Kwanini mimi niuelewe wewe usiuelewe?na huwezi kumhukumu mtu aliyepata ujumbe ambao ulijua kabisa kua hajauelewa na uwezo wa kumfanya aelewe unao. Mungu mjuzi wa yote na mwenye uwezo wote hatakiwi kutoa mafundisho, mungu akikupa mafundisho anapaswa kujua mfumo mzima wa ubongo wako bila hata kukupa mtihani.
Ndio, atakupa mtihani, na huo mtihani sio kwa ajili yake kujua kama wewe umeelewa au la, ni kwa ajili yako kujitambua na kujipima, yeye hana shida na sisi ila sisi ndio tuna shida na yeye.Kama mungu akijua kua umeelewa katika mafundisho aliyokuatia je atakupa mtihani ili akupime kuangalia kama umeelewa???
Ndio atakupa mtihani, ili wewe mwenyeo utambue kuwa umeelewa au hujaelewa, yeye hana shida ya kujua kama umeelewa au la, wewe ndie unaetakiwa kujua.Kama mungu akijua kua hujaelewa, je atakupa mtihani ili aweze kujua kua hujaelewa???
Mungu muweza wa yote, hufanya lile alitakalo na sio ulitakalo wewe. Hapo ndio mnafeli, yeye ameamua kila mtu awe na ujuzi wake. Hoja mfu kabisa. Angelifanya wote tuwe na ufahamu mmoja basi bado ungekuja kuhoji kwanini ametupa ufahamu mmoja.Vile vile mungu kama ni muweza wa yote kwanini ashindwe kukufanya ujue kila jambo analolitaka bila kukupima na mitihani ambayo hata baada ya kugundua kua hujaelewa hakuwezeshi ili nawe uweze kuelewa????
Uelewavyo wewe, uislam ni nini kwani?uislam unauwezo wa kuniepusha zinaa bila kunifundisha namna ya kuepuka??? Kama hauna uwezo basi hata kukosea kwangu sitaulaumu kwasababu una imperfection, ila kama unao uwezo wa kunifanya niepuka bila kufundishwa basi ni ujinga kuendelea kunifundisha kitu ambacho kinaweza kuniepushia.
uislam kwanini usifanye mambo automaticaly bila kumfundisha mtu kama ilivyo mmen'genyo wa chakula unavyo fanyika tumboni bila kufundishwa???
Jiepusha kwa sababu hujui maono ya Mungu. Hujui mungu ameona vipi kama utafanya mema au mabaya. ungelikuwa unajua basi ingekuwa hamna maana, lakini the whole point ni kwamba wewe hujui anachokijua, ndio maana unatakiwa ustrive for the best.nijiepushe kivipi na mabaya wakati mungu tayari alishaona kua ntayakwaaa??? Kwaiyo mungu akijua kua nitafanya mabaya mimi naweza nikaepuka nikafanya mazuri???
Adhabu ameziweka siku ya mwisho kwa watu kama nyie mnaompinga Mungu kwa sababu zilizokosa kichwa na miguu. Siku hio ikifika ndio mtapat uthibitisho mliokuwa mkiutafuta lakini itakuwa too late tena.Wakati huo baba yake sio mjuzi wa yote na muweza wa yote ni kweli nitamuadhibu maana hayakua mategemeo yangu kumuona mtoto wangu anafeli wakati nilimfundisha na itakua hukumu ya haki kwake.
Lakini kwa mungu mwenye sifa ya ujuzi wote na uwezo wote hapaswi kutoa mtihani wala kuadhibu mtu kwasababu hajaelewa wakati uwezo wa kumfanya aelewe bila mtihani anao
Hakuna kiumbe chochote ambacho kinaweza kumzidi huruma Allah. Na ndio maana Allah anakusamehe kwa kosa lolote utakalofanya ikiwa utatubia kabla siku yako ya kufa, tena unapotubu, anafuta dhambi hio kabisa, siku ya Akhera, hujikukumbushwa kama ulifanya kosa flani. Leo hii tunaona Msanii Diamon, mpaka leo anamchukia baba yake hata kama mzee ameomba msamaha, sasa unataka kufananisha na huruma za Mungu? Kuna kiumbe gani hasa chenye huruma zaid ya Allah aliemuumba? Na je Kuna kiumbe gani chenye kuadhibu kuliko Allah?Adhabu ya mungu kwa watu wake ni moto kwaiyo hii adhabu utaifananisha na adhabu ya huyo mtoto aliyopewa na baba yake?? Yani mzazi kamzidi mungu huruma mzazi ndio kama mungu halafu mungu ndio kama shetani sasa
Atheist leo unaamini uwepo wa mashetani? 😀 😀 😀
Mfano haujawa mfu, kwa sababu ni kitu ambacho kipo na kinawezekana sana tu. Watu kuikewa mitego ipo sana tu.kwa kusema tu inawezekana mzee alikua na uhakika umekua umefanya assumption ambayo sio uhalisia na kufanya mfano wako uwe mfu tena
Huyo sio muumin, labda muumin wa atheism 😀Kuna muumini mwenzako alisema mungu akiwa na sifa hii ya ujuzi wote halafu akakuadhibu kwa kile alichokiona kua utafanya halafu wewe ukawa huna namna ya kukikwepa basi huyu mungu ni snitch.
Mimi nasema sio snitch kwasababu hayupo angekuwepo kusingekua na dhana ya kusema anatoa mitihani wala uhuru wa kuchagua halafu katika kitu alichokiona huwezi kuchagua tofauti na alivyoona
Hapa narudi pale pale, Mungu anajua khatma yako, wewe unajua khatma yako? UTAJUAJE KUWA YEYE ALIONA WEWE UTAINGIA MOTONI? Hebu naomba unijibu hili angalau.
Hujajibu swali, kwanini mimi nielewe uwepo wake wewe ushindwe kuelewa? Au umechagua tu kutoamini uwepo wake kwa sababu humuoni? 😀Inamaana huelewi kua mungu alikwishajua kua sitaelewa mafundisho yake mpaka unauliza hili swali? Hujui kila kitu kinachofanyika hakifanyiki kwa bahati mbaya??
Mungu angekufanya uelewe, ile dhana ya uhuru yote ingefutika. Hata mimi Allah hajanifanya nimuelewe, ila amenipa akili ya kuchambua mambo na kujitafutia elimu. Hata mimi Allah hajanipeleka msikitini ila amenipa miguu niitumie kwenda uko.Kwanini yeye mwenye uwezo wote ambao angeweza kuutumia uwezo huo kunifanya namimi nielewe kama wewe, ameshindwa kunifanya nielewe?? kiasi kwamba hata wewe umeona umuhimu wa mimi kuelewa hayo mafundisho je inamaana huyu mungu ajaona umuhimu wa mimi kuelewa hayo mafundisho???
Ubongo wako umepewa uufanyie nini? utafute pesa tu na ulewe?Ujumbe ukishamfikia huyo mtu allah anakua hajui kua huyo mtu hajaelewa?? Akijua kua hajaelewa kwanini hakumfanya aweze kuelewa zaidi inamaana allah hana uwezo wa kumfanya mtu akaelewa nje ya adhabu???
