Athari za Majaji walioteuliwa na Hayati Magufuli


unataka tuandike unachopenda wewe.
Huna sababu ya kuandika ninachotaka mimi bali unatakiwa kuchangia hoja.

Kejeli, matusi, hufanywa na watu wasio na akili. Kutukana, hata kichaa anaweza, lakini kichaa hata siku moja hana uwezo wa kujenga hoja.

Anayetukana au kukejeli, ni uthibitisho usio na shaka kuwa kichwani kumepungua, na kwa vile JF, kimsingi ilianzishwa kama platform ya great minds, mtu wa namna hiyo ni misfit hapa.

Anaweza kusoma bila kuchangia kwa sababu hana uwezo wa kuchangia. Akitulia na kusoma kutoka kwa wenye uelewa, ataelelimika.
 
Tumewahi kusikia malalamiko kuhusu kada ya majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Malalamiko hayo, kwamba kuna majaji hawana viwango vya kiweledi vinavyotakiwa, yalitolewa bungeni, na mh. Tundu Lissu enzi hizo...
Wewe ni Mindi Kasiga?
 
Tumewahi kusikia malalamiko kuhusu kada ya majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Malalamiko hayo, kwamba kuna majaji hawana viwango vya kiweledi vinavyotakiwa, yalitolewa bungeni, na mh. Tundu Lissu enzi hizo...
Kuna taarifa za kuaminika zinadai kuwa wengi wa majaji walioteuliwa ni maofisa wa TISS
 
Ina maana majaji wote wameteuliwa na Magufuli, au una chuki na Magufuli! Uamuzi unapotolewa na jopo la majaji ambao hata hawakuteuliwa na Magufuli, wewe unasema nini juu yao!
Majaji wote wa Magufuli wa akawa lakini fulani. Wengine wameteuliwa kwa kusoma hukumu kwa Kiswahili.... That was Magufuli.
 
Majaji wanakandamizaje wapinzani wa serikali, toa mfano wa mpinzani aliyekandamizwa na jaji.
Mbowe amekandamizwa na majaji 3 mpaka sasa. Jaji Luvanda, jaji Siyani na yule jaji wa mahakama kuu alipotupa kesi ya kikatiba aliyofungua dhidi ya kutotendewa haki alivyokamatwa. Mifano ipo mingi sana
 
Kama sijakosea kuna Jaji wa Mahakama Kuu alipandishwa cheo na Magufuli kwa sababu eti aliandika hukumu kwa KISWAHILI!!!
Naam. Cha kushangaza, kazi kuu ya Jaji ni kutoa haki. Sasa huyu anapewa ujaji kisa kaandika hukumu yake kwa kiswahili. Hatujui ni kwa weledi kiasi gani hukumu yake ilikuwa. Inawezekana ilikuwa hukumu mbovu, ila tu imeandikwa kiswahili .
Halafu huyu Magu anajifanya mtetezi wa Kiswahili, wakati ameanza kuongea kiswahili baada ya kushindwa kuongea kiingereza kinachoeleweka
 
Msoga group linapambana kutia kiwi nyeusi kwenye legacy ya Mwendazake.
walishachelewa wananchi walimwelewa na UN ilimuelewa ikamuenzi.
Mtu kashiba magimbi ataweza?
Eti msoga group! Yaani wewe unafikiri kila anayemkosoa Magu ni msoga group? Magufuli alikuwa jambazi na muuaji. Sabaya kaweka wazi aliyekuwa anamwelekeza. Nakubaliana na wewe wananchi wanamjua Magu. Naam, wanajua kwamba ni mwizi, fisadi, jambazi. Magu mwenyewe alijua wananchi hawamtaki, ndio maana alipora uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Kama kweli angeamini anakubalika, ilikuwaje awaogope watu aliofanya kila njia kuwamaliza kwa kuwafunga, kuwahonga wajiunge ccm, kuwateka na hata kuwaua, na kuwazuiavwasifanye shughuli za siasa kwa miaka 5, wakati yeye masaa 24 kila siku anatangazwa natv, redio, magazeti?
 
Ina maana majaji wote wameteuliwa na Magufuli, au una chuki na Magufuli! Uamuzi unapotolewa na jopo la majaji ambao hata hawakuteuliwa na Magufuli, wewe unasema nini juu yao!
Kila uamuzi tunauangalia. Inawezekana wateule wa Magufuli wakatenda haki, na hapo hakuna atakayelalamika. Lakini malakamiko yanakuja kwa sababu imekuwa trend kwa majaji hasa wa Magufuli kutotenda haki. N

Na kwa kweli haishangazi, maana Magufuli huwa ni mtu mbabe. Amewahi kutamka anatamani angekuwa IGP. Aliwaagiza polisi wawafungulie kina Mbowe kesi ya mauaji ya Akwilina. Huwa anakerwa na maamuzi ya mahakama yasiyoendana na utashi wake.
 
Kasema nini...?

Na wewe unasema nini kama kujibu alichosema mwenzako?

Au jibu la hoja ya mwenzako (mleta mada kuu) ndicho hiki ulichoandika?

Hili wala halina uhusiano na sheria. Magufuli alitaka na aliutikisa sana mfumo wa utoaji haki Tanzania (Tanzania's justice system) na kuingiza siasa mahakamani...

Mathalani, kama wewe kweli ni mjuvi wa sheria, uamuzi wa kesi ndogo ya shauri la ugaidi wa Freeman Mbowe na wenzake wiki moja iliyopita wa Jaji Kiongozi Siyani Mutapha, ulijengwa ktk misingi ya sheria gani kama si "kudhani" na "kuhisi" tu kama alivyokuwa anasema mwenyewe siku hiyo akisoma hukumu yake?

Wewe unadhani ni kwanini Jaji mzima anashindwa kuzingatia sheria ktk kuamua kwake shauri fulani specific kwa hili la Ugaidi wa Mbowe?

JIBU NI RAHISI TU: No professionalism bali ni rushwa ya Ki - Magufuli ya cheo ya NIPE, NIKUPE.

Kama huoni ukweli huu na ukaendelea kubisha just for the sake ya kubisha tu, basi utakuwa na ugonjwa ya "kukosa ufahamu" wa kupambanua mambo.
Ila huyo unayemjua yupo pamoja na wewe, hukumwelewa tu, alikuwa anamjibu mmagufuli mmoja
 
Mbowe amekandamizwa na majaji 3 mpaka sasa. Jaji Luvanda, jaji Siyani na yule jaji wa mahakama kuu alipotupa kesi ya kikatiba aliyofungua dhidi ya kutotendewa haki alivyokamatwa. Mifano ipo mingi sana
Elezea ilitakiwa hao majaji wafanyeje ili ionekane wamemtendea haki mbowe
 
Eti msoga group! Yaani wewe unafikiri kila anayemkosoa Magu ni msoga group? Magufuli alikuwa jambazi na muuaji. Sabaya kaweka wazi aliyekuwa anamwelekeza. Nakubaliana na wewe wananchi wanamjua Magu. Naam, wanajua kwamba ni mwizi, fisadi, jambazi. Magu mwenyewe alijua wananchi hawamtaki, ndio maana alipora uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Kama kweli angeamini anakubalika, ilikuwaje awaogope watu aliofanya kila njia kuwamaliza kwa kuwafunga, kuwahonga wajiunge ccm, kuwateka na hata kuwaua, na kuwazuiavwasifanye shughuli za siasa kwa miaka 5, wakati yeye masaa 24 kila siku anatangazwa natv, redio, magazeti?
Duh nilichangia mada yako bila kujua wewe ni mgonjwa

so sorry.
 
Eti msoga group! Yaani wewe unafikiri kila anayemkosoa Magu ni msoga group? Magufuli alikuwa jambazi na muuaji. Sabaya kaweka wazi aliyekuwa anamwelekeza. Nakubaliana na wewe wananchi wanamjua Magu. Naam, wanajua kwamba ni mwizi, fisadi, jambazi. Magu mwenyewe alijua wananchi hawamtaki, ndio maana alipora uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Kama kweli angeamini anakubalika, ilikuwaje awaogope watu aliofanya kila njia kuwamaliza kwa kuwafunga, kuwahonga wajiunge ccm, kuwateka na hata kuwaua, na kuwazuiavwasifanye shughuli za siasa kwa miaka 5, wakati yeye masaa 24 kila siku anatangazwa natv, redio, magazeti?
Kweli na CHADEMA,maana alizika chama hiki.
 
Back
Top Bottom