Atheist wengi hawajui wanachokitafuta

Atheist wengi hawajui wanachokitafuta

Hata wewe mwenyewe uwepo wako hapa duniani ni nadharia tu maana huna purpose yoyote iliyokuleta. Umejitokezea tu by chance.
Unaweza kutuelezea kwamba kwanini uwepo wa mwanadamu hapa duniani usiwe na lengo na ilikuwaje mpaka tukatokea hapa "By Chance".

Embu tuelezee hili tupate faida.
 
Ulijuaje kama huna uwezo wa kuliepuka?

Kwasababu tayari nimesha lifanya na sikuweza kuliepuka

Swali langu bado hujajibu

Kama Lengo la mtihani ni kunijuza halafu mungu alijua kua akinipa mtihani sitaweza kujua, kwanini atoe hukumu kwa kosa ambalo lipo nje ya uwezo wangu ambalo sikuwa na uwezo wa kuliepuka???

Kuelewa uwepo wa Mungu haihitaji elimu ya juu, na Mungu hajakupangia ujuzi, ila amekupa ubongo tena kila mtu na ujuzi wake kwa vile atakavotafuta elimu. Haiwezekani ukae kitako nyumbani useme ah mi sijapewa ujuzi wa kutafuta kazi, nani atakuelewa.
kuna trend ya kukwepa maswali kwa kugeuza maswali

Nasubiri jibu kwa haya maswali

Kama mungu kaamua kila mtu awe na ujuzi wake aliopangiwa na watu wametofautiana katika huo ujuzi, inakuaje tena atoe hukumu kwa watu ambao wana ujuzi mdogo kwa kutoelewa mafunzo yake wakati yeye ndiye aliyewapa ujuzi huo mdogo usioweza kuelewa vitu vikubwa???

Imesaliwa na nani?
kusaliwa ndio nini?


Narudia tena, Mungu hajakupangia kuwa wewe unaingia peopni au motoni. Na kujua kwake khatma yako hakujahalalisha wewe kukaa ndani tu. Kama huna purpose, si ujiue tu yaishe? ukae uteseke, uje upate maradhi uhangaishe watu, jiue kabisa tu.

Nijue kisa mungu wakufikirika ambaye kihalisia hayupo?? Wewe unaweza kujiua kwasababu ya invisible pink unicorn???


Sina haja ya kukuthibitishia uwepo wa Mungu, kwa sababu umechagua kutoamini uwepo wake bila hoja yoyote ya elimu.
namimi hakuna sehemu nimesema nataka nithibitishiwe uwepo wa mungu kutoka kwa watu wenye "kuamini"

Kuamini kitu huhitaji kuwa na ukweli wala uthibitishi ili kushikiria imani yako, sasa kivipi nikuombe uthibitisho wakati hata wewe unaamini tu bila kujua???


Hata mimi najua ukiendelea ivo utaingia motoni tu 😀
Motoni ni sehemu ya kufikirika tu kama mungu na shetani

Halafu These days watu hawaogopi moto ilitakiwa mtumie trick nyingine hii ipo outdated mno. Moro gari ya mafuta ilivyowaka watu walikufa sana lakini bado watu hawakukoma kuchota mafuta kwenye magari yaliyoanguka huko mikoa mingine

Watu wanaogopa umasikini sio moto



Huwezi kumtolea mfano Mungu na kiumbe chengine ikiwa huamini uwepo wa Mungu na hicho kiumbe kingine.

mungu, shetani, panya mabaka aliyemvisha paka kengele, spiderman, hulk, harrypotter, vampires, zeus, zombies, pazi aliyebebwa na jogoo, batman, superman, nk hao wote ni character wakufikirika japokua naweza kuwajadili kama ni real character kulingana na hadithi zao

Ikiwa umemtolea mfano Mungu kuwa kama shetani, basi bila shaka shetani unamjua wewe 🙂 Atheist kwa kujigonga gonga bana....
Kuna uhusiano gani wa kutolea mfano na uhalisia wa mfano huo??

Mfano mimi scars ni mungu wako wewe chilubi. Utakubali kua mimi ni mungu wako??

Mfano pazi alivyobebwa na jogoo, mfano huu unauhalisia wowote kua kweli mtu aliyeitwa pazi alibebwa na jogoo??

Mitego ipo
na ndio imetawala hapa kuliko hoja za msingi


Sio juu yangu, ni juu yako kuthibitisha kama ni muumin au sio muumin, wewe ndio uliepewa habari na huyo unaemuita muumin. Yawezekana hata maana ya muumin hujui lakini. Anaweza kuwa muumin wa ujinga?
Kwa kuna muumini au muamini mungu asiye mjinga??


Ipo haja kubwa ya kufanya ibada ikiwa wewe hujui hatma yako.
kutokujua hatma yako si kigezo cha wewe kwenda tofauti na alivyopanga mungu. Mungu kajua utaua kesho wewe hata ukijua hilo unauwezo wa kuliepuka??

Ama kama wewe unajua hatma yako na kwamba unajua ni motoni tu, basi huna haja ya kufanya ibada.
ni kwasababu siwezi kuepuka alichokiona kwaiyo ibada haina msaada kama kivuli cha fimbo

Mungu akijua khatma yako kuwa ni motoni, hana wajibu wa kukufanya wewe usiende motoni
Mungu akijua hatma yako kuwa ni motoni na hana wajibu wa kukufanya wewe usiende motoni je ni wajibu wa nani wakukufanya usiende motoni???

inamaana nia yake kubwa nikukuchoma moto ilihali uwezo wa kutokuchoma anao??

ni wajibu wako mwenyewe uliepewa uwezo wa kutofautisha zuri na baya kuchagua kama unataka kwenda peponi au motoni.
Kwani sio wajibu wa mungu kuhakikisha kila mtu amempatia usezo wa kutosha ili achague yale yatayompendezesha yeye??

Na kama mabaya yaliwekwa ili yachaguliwe na binadamu iweje mungu huyu awaadhibu wataochagua mabaya??

Kama mabaya ni ubaya kwanini aruhusu mabaya yawepo, huoni kwamba huo ni ubaya kwa kuruhusu mabaya???



Bado hujajibu swali, unajua kuwa Mungu anajua Khatma yako lakini hujajua kile anachokijua, sasa je unajua khatma yako ya mwisho ni ipi?
Iko hivi

Dhambi = motoni

Mema = peponi

Mungu hataki ufanye mabaya kwasababu kufanya kwako mabaya hatma yako itakua motoni (mpaka hapa nimejua hatma yangu)

Sasa mtu kafanya mabaya bila kutubu huku akijua amefanya kosa, huku akijua mungu amejua kua ametenda dhambi (hapa yuko sambamba na mungu, alichokijua mungu naye kakijua)

Halafu mtu huyo akaamua kukatisha maisha yake kwa kujiua (hapa kaongeza dhambi nyingine ambayo alijua kabisa kua kujia ni dhambi)

Sasa mtu huyo atakua hajui hatma yake ilihali anajua sifa ya mungu kua ni mjuzi wa yote na anajua kua dhambi hupelekea hatma yako iwe motoni na yeye kafanya dhambi pasipo kutubu???


Huyo mtu aloua na akajiua, si tayari anazijua sheria na hukumu zake?
sio tu sheria bali anaelewa kua mungu amejua na hatma ya dhambi ile anajua kua ni motoni sasa umeelewa namna ambavyo inawezekana mtu kujua hatma yake??

Sasa akienda kinyume chake mana yake amejichagulia mwenyewe njia ya kwenda motoni kwani alikuwa na uwezo wa kuepuka kufanya ivo.
Ishu sio kinyume wala kimbele, ishu ni mtu kujua alichojua mungu au hatma yake. sijui kama umeelewa

Pia Hakuliepusha hilo kutokea kwa sababu lau kama angeliepusha maana yake ile sifa yake ya kuwa anajua kila kitu kabla hakijatokea ingefutika. Pia lau kama angeliepusha kutokea, wewe ungekuja kuhoji kwanini hajaliachia tu litokee?
pia kama kutoliepusha kungemfanya asiwe mjuzi wa yote huoni kwamba kuliacha litokee jambo hilo bila kuliepusha kunamfanya asiwe na uwezo wote???

Mungu alishindwa kuepusha hilo jambo bila kuweka kizuizi cha mimi kuhoji???

Kama mungu aliamua asiepusha hilo jambo kwasababu mimi ningehoji kwanini hajaliacha litokee, mbona saizi bado nahoji japokua hajaliepusha lisitokee?

I am not stoned, because i know, you chose not to believe, it is not like you do not understand.
You can't deny to not be stoned while you still believing and not knowing

Kwa sababu kama wewe unaamini kuwa Ulimwengu haukuwa na muumbaji na hauna purpos
hakuna sehemu nimesema naamini hivyo, so usipandikize maneno nisiyoyasema

Hata kama ulimwengu una purpose hiyo haimaanishi mungu ndiye muasisi wa ulimwengu

basi kwanini sisi tusiwe tunaishi maisha sayari ya Mars?
Vitabu vimesema shetani alitupwa duniani, na kila baya linafanyika kwa kusababishiwa na shetani kwanini mungu asiwapeleke mars ili kuwaepushia na shetani msije kutenda dhambi???


kwanini kwenye solar system yetu tuko peke yetu?
Hii ni kwa mujibu wa quran??

Peke yako na nani? Unalimaje kujua kua uko pekeyako na sio kwamba huna uwezo wa kuzunguka kuwaona wengine??

Kwanini position ya dunia iko on the right place to support life

position ya dunia ingekua iko katika right place basi inge support life bila viumbe kufariki


kwanini isiwe venus? Hivi unataka kunambia kuwa lile jengo la ikulu magogoni limejijenga wenyewe bila ya fundi?
ni kweli lile jengo limejengwa na wajenzi, hivi unataka kuniambia hao wajenzi hawana wazazi wao yani wamezuka tu bila chanzo chochote???


Uwepo wa Mungu hauhitaji kusoma mabuku, uwepo wa Mungu ni LOGIC tu.
kwa kusema tu "logic" umeshakubali mungu hayupo. Mungu mjuzi wa yote mwenye uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu wenye kuruhusu mabaya huyu mungu hayupo kwasababu ni illogic kua na mungu wa dzain hii


HAKUNA KIUMBE KILICHOKUWA HAKINA MUUMBAJI, NA HAKUNA KILICHOUNDWA KIKAKOSA MUUNDAJI. Kama vipo thibitisha!
Vile vile hakuna kilichounda kikakosa muundaji, au kichoumba kikakosa muumbaji. Yaani mjenzi aliyejenga jumba la magogoni akawa hana chanzo ni kitu ambacho hakiwezekani

na hakuna kisicho kiumbe kilakitu ni kiumbe eidha kiwe hai au kisiwe hai so point yako ni nini hapa??

Nikurudishie huwo mfano wako wa iphone 11.
Basi ni wajibu wangu mwenye iphone original kukuambia kuwa simu yako feki kwa sababu fulani na fulani.[/QUOTE]
kwasababu simu ni feki hivyo kosa sio lake na sio tegemeo lake kua na simu hiyo feki si ndiyo?

Siwezi kukwambia kuwa umeziwa simu chaka ikiwa sijui tofauti ya chaka na original.
na ndio maana ulipoangalia specs kutoka kwenye simu yako ukagundua kua yangu ni famba. Sasa hapo utaweza kumlaumu aliyeuziwa au kulaumu walioniuzia kua sio waaminifu wamenitapeli kwa kunipa kitu feki??

Ninapokwambia kuwa simu yako kimeo na wewe ukabisha, hasara anaipata nani?
unachokiandika kinachekesha sana

Sasa ukiniambia simu yangu kimeo na mimi nikikubali hasara haitakuwepo??

Huo ukimeo nakua nimeuweka mimi au imewekwa na wengine??


au nani atakuwa mjinga in this case? Itakuwa umechagua kuamini utakavyo wewe na sio vile ilivyo ukweli, kwa sababu ya wewe kukataa kuwa simu yako sio kimeo hakuondoshi kuwa simu yako ni kimeo.
Kwanza tutapaswa kujua kipi chanzo cha mimi kuonekana mjinga? Bila shaka ni wauzaji na bila wao kufanya uhuni kusingrkua na mjadala wa kujadili nani mjinga katika hili


Nilikuletea maana ya freedom/uhuru. Sivyo hivo unavojaribu kuaminisha watu. naileta tena;
Freedom - the power or right to act, speak, or think as one wants. kwa kiswahili tu ni kusema kuwa Uhuru ni uwezo wa kufanya lile utakalo. Sasa mtu kujua utafanya nini kunaondoaje uhuru? Hapa utaona kuwa umechagua kutoamini uwepo wake bila ya kuwa na hoja yoyote kiasi kwamba hata maana ya uhuru sasa unaipindisha.[/QUOTE]
Uhuru wa kuchagua kufanya lolote nitakalo, lakini hakuna uhuru wa kurudi nyuma ya muda. Hakuna uhuru wa kurudisha waliokufa wawe hai, hakuna uhuru wa kuchagua kutoumwa au kufa vyote hivyo tunachaguliwa automatically kivipi useme tuna uhuru wakuchagua lile tulitakalo??

mungu akijua kitu na katika kujua huko sina uhuru wa kufanya tofauti, utasema nina uhuru wa kufanya nachotaka??

Ili uhuru wakuchagua uwepo basi mungu hatakiwi kujua nacho chagua



By the way, ukienda tofauti na alivyojua? wewe utajuaje kuwa umeenda tofauti, kwani umejua? 😀
hii nishakujibu huko juu sitegemei kama hunaelewa


Kwa sababu Ametupa ubongo/akili za kutumia ili tumuelewe. Mungu ndivyo ALIVYOTAKA YEYE sio UTAKAVYO WEWE.

hapa pia unarudia pale pale nilipo kuelewesha. Nimekuelezea mapungufu ya ubongo hivyo mungu hapaswi kutoa adhabu kwa kigezo cha kutoelewa mafunzo yake wakati akijua udhaifu wetu

Mbona wewe hujajiumba mwenyewe utakavyo basi? 😀

Ni kwasababu haiwezekaniki kitu chochote kikajiumba chenyewe yani kikawepo tu bila chanzo unakubali??


Utaendaje msikitini ikiwa hujamuelewa? unaenda kufanya nini na kilichokupeleka msikitini nini? :O
For the same damn reason, mungu anaanzaje kukuhukumu ikiwa anajua kua hujamuelewa??


Allah ametaka kuumba kiumbe ambacho kitaitwa Binaadamu/Human. Sasa mwenyewe alichagua kuwa kiumbe hichi ili kiitwe human

wakati anachagua hayo ilipofika mda wa kuchagua kiumbe kiwe dhaifu au sio dhaifu akaamua kuchagua kiwe dhaifu siyo??


basi kitakuwa na sifa kadhaa wa kadhaa.

miongoni mwa hizo sifa ni pamoja na udhaifu??

Sasa kama hakutuumba ivi tulivyo, maanake sisi sio binaadamu tena, ni kiumbe kingine. Kwaio ili tuwe binaadamu basi hivi ndivyo alivotuumba, angetuumba na pembe kichwani basi ingekuwa kiumbe kingine. Pia ameumba kiumbe aina ya Malaika, hawa kawaumba wakiwa hawana matamanio ya nafsi kabisa na hawana free will, wao ni kutii amri tu, sasa hawa sio binaadamu, hawa tunawaita Malaika, sifa za malaika ndio hizo, sasa ikiwa ana sifa ya free will huyo sio tena malaika.

mungu kuumba halafu kuruhusu watu waweze kuhoji yale waliyoyaona bora endapo mungu angewafanyia hapo kosa la nani?
 
unayajuaje hayo mapenzi ya Mungu?? na unajuaje hili ni jema na hili ni baya?!
 
Kwasababu tayari nimesha lifanya na sikuweza kuliepuka

Swali langu bado hujajibu

Kama Lengo la mtihani ni kunijuza halafu mungu alijua kua akinipa mtihani sitaweza kujua, kwanini atoe hukumu kwa kosa ambalo lipo nje ya uwezo wangu ambalo sikuwa na uwezo wa kuliepuka???
Ikiwa hujafanya revision kwanini asikupe adhabu?

Naona nilikuuliza mengi hujajibu ata moja.

kuna trend ya kukwepa maswali kwa kugeuza maswali

Nasubiri jibu kwa haya maswali

Kama mungu kaamua kila mtu awe na ujuzi wake aliopangiwa na watu wametofautiana katika huo ujuzi, inakuaje tena atoe hukumu kwa watu ambao wana ujuzi mdogo kwa kutoelewa mafunzo yake wakati yeye ndiye aliyewapa ujuzi huo mdogo usioweza kuelewa vitu vikubwa???
Kuelewa uwepo wa Mungu haihitaji elimu ya juu, na Mungu hajakupangia ujuzi, ila amekupa ubongo tena kila mtu na ujuzi wake kwa vile atakavotafuta elimu. Haiwezekani ukae kitako nyumbani useme ah mi sijapewa ujuzi wa kutafuta kazi, nani atakuelewa?

kusaliwa ndio nini?
Nimekusudia "Imesajiliwa na nani" hio Taasisi ya upigaji?

Nijue kisa mungu wakufikirika ambaye kihalisia hayupo?? Wewe unaweza kujiua kwasababu ya invisible pink unicorn???
Sijakwambia ujiua kisa Mungu eti. Ujiue ili uepuka tabu za dunia tu. Yanini kuishi na huna purpose? huoni kama ni kujichosha uko?

Mimi nijiue kwa sababu ya pink unicorn kwani amenifanya nini? nataka kumuona huyo pink unicorn? hebu walau jifunze kutoa mifano yenye kuleta maana. Unicorn na Life Purpose vinafananaje kwa mfano?

sio tu sheria bali anaelewa kua mungu amejua na hatma ya dhambi ile anajua kua ni motoni sasa umeelewa namna ambavyo inawezekana mtu kujua hatma yake??
Hebu tuthibitishie kama ingekuwa wewe, umejuaje Khatma yako kabla ya kufanya icho kitendo?

Ishu sio kinyume wala kimbele, ishu ni mtu kujua alichojua mungu au hatma yake. sijui kama umeelewa
Thibitisha mtu utajuaje alichojua Mungu?
namimi hakuna sehemu nimesema nataka nithibitishiwe uwepo wa mungu kutoka kwa watu wenye "kuamini"

Kuamini kitu huhitaji kuwa na ukweli wala uthibitishi ili kushikiria imani yako, sasa kivipi nikuombe uthibitisho wakati hata wewe unaamini tu bila kujua???
Vizuri kuwa unathibitisha kuwa ni uchaguzi wako kumkataa Mungu na sio kuwa huelewi. Mimi najua ninachoamini.

hakuna sehemu nimesema naamini hivyo, so usipandikize maneno nisiyoyasema

Hata kama ulimwengu una purpose hiyo haimaanishi mungu ndiye muasisi wa ulimwengu
Kwaio wewe unaamini Ulimwengu unae Muumbaji?

Motoni ni sehemu ya kufikirika tu kama mungu na shetani

Halafu These days watu hawaogopi moto ilitakiwa mtumie trick nyingine hii ipo outdated mno. Moro gari ya mafuta ilivyowaka watu walikufa sana lakini bado watu hawakukoma kuchota mafuta kwenye magari yaliyoanguka huko mikoa mingine

Watu wanaogopa umasikini sio moto
Ujinga katika hali ya juu, wangekuwa wanaogopa umaskini nchi isingekalika hii. Watu wa vitu instead of Utu ndio nyie. Umaskini unauogopa wewe tu. Wenzako habari hawana na wanaishi kwa furaha tu.
Kuna uhusiano gani wa kutolea mfano na uhalisia wa mfano huo??

Mfano mimi scars ni mungu wako wewe @chilubi. Utakubali kua mimi ni mungu wako??

Mfano pazi alivyobebwa na jogoo, mfano huu unauhalisia wowote kua kweli mtu aliyeitwa pazi alibebwa na jogoo??
Una sifa za Uungu hata uwe Mungu wangu?

Kwani huo mfano umeutumia kwa mfumo gani? mafumbo ama? mana kama sio kwa mafumbo labda umemuona huyo pazi akibebwa na jogoo na watu watataka ushahidi, ila kama umezungumzia kwa mafumbo basi hata watakuelewa kimafumbo.

na ndio imetawala hapa kuliko hoja za msingi
Kutojua maana ya Kujua na kupanga, unajaribu kuweka neno kupanga kwenye Kujua 😀

Kwa kuna muumini au muamini mungu asiye mjinga??
Anaeamini uwepo wa Mungu ana akili na asieamini uwepo wa Mungu ni mjinga, kwa sababu unakataa kuwa Ulimwengu una muumbaji wake ila hapo hapo nikikwambia gari haina muundaji wake unaniona mjinga!

kutokujua hatma yako si kigezo cha wewe kwenda tofauti na alivyopanga mungu. Mungu kajua utaua kesho wewe hata ukijua hilo unauwezo wa kuliepuka??
Utalijua hilo? Toa hoja kiuhalisia. Huwezi kwenda tofauti na AJUAVYO (wewe umetumia neno kupanga ili kupotosha 😀) MUNGU. Na huwezi kujua kama ameenda tofauti kwa sababu hujui alijua vipi. SIO ALIPANGA VIPI



HUJUI MAANA YA KUJUA NA KUPANGA?

ni kwasababu siwezi kuepuka alichokiona kwaiyo ibada haina msaada kama kivuli cha fimbo
Kwanini usifanye ibada basi? kwanini uchague kutenda dhambi?
Vitabu vimesema shetani alitupwa duniani, na kila baya linafanyika kwa kusababishiwa na shetani kwanini mungu asiwapeleke mars ili kuwaepushia na shetani msije kutenda dhambi???
Mungu ametaka tu mwenyewe kuwatupa duniani, haya sasa nijibu na wewe nililokuuliza.

And by the way, Steve Jobs alikuwa hajui kama kuna tunda linaitwa Mango? Pineapple? ama?

Hii ni kwa mujibu wa quran??

Peke yako na nani? Unalimaje kujua kua uko pekeyako na sio kwamba huna uwezo wa kuzunguka kuwaona wengine??
Kwani si vyombo vinapelekwa kila miaka kuchunguza uko nje? Hebu nitajie basi sayari yenye civilization unayoijua wewe.

position ya dunia ingekua iko katika right place basi inge support life bila viumbe kufariki
Kufariki ndio cycle ya dunia, ingekuwa hakuna kufa, dunia ingejaa mara moja tu, na kwanini basi isikae kwenye hio right place uitakayo wewe? kwa sababu kama hakuna purpose ulimwenguni kwanini tufe tupishe wengine waje? and by the way, WHERE IS THE RIGHT PLACE ACCORDING TO YOU?

ni kweli lile jengo limejengwa na wajenzi, hivi unataka kuniambia hao wajenzi hawana wazazi wao yani wamezuka tu bila chanzo chochote???
Kwa vile umekubali kuwa lile jengo lina wajenzi, basi na Ulimwengu una mjenzi wake, na ndio maana akaiweka dunia hapa ilipo ili mimi na wewe tuishi. Tofauti ya hao wajenzi, wao ni VIUMBE lazima Viwe na chanzo.

Vile vile hakuna kilichounda kikakosa muundaji, au kichoumba kikakosa muumbaji. Yaani mjenzi aliyejenga jumba la magogoni akawa hana chanzo ni kitu ambacho hakiwezekani

na hakuna kisicho kiumbe kilakitu ni kiumbe eidha kiwe hai au kisiwe hai so point yako ni nini hapa??
Yupo aliekuwa sio Kiumbe nae ni Allah aleiumba mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake. Muumbaji hana Muumbaji.

Kuumba ni from nothing to something.

na ndio maana ulipoangalia specs kutoka kwenye simu yako ukagundua kua yangu ni famba. Sasa hapo utaweza kumlaumu aliyeuziwa au kulaumu walioniuzia kua sio waaminifu wamenitapeli kwa kunipa kitu feki??
Kwanini nisikulaumu wewe kwenda kununua kitu usichikijua? Mbona mimi binafsi washkaji wananifuata wananambia kuna iphone hii hapa ni original ama vipi? ina icloud ama vipi? na nawapa majibu, tena watajua wenyewe kama watanunua ama la, lakini hawana wa kumlaumu zaidi ya nafsi zao.

Kwanza tutapaswa kujua kipi chanzo cha mimi kuonekana mjinga? Bila shaka ni wauzaji na bila wao kufanya uhuni kusingrkua na mjadala wa kujadili nani mjinga katika hili
vipi wao uwaite wajinga wakati wewe ndio wamekufanya uwe mjinga? Utakuwa mjinga kwenda kununua kitu bila kuhakikisha wakati kuna njia tayari za kujua kama kitu feki ama si feki. Yaani utoke na miguu yako miwili ukafanye dhambi halafu useme Mungu ndo kajua ivo? huo si ujinga?

Uhuru wa kuchagua kufanya lolote nitakalo, lakini hakuna uhuru wa kurudi nyuma ya muda. Hakuna uhuru wa kurudisha waliokufa wawe hai, hakuna uhuru wa kuchagua kutoumwa au kufa vyote hivyo tunachaguliwa automatically kivipi useme tuna uhuru wakuchagua lile tulitakalo??
Uwezo wa kurudi nyuma ya muda unao? Na ukiwa nao utakuwa huna uhuru wa kurud nyuma?
Uwezo wa kurudisha waliokufa unao? ungekuwa na uwezo huo nani angekuzuia?
Uwezo wa kuchagua kuumwa au kutoumwa unao? ungekuwa unao, nani angekuzuia?

Unazungumzia UHURU AU UWEZO?

Hii point ipo in red nasubiri jibu kwa hamu hasa. I need your answers on this point to point.

mungu akijua kitu na katika kujua huko sina uhuru wa kufanya tofauti, utasema nina uhuru wa kufanya nachotaka??

Ili uhuru wakuchagua uwepo basi mungu hatakiwi kujua nacho chagua
Utafanyaje tofauti na alivyojua kuwa utafanya kwa maamuzi yako mwenyeo? Hio kanuni ya kuwa ili uhuru wakuchagua uwepo basi Mungu hatakiwi kujua unachochagua umeitoa wpi? kwa sababu Uhuru haihusiani na kujulikana chaguo lako. Kwani mfano mtu akijua kuwa unampenda Fulani, manake huna uhuru amekuchagulia yeye umpende?

hii nishakujibu huko juu sitegemei kama hunaelewa
Sijaelewa na ndio maana nataka ufafanue vizuri. Unajuaje kuwa umeenda tofauti na alivoona Mungu?

hapa pia unarudia pale pale nilipo kuelewesha. Nimekuelezea mapungufu ya ubongo hivyo mungu hapaswi kutoa adhabu kwa kigezo cha kutoelewa mafunzo yake wakati akijua udhaifu wetu
Umeambiwa kuna Mungu, haya nikuulize umesoma wapi habari zake?

Ni kwasababu haiwezekaniki kitu chochote kikajiumba chenyewe yani kikawepo tu bila chanzo unakubali??
Sasa mimi nimekuuliza swali ila naona unalijibu kwa woga. Basi ngoja nikwambie jibu langu halafu nini utaniuliza na jibu lake litakuaje;

Mimi: Haiwezekani kitu chochote kikajiumba chenyewe bila kuwepo chanzo
Scars: basi Mungu nae atakua ana chanzo chake
Mimi: Mungu sio Kiumbe, kisichoumbwa hakina source.

For the same damn reason, mungu anaanzaje kukuhukumu ikiwa anajua kua hujamuelewa??
Hujanijibu swali lakini? Mungu hujamuelewa unaenda msikitini kufanya nini? Kusali? Basi itakuwa umemuelewa na ndio maana ukaenda msikitini na ukasali. Lakini vipi unampinga Mungu halafu unasema kuwa hayupo bila ya kuwa na hoja yoyote yenye mashiko na bila kuthibitisha kutokuwepo kwake? vipi baada ya ishara zote zilizoletwa wewe ukazikataa? ivi kweli itakuwa hujajua kama kuna Mungu?

Ikiwa unajua kuwa hakuna kiumbe kinachoweza kujiumba chenyewe, tena vipi ukatae uwepo wa Muumbaji?

wakati anachagua hayo ilipofika mda wa kuchagua kiumbe kiwe dhaifu au sio dhaifu akaamua kuchagua kiwe dhaifu siyo??
Dhaifu mbele ya nani?

miongoni mwa hizo sifa ni pamoja na udhaifu??
Ndio
mungu kuumba halafu kuruhusu watu waweze kuhoji yale waliyoyaona bora endapo mungu angewafanyia hapo kosa la nani?
Hakuna kosa kutamani kuwa Mungu angekuumba Tajiri ama vile upendavyo. Ameshasema mwenyewe duniani ni mapito, atakaefuzu, atakwenda peponi, huko unachotaka wewe basi utapata. Ama kama mwenyewe unaona bora uende tu motoni, basi umechagua mwenyewe usimlaumu yeye kujua wewe utaishia motoni. kwa sababu ndivyo ulivotaka mwenyewe.
 
Kwani alishauriwa na nani asikuumbe wewe mchina ? ni mambo ambayo Ameamua mwenyewe kuyafanya kwa akili yake inavyopenda kuwa chilubi nitamtoa mwanaume kisha atakwenda motoni ova
Binadamu hatuwezi kufikiri kama Mungu anavyofikiri. Au ufahamu au maarifa ya mwanadamu ni tofauti na maarifa ya Mungu.

Mathalani unatizama movie ambayo kwako ni mpya hujawahi kuiona, ufahamu au maarifa ya mwanadamu hayawezi kujua mwanzo wa movie utakuwaje, katikati ya movie itakuaje na mwisho wa movie utakuwaje.

Kwa mfano huu wa movie kwa jinsi mwanadamu anavyoyaangazia mambo basi anamkadiria Mungu wake naye ufahamu wake wa kuangazia mambo upo kama aliyonao yeye binadamu.

Na hapa ndipo tunapofeli! Binadamu hawezi kufikiri kama Mungu! Na ufahamu au maarifa ya binadamu ni tofauti na Mungu!

Mungu anafahamu mwanzo wa jambo utakuwaje hata kabla ya hilo jambo kuzuka, na katikati ya jambo litakuwaje na mwisho litakuaje. Si hivyo tu! Bali Mungu anafahamu litatokea wakati/muda upi na hata baada ya wakati/muda Mungu anafahamu ni nini kitakachotokea.

Maamuzi ya maisha yako ya kwamba utakua wa peponi au wa motoni Mungu hajayapanga. Bali wewe mwenyewe binadamu ndiye uliyeyapanga. Ndiyo, Mungu ameshaandika kila kitu kitakavyokuwa na mwenendo wake utakavyokuwa na mwisho wake utakavyokua.

Kwa nini Mungu kajua hivyo? Kwa sababu Mungu elimu yake, ufahamu wake na ujuzi wake umetangulia nyakati. Elimu yake Mungu imetangulia kabla hata ya nyakati kutokea, baada ya nyakati kutokea, nyakati iliyopita, nyakati ya sasa na nyakati ijayo, na baada ya nyakati.

Ndiyo maana yeye Mungu anafahamu kwamba yule atakuwa wa motoni na yule atakuwa wa peponi. Kwa sababu yeye tayari alishaona kabla mwenendo wa hao viumbe wake utakuaje...
 
Ikiwa hujafanya revision kwanini asikupe adhabu?
Kwanini mungu aweke kipaumbele kwenye kutubu kuliko kuzuia baya ili kumuepusha huyo mtu asilifanye??

Kwaiyo mungu anaweza akajua kua kesho utamuua mama yako bila hatia halafu akaacha tu wewe ufanye mauaji ili akuone kama utatubu?? Yani mungu anaruhusu mtu mwingine afe bila hatia ili akupime kama utatubu???

Logic gani hapa itamkubali mungu wa dzaini hii??

Naona nilikuuliza mengi hujajibu ata moja.
Si kweli nimejibu mengi tena kwa urefu na kwamifano na unaweza kuweka hapa ambacho sijakijibu.


Kuelewa uwepo wa Mungu haihitaji elimu ya juu, na Mungu hajakupangia ujuzi, ila amekupa ubongo tena kila mtu na ujuzi wake kwa vile atakavotafuta elimu. Haiwezekani ukae kitako nyumbani useme ah mi sijapewa ujuzi wa kutafuta kazi, nani atakuelewa?
Hili nimelitolea majibu more than two times labda nisisitize tena

Kwanza kwa swali hili linaonesha kabisa hata wewe una matatizo ya ubongo, maana nimekuelezea kwa urefu sana lakini bado umeonekana kutokuelewa.

Ubongo unamapungufu mengi hauoneshi kama umeumbwa na Omnipotent power. kuanzia uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu hadi uwezo wa kustahimili hali ngumu pasipo kuruhusu matatizo katika mfumo wake

Unavyozaliwa ulikua na ubongo lakini je unakumbukumbu yeyote unayoikumbuka katika tukio la kuzaliwa kwako ukiachana na masimulizi kutoka kwa mashuhuda walikokuwepo siku hiyo?? Bila shaka huwezi na ndio maana hata vitu nilivyokuelezea mda mchache uliopita umeshindwa kuvikumbuka au hta kuvielewa kwasababu ya mapungufu ya ubongo

Mungu (naashumu kama yupo japokua hayupo) alijua hilo kua binadamu amewapa uwezo mdogo wa kiufanisi katika ubongo wao, alijua kua katika vitu nitakavyo wapa hawatoweza kuvifanya kikamilifu hivyo kama mungu alitaka watu wafanye vitu kikamilifu kama apendavyo, basi alipaswa kuweka mfumo ulio kamili usio kosea wala kusahau ili watu wafanye kile akitakacho bila kizuizi. Lakini hakufanya hivyo unafikiri ni kwanini?? Ukitumia logic utagundua mungu alitaka tufanye makosa, na kweli tukafanya makosa ambayo yeye ameyaruhusu yafanyike sasa kivipi atuadibu?? Hapa logic inakataa huu udwanzi wa kindeezi uliojaa upuuzi unaoonesha mungu si mjuzi na anafanya mambo ya kishenzi ambao hata sisi hatuwezi, je huyu anastahili kuitwa mwenyezi??


Nimekusudia "Imesajiliwa na nani" hio Taasisi ya upigaji?
kwanini kusajiliwa kuwe muhimu kuliko ubaya wa kitu???

Kila kilicho sajiliwa na kuhalalishwa kitakua halali kwako kwasababu tu kimesajiliwa na shirika fulani au uongozi fulani???

Utakua tayari kufanya jambo lolote ilimradi tu lisajiliwe?? Umtimamu?

Sijakwambia ujiua kisa Mungu eti. Ujiue ili uepuka tabu za dunia tu. Yanini kuishi na huna purpose? huoni kama ni kujichosha uko?
purpose kwani ni lazima liwe mungu??

Naweza kuishi kwa lengo la kujifunza vitu nisivyovijua na kusaidia wenye shida bila kutegemea malipo kutoka kwa mungu (ambaye hayupo) shida ambazo wakienda misikitini wala makanisani hawatasaidiwa zaidi ya kuambiwa wafunge na kusali, yaani mtu analia njaa halafu unamuambia funga bila kula allah atakunusuru what a joke but I ain't laughing??

Mimi nijiue kwa sababu ya pink unicorn kwani amenifanya nini? nataka kumuona huyo pink unicorn? hebu walau jifunze kutoa mifano yenye kuleta maana. Unicorn na Life Purpose vinafananaje kwa mfano?
invisible unicorn, shetani na mungu wote ni character wasiokua na maana kwasababu hawapo zaidi ya hadithi kama kirikuu

Hebu tuthibitishie kama ingekuwa wewe, umejuaje Khatma yako kabla ya kufanya icho kitendo?
Ok nitafanya hivyo ila kabla sija move on nataka nijue uliuelewaje ule mfano niliokupa?




Thibitisha mtu utajuaje alichojua Mungu?

mbona unanirudisha kule kule niliko kujibu swali hili?? Hivi ni kwamba huelewi kwa bahati mbaya au kusudi tu ili usionekane umeshindwa hoja??

Rejea mfano niliokupa kuhusu kuua na kujiua utaelewa

Vizuri kuwa unathibitisha kuwa ni uchaguzi wako kumkataa Mungu na sio kuwa huelewi. Mimi najua ninachoamini.

wewe unajua unachokiamini?? Hapo hakuna logic kwenye hoja yako, huwezi kuamini na kujua at the same time


Kwaio wewe unaamini Ulimwengu unae Muumbaji?

sijishugulishi na kilimo, vipi wewe unajishughulisha na uuzaji bangi??




Ujinga katika hali ya juu, wangekuwa wanaogopa umaskini nchi isingekalika hii. Watu wa vitu instead of Utu ndio nyie. Umaskini unauogopa wewe tu. Wenzako habari hawana na wanaishi kwa furaha tu.
umeona hoja zingine unazijibu mwenyewe, yani kumbe watu sio tu moto ambao hawauogopi bali hata umasikini nao hawaogopi aisee mi nikua sijui. sasa utawatisha kwa kipi unadhani au shumileta na saladini wa zamani??

Una sifa za Uungu hata uwe Mungu wangu?
Ni kweli sina sifa kwasababu i do exist and im not an imaginary being that cant be proved.

Kwani huo mfano umeutumia kwa mfumo gani? mafumbo ama? mana kama sio kwa mafumbo labda umemuona huyo pazi akibebwa na jogoo na watu watataka ushahidi, ila kama umezungumzia kwa mafumbo basi hata watakuelewa kimafumbo.
Kwani mfano wa kitu cha kufikirika ukiutumia kwa mfumo gani kunafanya mfano huo uwe kweli kihalisia???

Ukiutumia kwa mafumbo kunafanya pazi awe kweli alibebwa na jogoo??


Kutojua maana ya Kujua na kupanga, unajaribu kuweka neno kupanga kwenye Kujua 😀
.kwa mujibu wa dini yenu mungu sio mpangaji wa maisha ya binadamu??

Kwa mujibu wa dini zenu kuna kitu chochote kinachoweza kufanyika bila mungu kukiruhusu???


Anaeamini uwepo wa Mungu ana akili na asieamini uwepo wa Mungu ni mjinga
sijakataa hilo lakini hujui kua linaongeza uzito katika hoja zangu, yaani unapoonesha weakness za binadamu unakua unamshusha mungu wako viwango unamfanya ainekane kama fundi maiko kwasababu kwa mujibu wa dini zenu mimi na wewe ni kazi ya mikono ya huyo mungu wenu.


kwa sababu unakataa kuwa Ulimwengu una muumbaji wake ila hapo hapo nikikwambia gari haina muundaji wake unaniona mjinga!
Nitakubali kua gari lina muundaji kwasababu haiwezekani kitu kikawepo bila chanzo.
nikikubali kua ulimwengu una muumbaji wake halafu nikakuambia na huyo muumbaji naye ana muumbaji wake utakubali?? Kama utakataa nami ntakuona mjinga


Utalijua hilo?
jump to the solution, what will happen if you know? Kama hata ukijua huwezi badilisha chochote kwanini kujua kue hoja ya msingi??? BTW nimekupa mfano mzuri tu kuhusu hili ila naona umetafuta pakujifichia

Toa hoja kiuhalisia

niamini mimi bob, hoja za kiuhalisia na logic kwenye mambo ya kufikirika huwezi kuzikuta

Huwezi kwenda tofauti na AJUAVYO (wewe umetumia neno kupanga ili kupotosha 😀) MUNGU. Na huwezi kujua kama ameenda tofauti kwa sababu hujui alijua vipi. SIO ALIPANGA VIPI

Kwanini nisiweze wakati amenipa uhuru wa kufanya nitakalo??

Huoni unajifunga mwenyewe unapojaribu kumtetea upande huu unsjikuta unamchafua upande mwingine?



HUJUI MAANA YA KUJUA NA KUPANGA?
Anapanga kwasababu ni mjuzi wa yote na sina uhuru wa kuepuka kwakua alipanga litokee

akijua nitaiba sitaweza kuepuka kuiba kwakua tayari yeye alipanga iwe hivyo na kwasababu asingetaka iwe hivyo angeniepusha kwakua ni muweza wa yote

Lakini kuna swali, inamaana mafundisho ya dini yako yanapinga kua mungu sio mpangaji wa maisha ga binadamu? Na kuna vitu vinatokea bila mungu kuruhusu vitokee??

Kwanini usifanye ibada basi? kwanini uchague kutenda dhambi?
Kwasababu kila kitu ni sehemu ya mipango yake, kufanya ibada au kutokufanyi hskufanyiki kwa bahati mbaya ni yeye slitska wewe ufanye hivyo


Mungu ametaka tu mwenyewe kuwatupa duniani, haya sasa nijibu na wewe nililokuuliza.
Mungu kataka tu kuwatupa duniani huku akijua outcomes yake? Kama alijua inamaana alitaka iwe hivyo, sasa kwanini atoe adhabu?

And by the way, Steve Jobs alikuwa hajui kama kuna tunda linaitwa Mango? Pineapple? ama?
akikwambia kua alifanya kwa kubahatisha tu na wala hakutegemea kama jina apple lingekua popular kiasi hiki utasemaje?? Au akikwambia kua ilikua ni ngumu kutafakari wazo hilo peke yake mpaka alipohusisha mawazo ya wadau wake wakaribu ambao kati yao kuna waliotaja mango na pineaple lakini zilipopigwa kura ndio wazo la apple likspitishwa. Wewe utasemaje ukiambiwa hivyo

Kwani si vyombo vinapelekwa kila miaka kuchunguza uko nje? Hebu nitajie basi sayari yenye civilization unayoijua wewe.

Unaviamini hivyo vyombo kua vinatoa majibu ya hakika??


Kufariki ndio cycle ya dunia, ingekuwa hakuna kufa, dunia ingejaa mara moja tu
na ndio lengo la mungu kwa mujibu wa dini zenu kawaruhusu binadamu waijaze dunia. Uneona utata hapo?

na kwanini basi isikae kwenye hio right place uitakayo wewe? kwa sababu kama hakuna purpose ulimwenguni kwanini tufe tupishe wengine waje? and by the way, WHERE IS THE RIGHT PLACE ACCORDING TO YOU?

what makes you think there must be somewhere better than here??

Inventions za imaginary heaven zilitokana na swali la namna hii


Kwa vile umekubali kuwa lile jengo lina wajenzi, basi na Ulimwengu una mjenzi wake, na ndio maana akaiweka dunia hapa ilipo ili mimi na wewe tuishi. Tofauti ya hao wajenzi, wao ni VIUMBE lazima Viwe na chanzo.
na kwa vile nimekubali kua lile jengo lina mjenzi wake basi na huyo mjenzi lazima awe na mjenzi sake siyo??

Ulimwengu una mjenzi wake na huyo mjenzi naye anamjenzi wake tuko pamoja mpaka hapa??


Yupo aliekuwa sio Kiumbe nae ni Allah aleiumba mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake. Muumbaji hana Muumbaji.
Hapa umetumia logic au fallacy ya kidini??

Logic inasema hakuna kisicho kiumbe sasa kivipi allah huyo asiwe kiumbe je ni kwasababu hayupo??

Kuumba ni from nothing to something.
and nothing can come from something to nothing unskubali hili??


Kwanini nisikulaumu wewe kwenda kununua kitu usichikijua? Mbona mimi binafsi washkaji wananifuata wananambia kuna iphone hii hapa ni original ama vipi? ina icloud ama vipi? na nawapa majibu, tena watajua wenyewe kama watanunua ama la, lakini hawana wa kumlaumu zaidi ya nafsi zao.

jaribu kusoma vizuri nachokiandika hususani katika mifano maana nsona unspoteza umakini

Mfano umezungumzia makubaliano kati yangu mimi na wewe kua tununue simu aina moja iphone 11 katika duka moja na wote tumeuziwa kwa bei moja. Baada ya kufika nyumbani mimi nikagundua kua nimepigwa kwa kuilinganisha na yako. Kisha nikakuuliza je hapo kosa la nani kati ya wauzaji na mimi mnunuzi? Huku nikikusudia kua kati yangu mimi niliyepewa ubongo wenye errors na mungu aliyenipa huo ubongo nani mwenye makosa?

Wewe unasema utanilaumu mimi kwenda kununua kitu nisichokijua, hio inamaana utanilaumu mimi kwa kupewa ubongo na mungu wenye kuzidiwa ufanisi na ubongo wako??


vipi wao uwaite wajinga wakati wewe ndio wamekufanya uwe mjinga? Utakuwa mjinga kwenda kununua kitu bila kuhakikisha wakati kuna njia tayari za kujua kama kitu feki ama si feki. Yaani utoke na miguu yako miwili ukafanye dhambi halafu useme Mungu ndo kajua ivo? huo si ujinga?

kivipi aliyekufundisha unyama wa kuua watoto bila hatia asiwe mnyama??

Kivipi aliyekufundisha wizi awe mwema wakati bila yeye usingeiba??

Inamaana hata misingi ya dini yenu inaruhusu kufundisha mtu kuua kwasababu mtu huyo akiua wewe hauhesabiwi kua umekosea??

Kweli ujinga mzigo beba hata sikupokei, kusema chanzo cha ubaya si ubaya kiukweli umeniacha hoi...

Uwezo wa kurudi nyuma ya muda unao? Na ukiwa nao utakuwa huna uhuru wa kurud nyuma?
Uwezo wa kurudisha waliokufa unao? ungekuwa na uwezo huo nani angekuzuia?
Uwezo wa kuchagua kuumwa au kutoumwa unao? ungekuwa unao, nani angekuzuia?[/QUOTE]
Ulisema uhuru ni uwezo wa kuamua kufanya kile ukitakacho, kwa maana hiyo uhuru na uwezo ni vitu ambavyo vinafungamana

Kwaiyo kama binadamu hana uwezo basi hawezi kua na uhuru, na kama ana uhuru basi lazima awe na uwezo.

Umesema tumepewa uhuru wa kuchagua mema na baya sasa nikaamua kuchagua kurudi nyuma ya muda je ataniwekea kizuizi kwasababu ni jambo baya?? Hapana hawezi kukuzuia kwasababu ulipewa option ya kuchagua hadi mabaya. Na kama ni jambo zuri iweje tena alipige pin lisiwezekanike wakati ni moja ya chaguzi alizonipa nijichagulie as long as yawe mema au mabaya?? Sasa kwanini kila jambo lisiwezekanike kufanyika kama kweli kanipa uhuru??

Sasa kama sina uwezo wa kufanya hayo nitakayo utasemaje kuna uhuru??



Unazungumzia UHURU AU UWEZO?
Hii point ipo in red nasubiri jibu kwa hamu hasa. I need your answers on this point to point.

nazungumzia vyote uhuru na uwezo ni sawa na abdala kumuita dulla




Utafanyaje tofauti na alivyojua kuwa utafanya kwa maamuzi yako mwenyeo?

siwezi kufanya tofauti kwasababu hakuna uhuru wakuchagua kufanya tofauti


Hio kanuni ya kuwa ili uhuru wakuchagua uwepo basi Mungu hatakiwi kujua unachochagua umeitoa wpi?
kupitia logic

kwa sababu Uhuru haihusiani na kujulikana chaguo lako. Kwani mfano mtu akijua kuwa unampenda Fulani, manake huna uhuru amekuchagulia yeye umpende?
ujuzi wa mtu unaweza kukosolewa kwa kwenda kinyume lakini mungu alijua tukio ulilolifanya leo kabla hujazaliwa hivyo kivyovyote huwezi kuliepuka kwasababu kuepuka kwako kutam prove wrong mungu aonekane ni mbshatishaji


Sijaelewa na ndio maana nataka ufafanue vizuri. Unajuaje kuwa umeenda tofauti na alivoona Mungu?
ok twende taratibu ili uelewe

Unajua kua dhambi yeyote ukiifanya bila kutubu itakupeleka motoni au hujui??


Umeambiwa kuna Mungu, haya nikuulize umesoma wapi habari zake?
Kusoma habari si ishu ishu ni uhalisia wa hiyo habari

halafu pia habari za mungu zipo nyingi kulingana na utamaduni fulani sasa wewe ulishasoma habari zote zinazohusu mungu??

Kwani wewe hujasoma habari ya panya mabaka aliyemvisha paka kengele, hujamsoma pazi na jogoo??


Sasa mimi nimekuuliza swali ila naona unalijibu kwa woga. Basi ngoja nikwambie jibu langu halafu nini utaniuliza na jibu lake litakuaje;
kuhusu woga sina hata chembe, nakomaa na mjadala bila kua na wenge...

Mimi: Haiwezekani kitu chochote kikajiumba chenyewe bila kuwepo chanzo
sawa nakubali, lakini unaweza kuniambia chanzo cha huyo mungu unayemuamini??

Scars: basi Mungu nae atakua ana chanzo chake
sahihi kabisa kwasababu msingi wa logic ndio unaotupa jibu

Mimi: Mungu sio Kiumbe, kisichoumbwa hakina source.
hakuna kisicho kiumbe, kila kitu ni kiumbe eidha kiwe hai au kisiwe hai

Pia nakurahisishia kwa kuweka swali liwe clear

Kila kilichopo ni lazima kiwe na chanzo?


Hujanijibu swali lakini? Mungu hujamuelewa unaenda msikitini kufanya nini? Kusali? Basi itakuwa umemuelewa na ndio maana ukaenda msikitini na ukasali. Lakini vipi unampinga Mungu halafu unasema kuwa hayupo bila ya kuwa na hoja yoyote yenye mashiko na bila kuthibitisha kutokuwepo kwake? vipi baada ya ishara zote zilizoletwa wewe ukazikataa? ivi kweli itakuwa hujajua kama kuna Mungu?
Naweza kwenda msikitini kwasababu hawakatazi kuingia na sio kwamba naenda kwa kigezo cha kusali.

Sasa kama sijamuelewa kwanini anihukumu kwa kutomuelewa wakati alikwishajua kua hilo??

Ikiwa unajua kuwa hakuna kiumbe kinachoweza kujiumba chenyewe, tena vipi ukatae uwepo wa Muumbaji?

ni kwasababu naelewa kua hakuna kisicho kiumbe

Dhaifu mbele ya nani?

dhaifu kiujumla, haijalishi mbele ya nani.


Ukishajua kua wizi ni jambo baya utaweza kuuliza kua wizi mbele ya nani???



na udhaifu huo ndio unaopelekea wewe ufanye dhambi siyo?

Hakuna kosa kutamani kuwa Mungu angekuumba Tajiri ama vile upendavyo. Ameshasema mwenyewe duniani ni mapito, atakaefuzu, atakwenda peponi
Kwaiyo mungu hataki watu wote waende peponi na ndio maana kaweka kizuizi cha kuwachuja ili sengine wasiende??

huko unachotaka wewe basi utapata. Ama kama mwenyewe unaona bora uende tu motoni, basi umechagua mwenyewe usimlaumu yeye kujua wewe utaishia motoni. kwa sababu ndivyo ulivotaka mwenyewe.
kivipi tena niwe nimechagua mimi wakati mungu ndiye kaniumba nikiwa mdhaifu na kunichagulia ubongo wenye udhaifu usioweza kufata kila jambo ambalo yeye analitaka??
 
Kwanini mungu aweke kipaumbele kwenye kutubu kuliko kuzuia baya ili kumuepusha huyo mtu asilifanye??

Kwaiyo mungu anaweza akajua kua kesho utamuua mama yako bila hatia halafu akaacha tu wewe ufanye mauaji ili akuone kama utatubu?? Yani mungu anaruhusu mtu mwingine afe bila hatia ili akupime kama utatubu???

Logic gani hapa itamkubali mungu wa dzaini hii??
Mwenyewe amependa iwe hivo, au umesahau kama Mungu anafanya atakavyo na sio utakavyo wewe? Wewe huoni kuwa akifanya utakavyo wewe, na mwengine atakuwa na vile anavyotaka yeye sasa kila mmoja akiwa na atakavyo itakuaje?

Kipi kigumu katika sentensi hii "Mungu anafanya atakavyo"

Hili nimelitolea majibu more than two times labda nisisitize tena

Kwanza kwa swali hili linaonesha kabisa hata wewe una matatizo ya ubongo, maana nimekuelezea kwa urefu sana lakini bado umeonekana kutokuelewa.

Ubongo unamapungufu mengi hauoneshi kama umeumbwa na Omnipotent power. kuanzia uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu hadi uwezo wa kustahimili hali ngumu pasipo kuruhusu matatizo katika mfumo wake

Unavyozaliwa ulikua na ubongo lakini je unakumbukumbu yeyote unayoikumbuka katika tukio la kuzaliwa kwako ukiachana na masimulizi kutoka kwa mashuhuda walikokuwepo siku hiyo?? Bila shaka huwezi na ndio maana hata vitu nilivyokuelezea mda mchache uliopita umeshindwa kuvikumbuka au hta kuvielewa kwasababu ya mapungufu ya ubongo

Mungu (naashumu kama yupo japokua hayupo) alijua hilo kua binadamu amewapa uwezo mdogo wa kiufanisi katika ubongo wao, alijua kua katika vitu nitakavyo wapa hawatoweza kuvifanya kikamilifu hivyo kama mungu alitaka watu wafanye vitu kikamilifu kama apendavyo, basi alipaswa kuweka mfumo ulio kamili usio kosea wala kusahau ili watu wafanye kile akitakacho bila kizuizi. Lakini hakufanya hivyo unafikiri ni kwanini?? Ukitumia logic utagundua mungu alitaka tufanye makosa, na kweli tukafanya makosa ambayo yeye ameyaruhusu yafanyike sasa kivipi atuadibu?? Hapa logic inakataa huu udwanzi wa kindeezi uliojaa upuuzi unaoonesha mungu si mjuzi na anafanya mambo ya kishenzi ambao hata sisi hatuwezi, je huyu anastahili kuitwa mwenyezi??
Umelitolea majibu ama unaendelea kusisitiza kile ukitakacho wewe Mungu awe? Maana nilikuuliza swali very simple. Kwanini Steve Jobs kaamua aite kampuni yake Apple na asiite tunda jengine au kitu chochote kile, ukaanza kuuzunguka mbuyu.

Mapungufu yapi ambayo hayaoneshi kuwa umeumbwa na omnipotent? Mbona ubongo wa PC tu unahitaji muundaji ili uweze kufanya kazi tena huu wa kiumbe usiwe na Muumbaji. Yaani Undezi ni pale mifano hai ipo ila unaipuuza, Mugnu hawezi kuwa mshenzi, mshenzi ni yule ambae mifano ipo usoni mwake lakini anaipinga bila sababu za msingi.

Wewe kama si mshenzi utakuwa nani umpangie Mungu utakavyo? Unashindwa kuipangia utakavyo Familia yako utaweza ya Mungu kweli?

Ukitumia akili utagundua kuwa Mungu alitupa Ubongo kwa ajili ya kutafuta elimu na kujifunza, hakutupa ubongo watu wafanye makosa, huo ndio undezi wenyewe, hebu nijibu swali hili, kwanini unawaza kufanya makosa tu na sio kufanya mema?

kwanini kusajiliwa kuwe muhimu kuliko ubaya wa kitu???

Kila kilicho sajiliwa na kuhalalishwa kitakua halali kwako kwasababu tu kimesajiliwa na shirika fulani au uongozi fulani???

Utakua tayari kufanya jambo lolote ilimradi tu lisajiliwe?? Umtimamu?
Wewe umesema Uislam ni Taasisi, sasa labda imesajiliwa ndio maana nkakuuliza hio Taaisi imesajiliwa nani?

Unajua maana ya Dini na maana ya Taasisi?

purpose kwani ni lazima liwe mungu??

Naweza kuishi kwa lengo la kujifunza vitu nisivyovijua na kusaidia wenye shida bila kutegemea malipo kutoka kwa mungu (ambaye hayupo) shida ambazo wakienda misikitini wala makanisani hawatasaidiwa zaidi ya kuambiwa wafunge na kusali, yaani mtu analia njaa halafu unamuambia funga bila kula allah atakunusuru what a joke but I ain't laughing??
Its a Joke on you, spending all those years on earth and one day you die and then nothing? What is the point?

umeona hoja zingine unazijibu mwenyewe, yani kumbe watu sio tu moto ambao hawauogopi bali hata umasikini nao hawaogopi aisee mi nikua sijui. sasa utawatisha kwa kipi unadhani au shumileta na saladini wa zamani??
Watatishwa hio siku watakayoingia kaburini, ndipo mtakapojua nani kala hasara. 😀

invisible unicorn, shetani na mungu wote ni character wasiokua na maana kwasababu hawapo zaidi ya hadithi kama kirikuu
Mungu na Shetani hawana maana kwako tu ULIECHAGUA kutoamini uwepo wao. Uko HURU kuchagua ivo 🙂

Ok nitafanya hivyo ila kabla sija move on nataka nijue uliuelewaje ule mfano niliokupa?
Jibu swali na ukihisi sijaelewa rudia kufafanua

mbona unanirudisha kule kule niliko kujibu swali hili?? Hivi ni kwamba huelewi kwa bahati mbaya au kusudi tu ili usionekane umeshindwa hoja??

Rejea mfano niliokupa kuhusu kuua na kujiua utaelewa
Hakuna hoja ulioitoa ikanishinda hadi sasa, kikubwa naona kuwa unarudia rudia point zako ambazo tayari zimeshatolewa ufafanuzi kitambo tu. Lakini ni majibu yanayokuchukiza kwaio huyakubali, 😀

wewe unajua unachokiamini?? Hapo hakuna logic kwenye hoja yako, huwezi kuamini na kujua at the same time
Huwez kuamini na kujua? 😀 we jamaa kituko kweli. Kanuni ipi inasema ivo?

Kwaio jirani yangu akisema kuwa " hapa mtaani mwizi kapita kwangu kuniibia" uku mimi nikiwa nimeshuhudia mimi mwenyewe nimeibiwa na akaruka kwake, huwa siwezi kuamini alichonambia?

Yaani, KUJUA, KUPANGA, KUAMINI, UHURU hujui kabisa maana ya ivi vitu halafu unataka mjadala?

sijishugulishi na kilimo, vipi wewe unajishughulisha na uuzaji bangi??
Kwaio wewe unaamini Ulimwengu unae muumbaji? Hili swali linahitaji majibu, usiogope.

Ni kweli sina sifa kwasababu i do exist and im not an imaginary being that cant be proved.
Imaginary kwako kwa kuchagua kuwa mjinga.

na ndio lengo la mungu kwa mujibu wa dini zenu kawaruhusu binadamu waijaze dunia. Uneona utata hapo?
Onesha hilo lengo.

na kwa vile nimekubali kua lile jengo lina mjenzi wake basi na huyo mjenzi lazima awe na mjenzi sake siyo??

Ulimwengu una mjenzi wake na huyo mjenzi naye anamjenzi wake tuko pamoja mpaka hapa??
Wapi hufahamu nlipokwambia kuwa Mjenzi wa Ulimwengu sio Kiumbe? Sasa kama sio kiumbe atajengwa na nani? 😀

Unataka kufananisha na kiumbe chake?
KWANI KISICHOUMBWA KINAMUUMBAJI?

.kwa mujibu wa dini yenu mungu sio mpangaji wa maisha ya binadamu??

Kwa mujibu wa dini zenu kuna kitu chochote kinachoweza kufanyika bila mungu kukiruhusu???
Likikukuta ujue Mungu kaliruhusu ilo ndio. RUHUSA sio UPANGAJI.

sijakataa hilo lakini hujui kua linaongeza uzito katika hoja zangu, yaani unapoonesha weakness za binadamu unakua unamshusha mungu wako viwango unamfanya ainekane kama fundi maiko kwasababu kwa mujibu wa dini zenu mimi na wewe ni kazi ya mikono ya huyo mungu wenu.

Ukweli haliongezi uzito zaidi ya kuzidi kukufunga.

Unaposema kuwa namshusha Mungu uwezo wake kwa kuonesha weakness za Binaadam, naomba nikuulize, unamfananisha na nani?

Fundi Maiko ametengeza binaadam?

Hapa umetumia logic au fallacy ya kidini??

Logic inasema hakuna kisicho kiumbe sasa kivipi allah huyo asiwe kiumbe je ni kwasababu hayupo??
Nimetumia logic tu hapo, yaani bila hata maandishi ya kidini. Ili ulimwengu uwepo, lazima pawe na alieuumba. Na ili huyu alieumba ambae amesema kuwa hajazaa wala hajazaliwa basi awe hajaumbwa, kwa sababu kama angekuwa ameumbwa basi angekuwa na muumbaji wake mpaka infinity na ulimwengu ungekosa order kabisa.

Nitakubali kua gari lina muundaji kwasababu haiwezekani kitu kikawepo bila chanzo.
nikikubali kua ulimwengu una muumbaji wake halafu nikakuambia na huyo muumbaji naye ana muumbaji wake utakubali?? Kama utakataa nami ntakuona mjinga
Wewe utaniona mimi mjinga, lakini mimi nakuona wewe mjinga, kwa sababu kwenye post yangu nimekwisha kwambia zamani jinsi utakavokuja kuuliza, sasa sijui namie nimekupangia 😀

Muumbaji kama sio kiumbe ataumbwa na nani?

jaribu kusoma vizuri nachokiandika hususani katika mifano maana nsona unspoteza umakini

Mfano umezungumzia makubaliano kati yangu mimi na wewe kua tununue simu aina moja iphone 11 katika duka moja na wote tumeuziwa kwa bei moja. Baada ya kufika nyumbani mimi nikagundua kua nimepigwa kwa kuilinganisha na yako. Kisha nikakuuliza je hapo kosa la nani kati ya wauzaji na mimi mnunuzi? Huku nikikusudia kua kati yangu mimi niliyepewa ubongo wenye errors na mungu aliyenipa huo ubongo nani mwenye makosa?
Mungu hajakupa ubongo wenye errors lakini, amekupa ubongo wenye kupata elimu, sasa kama hukutafuta elimu utamlaumu nani?

kivipi aliyekufundisha unyama wa kuua watoto bila hatia asiwe mnyama??

Kivipi aliyekufundisha wizi awe mwema wakati bila yeye usingeiba??

Inamaana hata misingi ya dini yenu inaruhusu kufundisha mtu kuua kwasababu mtu huyo akiua wewe hauhesabiwi kua umekosea??

Kweli ujinga mzigo beba hata sikupokei, kusema chanzo cha ubaya si ubaya kiukweli umeniacha hoi...
Wapi amekufundisha kuuwa watoto bila hatia?
Wapi kakufundisha wizi?

Wapi huo msingi unaozungumzia ni upi?

Uwezo wa kurudi nyuma ya muda unao? Na ukiwa nao utakuwa huna uhuru wa kurud nyuma?
Uwezo wa kurudisha waliokufa unao? ungekuwa na uwezo huo nani angekuzuia?
Uwezo wa kuchagua kuumwa au kutoumwa unao? ungekuwa unao, nani angekuzuia?
Ulisema uhuru ni uwezo wa kuamua kufanya kile ukitakacho, kwa maana hiyo uhuru na uwezo ni vitu ambavyo vinafungamana

Kwaiyo kama binadamu hana uwezo basi hawezi kua na uhuru, na kama ana uhuru basi lazima awe na uwezo.

Umesema tumepewa uhuru wa kuchagua mema na baya sasa nikaamua kuchagua kurudi nyuma ya muda je ataniwekea kizuizi kwasababu ni jambo baya?? Hapana hawezi kukuzuia kwasababu ulipewa option ya kuchagua hadi mabaya. Na kama ni jambo zuri iweje tena alipige pin lisiwezekanike wakati ni moja ya chaguzi alizonipa nijichagulie as long as yawe mema au mabaya?? Sasa kwanini kila jambo lisiwezekanike kufanyika kama kweli kanipa uhuru??

Sasa kama sina uwezo wa kufanya hayo nitakayo utasemaje kuna uhuru??

[/QUOTE]
Kutokuwa na uwezo wa kitu haina maana ya kuwa na uhuru au La. Kuna swali mbele ya swali na hakuna hata moja ulilojibu.

Mimi naendelea kukujibu, i hope na wewe utayajibu instead of kuzunguka mbuyu

Sio kila jambo linawezekana kwa sababu ya limitation aliokuwa nayo kiumbe. lile ambalo analiweza hazuiliwi. Mbona binadaama tumetuma satellite na imeshatoka kwenye solar system? Miaka 1000 iliopita haikuwezekana.

Nitasema unao uhuru kwa sababu kama ungekuwa na uwezo wa kurudisha mda nyuma ungelifanya hilo lakini hujawa nao uwezo huo.

nazungumzia vyote uhuru na uwezo ni sawa na abdala kumuita dulla
Sio sawa sawa kabisa.

Na Abdalla kumuita dulla sio sawa 😀

siwezi kufanya tofauti kwasababu hakuna uhuru wakuchagua kufanya tofauti
huwezi kufanya tofauti kwa sababu hujui anachojua.

kupitia logic
misuse of logic

ujuzi wa mtu unaweza kukosolewa kwa kwenda kinyume lakini mungu alijua tukio ulilolifanya leo kabla hujazaliwa hivyo kivyovyote huwezi kuliepuka kwasababu kuepuka kwako kutam prove wrong mungu aonekane ni mbshatishaji
Kwani mfano mtu akijua kuwa unampenda Fulani, manake huna uhuru amekuchagulia yeye umpende? Jibu hili swali

sawa nakubali, lakini unaweza kuniambia chanzo cha huyo mungu unayemuamini??
Mungu ni Eternal hana chanzo na sio kiumbe

sahihi kabisa kwasababu msingi wa logic ndio unaotupa jibu
Ikiwa humjui Mungu, sikulaumu ukiuliza ivo. Ili uwe Mungu basi uwe na sifa za kiungu.

Sasa kama sijamuelewa kwanini anihukumu kwa kutomuelewa wakati alikwishajua kua hilo??
Unazungumza ikiwa hujatafuta elimu!

dhaifu kiujumla, haijalishi mbele ya nani.
Injaalisha dhaifu mbele ya nani
Ukishajua kua wizi ni jambo baya utaweza kuuliza kua wizi mbele ya nani???
Ukishajua Wizi basi unajua usio wizi.

Kwaiyo mungu hataki watu wote waende peponi na ndio maana kaweka kizuizi cha kuwachuja ili sengine wasiende??
Ameshakuwekea njia ya kupita ya kwenda peponi na nyingine ya motoni, yes ukichagua ya kwenda motoni basi anataka akakuchome.

kivipi tena niwe nimechagua mimi wakati mungu ndiye kaniumba nikiwa mdhaifu na kunichagulia ubongo wenye udhaifu usioweza kufata kila jambo ambalo yeye analitaka??
Amekwambia ukiasi utaenda motoni, na amekwambia ukitii utaenda peponi. Sasa wewe unataka kufanya lipi?
 
Mwenyewe amependa iwe hivo, au umesahau kama Mungu anafanya atakavyo na sio utakavyo wewe? Wewe huoni kuwa akifanya utakavyo wewe, na mwengine atakuwa na vile anavyotaka yeye sasa kila mmoja akiwa na atakavyo itakuaje?
Inamaana alishindwa kubalance kitu atachokitaka yeye namimi nikitake bila kuhoji kinyume chake??

Kipi kigumu katika sentensi hii "Mungu anafanya atakavyo"

ugumu unakuja pale ambapo unasema mungu hufanya kile atakacho na huwezi kuamua kufanya kitu chochote tofauti na mapenzi yake halafu at the same time unasema una uhuru wakuchagua
 
Umelitolea majibu ama unaendelea kusisitiza kile ukitakacho wewe Mungu awe? Maana nilikuuliza swali very simple. Kwanini Steve Jobs kaamua aite kampuni yake Apple na asiite tunda jengine au kitu chochote kile, ukaanza kuuzunguka mbuyu.

steve job anauwezo wote na ujuzi wote na hakosei??

Ikiwa kama desire yake ni kutaka kila mmoja afurahie jina hilo lakini akawa hana uwezo wote wa kufanya kila mtu afurahie hilo jina kama atakavyo utamlaumu??

Mapungufu yapi ambayo hayaoneshi kuwa umeumbwa na omnipotent?

yoyote yanayoitwa mapungufu ambayo yapo katika ulimwengu ambao unaodaiwa kua umeumbwa na mungu haijalishi aina gani ya mapungufu



Mbona ubongo wa PC tu unahitaji muundaji ili uweze kufanya kazi tena huu wa kiumbe usiwe na Muumbaji.
Complex ikihitaji muundaji hata mungu naye ni complex kwasababu kaweza kuumba mtu unaweza kuniambia mungu kaumbwa na nani??

Yaani Undezi ni pale mifano hai ipo ila unaipuuza, Mugnu hawezi kuwa mshenzi, mshenzi ni yule ambae mifano ipo usoni mwake lakini anaipinga bila sababu za msingi.
actually hawezi kua mshenzi kwasababu hayupo

Wewe kama si mshenzi utakuwa nani umpangie Mungu utakavyo? Unashindwa kuipangia utakavyo Familia yako utaweza ya Mungu kweli?
Kama ushenzi huja kwa kumpangia mtu, basi hata wewe ni mshenzi maana unanipangia niende kuipangia familia yangu bila mimi kujipangia kwa hiari yangu


Ukitumia akili utagundua kuwa Mungu alitupa Ubongo kwa ajili ya kutafuta elimu na kujifunza, hakutupa ubongo watu wafanye makosa, huo ndio undezi wenyewe, hebu nijibu swali hili, kwanini unawaza kufanya makosa tu na sio kufanya mema?
ukitumia akili utagundua mungu hayupo maana akili itadai uthibitisho na sio kuamini tu bila evidence yeyote. Na wasiokua na akili hawajishughulishi na kutafuta ukweli wao kazi yake ni kuamini tu
 
Unajibu kwa kukurupuka hujui hata mantiki ya hilo swali nililokuuliza na sizani kama umelielewa
Mimi sijazungumzia kubadilika kwa maono au lah, na ndio maana nilikua nasisitiza kuuliza kua kama naye anatabia ya kukosea ili niweze kujenga hoja kupitia jibu utalonipa
Nimeuliza kama mungu anajua kila kitu na hakuna kitu utachokifanya leo hii kikawa kigeni machoni mwake kwasababu yeye ni mungu asiyekosea alichokiona ni lazima kiende sawa sawa. Sasa wewe leo hii ukiamua kutoenda kanisani au msikitini utakua umebadilisha chochote katika ujuzi wake kuhusu hatma yako???
Kwa ufupi ni hivi; elimu ya Mungu, ujuzi wake na maarifa yake ni tofauti na sisi binadamu.

Maarifa ya binadamu kwenye kujua mwanzo na hatma ya kitu eidha atumia historia, au tafiti ya hicho kitu na mfanano mwengineo kama huo

Mfano rahisi chukulia unatizama tamthilia ambayo ni mpya kabisa kwa maana hujawahi kuiona. Hutojua mwanzo wa hiyo tamthilia utakuaje, mwenendo wa hiyo tamthilia utakuaje na hutojua mwisho wa hiyo tamthilia utakuaje.

Lakini kwa Mungu hiyo siyo case! Kwa sababu maarifa yake, ujuzi wake na elimu yake unao uwezo wa kuona hayo yote! Hatua kwa hatua na jinsi mwanzo utakavyokuwa na jinsi mwenendo wa kitu utakavyokua na hatma yake itakuwa ni ipi.

Mwanadamu amepewa uhuru wa kufanya mambo na katika hilo Mungu hamuingilii binadamu, ana muacha binadamu afanye atakavyo. Kama binadamu A akiingia motoni na binadamu B akaingia peponi lawama usimrushie Mungu kwa vile tayari ameshaandika A ni wa motoni na B wa peponi.

Ni kweli Mungu ameshandika. Lakini kuandika kwake si kwamba tayari ameshakuhukumu kwamba ni wa peponi ama motoni, isipokuwa maarifa, ujuzi na elimu yake Mungu imeyatangulia haya ambayo binadamu anayoyafanya. Tayari ameshaona present yako, past yako na future yako na mwenendo wako utakuwaje na hatma yako itakuaje.

Tunachofeli ni kwamba God's thinking tunaiweka daraja moja na human's thinking pasipo kujua kwamba binadamu hawezi Ku' think kama Mungu. Kwa sababu binadamu tupo kwenye specific spot in time. Tunachogundua sisi ni kwa kupitia tuliyoyapitia.

Lakini Mungu yupo nje ya time. Anaona mwanzo utakuaje, na anaona na mwisho utakuaje. That's why tayari ameshaandika kila kitu na hatma ya hivyo vitu vitakuaje.
 
Its a Joke on you, spending all those years on earth and one day you die and then nothing? What is the point?

Hiyo ndiyo dhana iliyotumika kumuumba mungu baada ya watu wapumbavu wasiokua na fikra pana kufikiri kua ni lazima kuwe na life purpose and others bullshit[/QUOTE]
 
Mungu na Shetani hawana maana kwako tu ULIECHAGUA kutoamini uwepo wao. Uko HURU kuchagua ivo 🙂

Kisichokuwepo hakina maana, kwani wewe invisible unicorn ana maana kwako??
 
Jibu swali na ukihisi sijaelewa rudia kufafanua

Unajuaje sijakujibu na sio kwamba nimekujibu kupitia mfano ila wenge lako tu limekufanya usione kama hujajibiwa??
 
Hakuna hoja ulioitoa ikanishinda hadi sasa, kikubwa naona kuwa unarudia rudia point zako ambazo tayari zimeshatolewa ufafanuzi kitambo tu. Lakini ni majibu yanayokuchukiza kwaio huyakubali, 😀

ni kweli hakuna hoja iliyokushinda kwasababu hatakuiangaikia kuielewa hujaweza
 
Huwez kuamini na kujua? 😀 we jamaa kituko kweli. Kanuni ipi inasema ivo?

Kwaio jirani yangu akisema kuwa " hapa mtaani mwizi kapita kwangu kuniibia" uku mimi nikiwa nimeshuhudia mimi mwenyewe nimeibiwa na akaruka kwake, huwa siwezi kuamini alichonambia?

Yaani, KUJUA, KUPANGA, KUAMINI, UHURU hujui kabisa maana ya ivi vitu halafu unataka mjadala?

Karudie shule nishakuwekea bench

imani na kujua ni vitu viwili tofauti
 
Back
Top Bottom