Atlas Primary School - Madale, Dar

Atlas Primary School - Madale, Dar

Ifungiwe haraka. Hii ni Serikali ya wanyonge, wababe tutalala nao mbele kwa mbele ili waishi kama mashetani.
 
Tupeane uzoefu wa shule tofauti ili tusifanye makosa ya kupeleka mtoto shule kwa kuambiwa na rafiki/ndugu kumbe kimeo ....
Tuwapende watoto, iko Mabwe pande -Bunju. Ni shule nzuri pia. Kijana wangu amemaliza hapo last year.
 
Huko mtaani kwenu hakuna shule za msingi za umma????? Mtutolee uchuro sisi...
 
Halafu walivyo watu wa ajabu siku ukienda kumhamisha mtoto pale wanakupeleka kwa mwalimu wao sijui ni mshauri au ni mwalimu wa taalum.Anaanza kukuhoji kwa unyenyekevu ooohhh tatizo liko wapi,ukishamwelezea anakwambia tupe muda tutajirekebisha na umwache mtoto aendelee kusoma hapahapa.Mimi nikawaambia jirekebisheni kwanza mkikaa sawa nitamrudisha mtoto hapa,basi toka mwezi wa tisa mwaka huu mpaka leo hawataki kunipa namba ya uhamisho wananizungusha mara jina la mtoto limekosewa,mara mwalimu anayeshughulikia hayupo yaani ili mradi ni karaha tu
Nenda Takukuru..!!!
 
Suala la maji salama ya kunywa watoto wa bweni pale shuleni ni pasua kichwa. Watoto wanakunywa maji ya bomba. Kichekesho maji salama yanaletwa siku ya visting day tu. Baada ya hapo utaratibu ule ule unaendelea.

Kwenye vyoo vya watoto hakuna mabomba ya maji. watoto inabidi wateke kwenye ndoo zao za lita 10 kila mmoja maji hayo hayo mtoto atumie kuoga na chooni na hii mbaya zaidi nyakati za uck ndoo zinakuwa tupu. Baada ya mtoto kujisaidia hakuna sehemu ya kinawa mikono.
 
Vipi kuhusu King's ?
Nimeona wazazi walio na watoto King's wanawatoa wanawapeleka atlas....kwa kifupi madale na Goba bado hakuna shule nzuri.....ikitokea mtu akafungua shule nzuri kimazingira na kitaaluma atapata sana hela.
 
Tupeane uzoefu wa shule tofauti ili tusifanye makosa ya kupeleka mtoto shule kwa kuambiwa na rafiki/ndugu kumbe kimeo ....
Ingependeza ungeanzisha uzi wa hiyo mada.
 
Sio kweli, kimkoa Hazina iko juu, na hiyo ya Madale ndio kabisaa inapitwa na shule kibao kama Lieberman, Rightway etc
Rightway ipo maeneo yapi? lieberman huwa wana primary? Naijua tu ile pale juu Goba ya sec.
 
Rightway ipo maeneo yapi? lieberman huwa wana primary? Naijua tu ile pale juu Goba ya sec.
Rightway ipo Mbezi Makonde na Lieberman ya primary ipo Mbezi pia maeneo hayo hayo kwa ndani kidogo.
 
Kwaio ni heri uhatarishe maisha yake kisa atapoteza marafiki? hivi unae mtoto kweli wewe?

Mkuu maamuzi ya kukurupuka siyo priority yangu daima. Nakubaliana na wewe na tunaamini endapo hatalifanyia kazi jambo hili kwasasa basi next Year uhamisho atautoa hata kwa mapanga
 
Kutokana na Location tuliyokua tunakaa Awali ilibidi nimpeleke hapo, lakini hata hiyo ya ubungo nasikia ni hayo hayo!
Ulichojibu ndio nilichokuwa nawaza ila sidhani kama umechelewa mtafutie shule ya karibu ni mtoto atamudu mazingira mapema
 
Msaada wa kimawazo khs kumuhamisha Mwanangu atlas ya madale kutokana na changamoto za hostel zao,na kuna mwenye kufahamu iwapo naweza kupata uhamisho wa mtoto wa std 7?
 
Back
Top Bottom