Azimio La Arusha: Why We Were Dead Wrong!

Apr 27, 2006
26,588
10,375
Well, heshima mbele sana JF,

- Ninaomba kusema tena na tena, we were Dead wrong na idea za Azimio La Arusha, infact ndilo limetufikisha hapa tulipo yaani tumekwama hili taifa, hatujui tunakokwenda wala tulikotoka. Halafu wanatokea wasomi wanaodai eti turudi kwenye Azimio, hilo Azimio limetushinda mwanzoni kwa nini kuna wanaoamini tutaliweza sasa?

- Recently, nimeona wale wengi walioachwa kwenye uongozi wa juu yaani kwenye mlo, wakililia Azimio, halafu ninachukizwa sana ninapoona media inawapa free lunch hawa waliokosa mlo, sijawahi kuwasikia wakisema Azimio liliwahi kumfunga kiongozi gani wa juu mwizi, sijawasikia wakisema Azimio lilifanya nini cha maaana mpaka wanalilia!

- Mwalimu, yes was the greatest ever, lakini Mwalimu alikuwa na mapungufu makubwa mawili, hakujua;- !. Uchumi 2. Sheria, hivi vitu viwili Mwalimu simply hakuvijua kama alivijiua basi hakuvitilia maanani, na ndivyo vinavyolitafuna taifa letu sasa akiwa hayupo!

- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!

RESPECT PEOPLE!

Mr. Willie @DSM City!
 
Heshima Kwako baharia 1 Kwako wewe azimio ni libaya kwani kufa kwa azimio la arusha baba yako alinufaika kufa kwake na alishiriki kuliua hilo azimio na ndio maana mwl alipo wauliza paolo paolo na wewe ulikuwapo basi halitawaacha salama na ni kweli kwani wameweza kukopa pesa kwa kina jituu petel ili waweze gombea urais na walikosa kama sio ukweli muulizee Anne malechela atakueleza usijaribu kuzungumzia azimio la arusha lilikuwa na miiko ya uongozi kwa waliofaidika watalipinga
 
William,

..Azimio la Arusha ninavyoelewa mimi lilikuwa na sehemu mbili.

..sehemu ya kwanza, ilihusu masuala ya siasa za Ujamaa, pamoja uendeshaji na umiliki wa uchumi wetu.

..sehemu ya pili, ilihusiana na masuala ya utawala wa sheria na miiko ya uongozi.

..tunaweza kukwepa sehemu ya kwanza, lakini hii ya pili hatuwezi kuikwepa.

..hata kama tukizamia mia kwa moja kwenye ubepari lazima utawala wa sheria na miiko ya uongozi iwepo.

..hata USA ambako umeishi kwa miaka mingi wana miiko ya uongozi, wenyewe wanasema conflict of interests.

..mwisho, practically tumekuwa tukiendesha nchi kibepari, what has not happened is CCM declaring kwamba tumekuwa tukifuata mfumo wa Kibepari tangu Mwalimu aondoke madarakani.

NB:

..mbona mimi naona hawa viongozi baada ya Mwalimu nao hawajui sheria wala uchumi??

..Nyerere alikuwa hajui sheria lakini hata mara moja hatukusikia serikali yake imejitumbukiza kwenye mikataba ya hovyo-hovyo kama Richmond, au amejimilikisha mgodi wa madini.
 
It is a good thing wewe hukuchaguliwa eala. Ccm ina tatizo kubwa sana sasa,tatizo la kuiondoa dhana kwamba haiwajali wanyonge,haiwatumikii wanyonge,ccm ni leftist party,inajulikana abroad as 'tanzania' ruling revolutionary party' sasa we unataka ccm ivunje original contract na wananchi. Ccm ni leftist party,kama labour party au democrats,mwana ccm akipendekeza righist policies,lazima aombwe kujieleza kwa ufasaha zaidi.
 
William,

..Azimio la Arusha ninavyoelewa mimi lilikuwa na sehemu mbili.

..sehemu ya kwanza, ilihusu masuala ya siasa za Ujamaa, pamoja uendeshaji na umiliki wa uchumi wetu.

..sehemu ya pili, ilihusiana na masuala ya utawala wa sheria na miiko ya uongozi.

..tunaweza kukwepa sehemu ya kwanza, lakini hii ya pili hatuwezi kuikwepa.

..hata kama tukizamia mia kwa moja kwenye ubepari lazima utawala wa sheria na miiko ya uongozi iwepo.

..hata USA ambako umeishi kwa miaka mingi wana miiko ya uongozi, wenyewe wanasema conflict of interests.

..mwisho, practically tumekuwa tukiendesha nchi kibepari, what has not happened is CCM declaring kwamba tumekuwa tukifuata mfumo wa Kibepari tangu Mwalimu aondoke madarakani.

NB:

..mbona mimi naona hawa viongozi baada ya Mwalimu nao hawajui sheria wala uchumi??

..Nyerere alikuwa hajui sheria lakini hata mara moja hatukusikia serikali yake imejitumbukiza kwenye mikataba ya hovyo-hovyo kama Richmond, au amejimilikisha mgodi wa madini.

- Joka Kuu, heshima yako sana mkuu, mataifa yote yaliyoendelea Duniani hayaishi kwa miiko ya uongozi, yanaishi kwa utawala unaoheshimu sheria tu! Ukishaanza maneno ya miiiko automatically, unatoka kwenye mkondo wa sheria na ku-establish alternative ya sheria matokeo yake ndiop haya tumekwama, kiongozi mwizi kwenda kujadiliwa kwenye vikao vya chama, nonsense!

- Mawaziri wezi, mnaenda kubishana bungeni, bdala ya kwenda kwenye sheria, Mataifa yote yaliyoendelea Duniani, kamati yao ya bunge inaangalia ishu ikiona waziri ni mwizi anaitwa mbele ya kamati na kuhojiwa, akishindwa kuridhisha kamati hoja inapelekwa kwenye full bunge, inapigwa kura ili aende mahakamani au aadhibishwe na kamati ya bunge, kama kura hazitoshi kama ilivyo bunge letu ni kazi ya upinzani kuichukua kesi kwa wananchi! Wananchi wataamua tena in a very good way kwa kuwafundisha viongozi kwenye kura,

- Sisi tumekalia kulia lia tu, Azimio! hivi lile Azimio gani lililokuwa dead hata kabla halijaanza?

Willie!
 
Good analysis.Inashangaza watu kufikiria kurudi kwenye azimio la Arusha.

- Sometimes ninashangazwa sana na hata Viongozi wa upinzani kuwasikia wakililia Azimio la Arusha, please hawa wanatakiwa kukamatwa na kuchapwa viboko hadharani, ni ma-sell out, hakuna Azimio hapa, kinachotakiwa ni uchumi na sheria tu, wala hakuna miiiko ya uongozi, sheria kwanza!

Willie!
 
Well, heshima mbele sana JF,

- Ninaomba kusema tena na tena, we were Dead wrong na idea za Azimio La Arusha, infact ndilo limetufikisha hapa tulipo yaani tumekwama hili taifa, hatujui tunakokwenda wala tulikotoka. Halafu wanatokea wasomi wanaodai eti turudi kwenye Azimio, hilo Azimio limetushinda mwanzoni kwa nini kuna wanaoamini tutaliweza sasa?

- Recently, nimeona wale wengi walioachwa kwenye uongozi wa juu yaani kwenye mlo, wakililia Azimio, halafu ninachukizwa sana ninapoona media inawapa free lunch hawa waliokosa mlo, sijawahi kuwasikia wakisema Azimio liliwahi kumfunga kiongozi gani wa juu mwizi, sijawasikia wakisema Azimio lilifanya nini cha maaana mpaka wanalilia!

- Mwalimu, yes was the greatest ever, lakini Mwalimu alikuwa na mapungufu makubwa mawili, hakujua;- !. Uchumi 2. Sheria, hivi vitu viwili Mwalimu simply hakuvijua kama alivijiua basi hakuvitilia maanani, na ndivyo vinavyolitafuna taifa letu sasa akiwa hayupo!

- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!

RESPECT PEOPLE!

Mr. Willie @DSM City!
Mkuu wangu baharia mbona unaturudisha nyuma kiasi hicho.. Wewe Azimio la Arusha ndilo limekusomesha bure na ukajisifia kwa kumpa sifa zote Nyerere leo unaliponda.. Nyerere hakujuja Uchumi vipi?..Ni Azimnio la Arusha lilojenga reli ya Tazara, Azimio la Arusaha lkililojenga viwanga vya matairi General tyre, UFI, viwanda vya nguo, saruji, nguvu za umeme ukayarudi disco la Mbowe hata siku moja umeme haukukatika, leo unaliponda wakati ndio kwanza tulijenga vitu hivyo tukashindwa kuviendesha sisi wenyewe kama walivyoshindwa China na Russia..

Au mwenzetu una maana tofauti ya Uchumi? maana kuwa na wazo zuri ukashindwa kufanikiwa haina maana hata wazo lenyewe halikuwa na maana. Leo hii umetaka kugombea Ubunge wa EA na ukashindwa je tuseme wewe huna maana tena kwa sababu umeshindwa huko..Tafadhali mkuu wangu Azimio la Arusha lilikuwa na mapungufu yake kimfumo hasa pale tulipochagua serikali kumiliki uchumi lakini haina maana hakuna kitu hicho ktk somo la Uchumi. Asiyejua Uchumi atafanya jambo ambalo halipo ktk somo la Uchumi lakini ukifanya ikashindikana haina maana hujui uchumi..

Na unaposungumzia Sheria ni sheria gani?..ati kwa nini Nyerere aliendelea kuwatumia viongozi wabovu, hivi nikuulize tulikuwa na wasomi wangapi? angembadilisha mzee Malecela akamweka nani ikiwa wote walikuwa wabovu. Wewe hapo ulipo nambie mtu hata mmoja ambaye wewe ulimwoina kingozi mzuri Nyerere angemtumia na hakumtumia. Haya leo hii pamoja na kuwa nao kibao na tumebadilisha mfumo mbona ndio kwanza tunatokomea zaidi shimoni tuna excuse gani?
 
kwa upande wangu naona kuna mambo ambayo hayakutakiwa kutupwa kabisa,
kwa mfano

1. Kiongozi wa TANU au wa Serikali sharti awe mkulima au
mfanyakazi na asishiriki katika jambo lo lote la kibepari au
kikabaila.
2. Asiwe na hisa katika makampuni yo yote.
3. Asiwe mkurugenzi katika kampuni ya kikabaila au kibepari.
4. Asiwe na mishahara miwili au zaidi
5. Asiwe na nyumba ya kupangisha.

kuna baadhi ya mambo yaliwekwa hapo ili kuweza kupunguza ama kuondoa hii tuitayo ufisadi kwa sasa,kwani unapokuwa na hisa ktk kampuni itakulazima kuipendelea kampuni hiyo pindi itakapo jiingiza ktk maswala ya tenda

kwa hiyo nyerere hakuwa kicha kusema hayo juu,alielewa tu kuwa baadhi ya viongozi wetu si wazarendo na unajionea mwenyewe


Lakini pia ni lazima serikali imiliki njia kuu za uchumi,mfano viwanda,madini,kilimo,usafirishaji,bandari na mambo mengine,lakini kwa sasa TUMEBINAFSISHA NJIA ZOTE ZA UCHUMI .

(h) Kwamba ili kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakwenda
sawa Serikali lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia
muhimu za kuukuza uchumi;
na
(i) Kwamba ni wajibu wa Serikali, ambayo ni watu wenyewe,
kuingilia kati kwa vitendo maisha ya uchumi ya Taifa ili
kuhakikisha usitawi wa raia wote na kuzuia mtu kumnyonya
mtu mwingine au kikundi kimoja kunyonya kikundi kingine

na kuzuia limbikizo la utajiri kufikia kiasi ambacho hakipatani
na siasa ya watu wote kuwa sawa.
 
Mkuu William Malecela,

Unaposema Azimio la Arusha ndio kiini cha matatizo yanayotukabili leo kama taifa, una maana gani hasa, kwani azimio la arusha per se ni pana sana. Ungefunguka kidogo tungeweza pata mjadala mzuri zaidi.
 
- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!

RESPECT PEOPLE!

Mr. Willie @DSM City!

Sasa mbona unalijadili?
 
William,

..Azimio la Arusha ninavyoelewa mimi lilikuwa na sehemu mbili.

..sehemu ya kwanza, ilihusu masuala ya siasa za Ujamaa, pamoja uendeshaji na umiliki wa uchumi wetu.

..sehemu ya pili, ilihusiana na masuala ya utawala wa sheria na miiko ya uongozi.

..tunaweza kukwepa sehemu ya kwanza, lakini hii ya pili hatuwezi kuikwepa.

..hata kama tukizamia mia kwa moja kwenye ubepari lazima utawala wa sheria na miiko ya uongozi iwepo.

..hata USA ambako umeishi kwa miaka mingi wana miiko ya uongozi, wenyewe wanasema conflict of interests.

..mwisho, practically tumekuwa tukiendesha nchi kibepari, what has not happened is CCM declaring kwamba tumekuwa tukifuata mfumo wa Kibepari tangu Mwalimu aondoke madarakani.

NB:

..mbona mimi naona hawa viongozi baada ya Mwalimu nao hawajui sheria wala uchumi??

..Nyerere alikuwa hajui sheria lakini hata mara moja hatukusikia serikali yake imejitumbukiza kwenye mikataba ya hovyo-hovyo kama Richmond, au amejimilikisha mgodi wa madini.
JokaKuu Hiyo sehemu ya pili!!

Ninaamini mtu ambaye hatambui thamani ya uongozi wenye kusimamia maadili, amepotoka kabisa! Nani haoni kuwa taifa letu kwa sasa linaangamia just becaus eof that? !!
 
Last edited by a moderator:
Tatizo kwenye thread yake hauingii tena baada ya kushushiwa nondo za ukweli.

Azimio ccm wakishirikiana na baba yako walishaliua miaka ya 70 unataka tulijadili lipi?
Kuturudisha kulijadili azimio ambalo baba yako alishiriki kuliua ni kutupotosha tusijadili current issues.

- Mkuu hapa hakuna baba yako wala wa mtu yoyote, the agenda ni uozo wa Azimio la Arusha, we were dead wrong na Mungu awajalie wale wote walioliua, maana ndilo limetufikisha hapa, Taifa limekwama hatujui tunatoka wapi, tunakwenda wapi? Ukiwauliza viongozi wa juu hakuna mwenye jawabu, na huku kwetu ndio kabisaa great thinker anaongelea miiiko ya uongozi, mtumzima na akili timammu anaongelea miiiko ya uongozi!

- MUNGU IBARIKI TANZANIA, NA HAWA MASKINI WAKO WA AKILI NA KUTOFIKIRIA SAWA SAWA, wanaolilia miiiko badala ya sheria!


William.
 
- Joka Kuu, heshima yako sana mkuu, mataifa yote yaliyoendelea Duniani hayaishi kwa miiko ya uongozi, yanaishi kwa utawala unaoheshimu sheria tu! Ukishaanza maneno ya miiiko automatically, unatoka kwenye mkondo wa sheria na ku-establish alternative ya sheria matokeo yake ndiop haya tumekwama, kiongozi mwizi kwenda kujadiliwa kwenye vikao vya chama, nonsense!

- Mawaziri wezi, mnaenda kubishana bungeni, bdala ya kwenda kwenye sheria, Mataifa yote yaliyoendelea Duniani, kamati yao ya bunge inaangalia ishu ikiona waziri ni mwizi anaitwa mbele ya kamati na kuhojiwa, akishindwa kuridhisha kamati hoja inapelekwa kwenye full bunge, inapigwa kura ili aende mahakamani au aadhibishwe na kamati ya bunge, kama kura hazitoshi kama ilivyo bunge letu ni kazi ya upinzani kuichukua kesi kwa wananchi! Wananchi wataamua tena in a very good way kwa kuwafundisha viongozi kwenye kura,

- Sisi tumekalia kulia lia tu, Azimio! hivi lile Azimio gani lililokuwa dead hata kabla halijaanza?

Willie!

William,

..basically tunazungumza kitu kilekile.

..miiko ya uongozi na rule on law inatakiwa isimikwe kwenye katiba yetu, na kusimamiwa na vyombo vya dola na mahakama zetu.

..ni kweli kabisa unavyosema kiongozi au mwanasiasa akivunja sheria au akikiuka kiapo chake basi anapaswa kushughulikiwa na vyombo vya dola pamoja na mahakama.

..yaani haya masuala ya richmond,dowans, kiwira, etc etc, wahusika walipaswa kunyakuliwa na Director wa Criminal Investigation, na siyo kujadiliwa kwenye CCM-NEC.
 
- Mkuu hapa hakuna baba yako wala wa mtu yoyote, the agenda ni uozo wa Azimio la Arusha, we were dead wrong na Mungu awajalie wale wote walioliua, maana ndilo limetufikisha hapa, Taifa limekwama hatujui tunatoka wapi, tunakwenda wapi? Ukiwauliza viongozi wa juu hakuna mwenye jawabu, na huku kwetu ndio kabisaa great thinker anaongelea miiiko ya uongozi, mtumzima na akili timammu anaongelea miiiko ya uongozi!

- MUNGU IBARIKI TANZANIA, NA HAWA MASKINI WAKO WA AKILI NA KUTOFIKIRIA SAWA SAWA, wanaolilia miiiko badala ya sheria!


William.
Leo umeamka vipi hasa, Sasa utaweza vipi kuwa na sheria ikiwa huna miiko?
 
... Hakuna kitu rahisi na kizuri kama kukosoa. Kila mtu anaweza kukosoa fikra za yeyote. Kazi nzito ni kuweza kujenga fikra. Willy, msimamo wako juu ya mwalimu upo wazi sana. Hapo awali nilidhani una fikra mbadala za kututoa hapa tulipo, nilidhani una maono-nilijua tuna watanzania vichwa wapo nje ya nchi! Hivi karibuni nilipata nafasi ya kujua jinsi ulivyo mweupe baada ya kukusikia ukiongea redio Uhuru wakati wa kampeni za EALA!

Itoshe tu kusema kwamba kwa mwanasiasa mchanga kama wewe, nafasi ya pekee ya angalau "kuonekana" ktk medani za siasa ni kumponda Nyerere, tena bila hoja. Ilitakiwa utuambie kila sera ya Azimio la Arusha na jinsi kila sera ilivyoshindwa kutuletea maendeleo. Sio kuja hapa na "blanket allegation"!
 
Azimio la Arusha was a living document iliyobeba dira na 'definition' ya taifa tulilokuwa tunataka kujenga. Iliweka misingi na taratibu za kiutawala pamoja na mahusiaono ya kijamii. Azimio la Arusha lilibeba 'mipaka' na 'barabara' za kupita ili tupate aina ya taifa tulilotaka.

Kwa mtazamo wangu a living document inaweza kufanyiwa update kutokana na mabaliko ya lazima ambayo yanaigusa jamii husika. Lakini sisi tulilifuta Azimio la Arusha kimoja bila mbadala ya maana! Sasa hivi William unaweza kusema Tanzania ni nchi ya aina? Au tuna-aspire kuwa Taifa gani? Na kama unajua aina ya taifa linalojengwa kwa sasa nini misingi ya ujenzi huo?

Ni rahisi sana kuona Azimio la Arusha si chochote kama hujalisoma kwa makini na kuelewa logic yake. Na kwa bahati mbaya au nzuri sasa hivi tunaishi post-Azimio la Arusha, hivyo tunaweza kutofautisha kabisa pande mbili hizi za shilingi. Kulaumu kwamba hali tuliyonayo imesababishwa na Azimio la Arusha ni dalili ya uelewa mdogo wa Azimio lenyewe. With Azimio la Arusha tusengekuwa tunamumunya maneno kuhusu mawaziri wananen waliovurunda!

Azimio la Arusha lilikuwa linahimiza kutafuta majibu ya matatizo yetu kama nchi from within na sio ku-import solutions! Hakuna nchi iliyoendelea kwa kutegemea wawekezeji huku asilimia kubwa ya population yake ikiwa iko outside the system! CCM ya sasa hawatataka kulisikia Azimio la Arusha kwa sababu wamejipa 'hati miliki' ya nchi. Watalisema vibaya kwa ujumla wake bila kuangalia kipengele kimoja kimoja na kufanya marekebisho pale inapobidi. Wanafaidika moja kwa moja na hii nyumba isiyokuwa na msingi na incase inaanguka tayari wameshajiwekea mpango wa dharura kama kuwa na account visiwa ya Jersey huko Uingereza!.
 
- Mkuu hapa hakuna baba yako wala wa mtu yoyote, the agenda ni uozo wa Azimio la Arusha, we were dead wrong na Mungu awajalie wale wote walioliua, maana ndilo limetufikisha hapa, Taifa limekwama hatujui tunatoka wapi, tunakwenda wapi? Ukiwauliza viongozi wa juu hakuna mwenye jawabu, na huku kwetu ndio kabisaa great thinker anaongelea miiiko ya uongozi, mtumzima na akili timammu anaongelea miiiko ya uongozi!

- MUNGU IBARIKI TANZANIA, NA HAWA MASKINI WAKO WA AKILI NA KUTOFIKIRIA SAWA SAWA, wanaolilia miiiko badala ya sheria!


William.

mimi sikuelewi kabisa ndugu yangu

azimio hilo ndilo lililojenga viwanda vyote hapa Tanzania na njia kuu za usafirishaji,lakini pia Azimio hilo ndilo lililo jenga njia kuu za kuzalisha umeme ,

cha kushangaza viwanda vyote,reli na mashamba yaliyo anzishwa na azimio hilo leo hii hayapo,viwanda vimeuzwa na naomba uelewe kuwa,hakuna nchi iliyoendelea pasi kuwa na viwanda inavyo vimiliki yenyewe.

angalia uchina,mambo mengi tunayoyakataa ndani ya azimio la arusha ndiyo yanayotumika uchina

mfano
-serikali kujihusija ktk kumiliki njia kuu za uchumi-wachina hawakuuza viwanda,waliandaa maeneo ya ubinafsisha na serikali ilishiriki kumiliki njia kuu za uchumi na haikuwaachia wawekezaji

angalia viwanda,mashirika ya simu,njia za usafirishaji na hata uchimbaji wa madini kule inner mongoria hakuna wawekezaji ni serikali ndiyo inayomiliki njia kuu za uchumi

mpaka leo serikali haijaweza kuanzisha vyanzo vipya vya kuzarisha umeme ni vilevile vya baba wa taifa


kiukweli azimio la arusha lilikuwa na mambo mengi mazuri,ingawaje hatukutaka kuyafanyia kazi
 
Back
Top Bottom