Kuna jirani yangu ana mtoto anasoma Atlas ya Ubungo darasa la sita au la saba, cha ajabu mwanafunzi alikuwa anchukua simu ya dada wa kazi anaongea nayo sana hasa usiku maana analala chumba kimoja na huyo dada, alikuwa anaongea issues za mapenzi. Dada alipombana kwamba anaongea na nani akasema no dereva wao wa gari ya shule. Inaonekana dereva alianza kumuandaa yule mtoto maana ni mrefu kidogo na matiti yashaanza kuchomoza. Kwakweli sikuwa na cha kuongea ila nilimwambia tu huyo dada yao wa kazi amkanye na kumtishia kwamba atamwambia mama yake. Kama wenye shule atapitia jukwaa hili ni vzr akamkanya dereva wake anayechukua watoto wa TABATA KISIWANI ( MAENEO YA MWANANCHI COMMUNICATIONS). Aache hiyo tabia ya kitongoza kitoto cha jirani yangu.
NB: Hii habari niliipata nilipoenda dsm nikitokea Mtwara ,kwani huyo dada alimwambia make l wangu ambaye bado anaishi huko.