bora. Tunazungumzia njaa na chakula. Hata wali maharage si chakula kwa afya bora. Elewa muktadha kisha changia hoja. Kama ukiwa na tafsiri ya chakula ni nini itatusaidia katika mkanasha maana wengine wote wamegoma kutoa tafsiri ya chakula.
 
Nipo napiga Maembe hapa taratiiiibu...:

Cha msingi usikae mbali na choo tuu ila hayana shida kabisa..
 
Kichwa chako kazi yake ni nyele tu!

Asante sana, lakini kama ungetia japo hoja ya sentensi moja tu kuonesha kichwa changu kazi yake nywele ingependeza sana kuliko hivi ulivyofanya, umejionesha u mtupu kuliko mimi
 
Dunia hii tuliyomo inatuhitaji tufikirie nje ya box, kufikiri nje ya box nako si kazi ndogo, kunahitaji si kubadili fikra tu bali mpaka baadhi ya mila na desturi. Ikiwepo tabia ya kuvumilia wazo gumu usilokuwa na jibu lake badala ya kutumia matusi kujibu hoja[/QUOTE]

Naona umezungumzia mtu kuishi kwa maziwa pekee. Ila kila kitu kina umuhimi wake,siyo kwamba maziwa inakuwa kila kitu kwao.matunda yanaweza kutumika kama chakula ila siyo aina moja tu mda wote maana kila tunda lina kiburutisho chake na ndiyo maana Maulana akaweka matunda kwa msimu ili mwili uweze kuchukua kiburutisho chake huku ukisaidiwa na vyakula vingine.jaribu wewe kushinda unakula maembe kwa muda wa siku tatu halafu kapime uzito
 
Bado maana kila sehemu wanakula sana matunda kutokana na aina na msimu wenyewe ila haiondoi ukweli kuwa ndiyo kinakuwa chakula siku zote.hiyo inakuwa nyongeza tu katika maisha yao na kwa muda fulani
Safi kabisa, hakuna njaa nchini...tusijitakie laana. Kuna desturi ya baadhi ya watu hayo ndio maisha yao tangu zamani....hata Mimi nina ndugu wao maisha yao hawajawahi kunywa chai wanashindia matunda tangu enzi za NYERERE hadi Leo.....hata mvua ingenyesha bado watu wasingevuna saizi...mtoa mada naunga mikono hakuna njaa nchi ninayoishi.....kuna nchi zinanjaa tuache usaniii walahii!
 
Domokaya unaongea point sana hapo. Kweli maembe ghali Dsm na bei yake ni sawa nusu kilo ya Michele. Pia umesema kama wanamaembe wanakula basi hawana njaa..ni kweli wana matunda hivyo wanakula kupoza njaa. Na kwa maoni yako tukufu waweke chakula akiba (ambacho hawana kwa sasa) hivyo wasilie njaa wafanye kazi kama anavyoagiza mwenyekiti wetu. Na kwa kweli kama unakula na kushiba kabisa huwezi kumjua mwenye njaa ndio maana unwashangaa mwenye kula maembe wakati ugali upo kibao mtaani. It is obvious kuwa nyuma ya key board na kuandika kwa mzaha juu ya njaa sishangai kabisa.

Watu tunakimbia kujadili ukweli, kujadili kiini ili tujue tuna tatizo au hatuna. Tukipata tafsiri ya chakula ni nini? Ukosefu wa chakula ni nini? Kiwango gani cha ukosefu wa chakula kinatafiriwa kama baa la njaa. Je ni ukosefu wa kaya ngapi? Je ni uwezo wa kununua au kutokuwepo kabisa hata hicho cha kununua? Inawezekana kabisa kaya moja au mbili za walevi wakakosa chakula wakala maembe kwa ulevi wa wakuu wao wa kaya, je hawa nao wana njaa au wana baa la njaa? Tuache unafiki, tuache kufikiri kwa hisia, tu u face ukweli. Siasa siasa za kitoto hizi hazitupeleki popote
 
Dunia hii tuliyomo inatuhitaji tufikirie nje ya box, kufikiri nje ya box nako si kazi ndogo, kunahitaji si kubadili fikra tu bali mpaka baadhi ya mila na desturi. Ikiwepo tabia ya kuvumilia wazo gumu usilokuwa na jibu lake badala ya kutumia matusi kujibu hoja

Naona umezungumzia mtu kuishi kwa maziwa pekee. Ila kila kitu kina umuhimi wake,siyo kwamba maziwa inakuwa kila kitu kwao.matunda yanaweza kutumika kama chakula ila siyo aina moja tu mda wote maana kila tunda lina kiburutisho chake na ndiyo maana Maulana akaweka matunda kwa msimu ili mwili uweze kuchukua kiburutisho chake huku ukisaidiwa na vyakula vingine.jaribu wewe kushinda unakula maembe kwa muda wa siku tatu halafu kapime uzito[/QUOTE]

Uwezo wako wakufikiri ndio umeishia hapa?
 
Soma tena na chukua muda utaelewa nilichokuwa na maanisha
 
Kama Mkuu wa Wilaya analia kwa kuona watu wakila maembe huyo hafai kuwa Mkuu wa Wilaya. Watanzania umefika wakati wa kuacha kukariri, nani kasema maembe hayafai kuwa chakula? Tena mimi naona tungekuwa na vionzozi wenye maono wangehamasisha watu wale maembe kipindi hiki cha msimu wa maembe kwa wingi huku wakihifadhi chakula cha aina nyingine kwa vile maembe hayahifadhiki kwa tekinolojia tuliyo nayo mpaka sasa. Tuna tatizo kubwa la kufikiri. Taarifa kwa wajinga wenzangu, maembe ni chakula ghali dar kuliko hata huo mchele.
Wengine tungewashauri mrudi SHULE tu mkasome upya, tena sio mbali, shule ya msingi tu. Kuna somo nilisoma linaitwa Sayansi kimu (sina hakika kama bado lipo) na wewe ukasome hilo, naona Biology itakua kubwa mno kwako, soma tu Sayansi kimu inakutosha; huko utakutana na vyakula vinaitwa Hamilojo, protein, vitaminis, madini, wanga nk and then kila chakula utafundishwa kina fanya nini mwilini. Nakutakia shule njema.
 
Jamaa naona kibarua chake kinakwenda kuota nyasi, yaani analia wananchi wake kukosa chakula???
 
Handeni baa la Njaa ni kubwa sana ! Kwanza hata hayo maembe Kwa sasa naweza kusema hakuna tena msimu umeishia! Hali siyo nzuri sijui hadi itolewe taarifa ya Mtu au Watu kufa Njaa Ndiyo itaanza kueleweka?! Mwenyezi Mungu azidi kuepusha mbali lakini tahadhari inahitajika haraka! DC alishaambiwa Na madiwani kwenye vikao vya halmashauri kuwa hali siyo nzuri lakini jamaa akawa Kama anasita sasa Kama amejionea mwenyewe basi ni vizuri zaidi! Ukame ume jitokeza Kwa mfululizo hata mboga za majani Zimekuwa zikitoka mikoani imagine
 
Kama Mkuu wa Wilaya analia kwa kuona watu wakila maembe huyo hafai kuwa Mkuu wa Wilaya. Watanzania umefika wakati wa kuacha kukariri, nani kasema maembe hayafai kuwa chakula? Tena mimi naona tungekuwa na vionzozi wenye maono wangehamasisha watu wale maembe kipindi hiki cha msimu wa maembe kwa wingi huku wakihifadhi chakula cha aina nyingine kwa vile maembe hayahifadhiki kwa tekinolojia tuliyo nayo mpaka sasa. Tuna tatizo kubwa la kufikiri. Taarifa kwa wajinga wenzangu, maembe ni chakula ghali dar kuliko hata huo mchele.
We ni mpuuzi sana..unaweza shindia maembe wewe
 
Kama Mkuu wa Wilaya analia kwa kuona watu wakila maembe huyo hafai kuwa Mkuu wa Wilaya. Watanzania umefika wakati wa kuacha kukariri, nani kasema maembe hayafai kuwa chakula? Tena mimi naona tungekuwa na vionzozi wenye maono wangehamasisha watu wale maembe kipindi hiki cha msimu wa maembe kwa wingi huku wakihifadhi chakula cha aina nyingine kwa vile maembe hayahifadhiki kwa tekinolojia tuliyo nayo mpaka sasa. Tuna tatizo kubwa la kufikiri. Taarifa kwa wajinga wenzangu, maembe ni chakula ghali dar kuliko hata huo mchele.
Wacha porojo wewe, hivi ulishasikia wapi watu wanashindia maembe kama mlo wa siku? Unaweza kula maembe kila siku kwa wiki nzima au mwezi mzima wewe? Ukweli ubaki tu kwamba nchi inakabiliwa na baa la njaa, ni mpuuzi ndo anaweza kusema hali iko shwari. Kuna mtu anavuliwa nguo na maaskofu sijui atajificha wapi? Hata kama una maembe lazima ugali uwepo, unalijua tatizo linaloitwa Hypervitaminosis? Msitake kutuletea matatizo kwa ujinga wenu, tathmini ifanyike ili kubaini nani anastahili kusaidiwa na nani anastahili kuuziwa chakula cha msaada. Wenzake wenye akili wakati wa mavuno walikuwa wanakusanya chakula na kuweka kwenye maghala ya Taifa, sasa kama yeye hakufanya hilo ajitathmini kama anastahili kuendekea kuitwa Rais wa nchi! Kauli za kuwakejeli wananchi kwa kweli hazijengi, zinazidi kuwaweka kwenye wakati mgumu wananchi kwamba waendelee kukuheshimu au wakupuuze? TIME WILL TELL THE TRUTH!!
 
Back
Top Bottom