ATCL kuanza direct flights to Mumbai

ATCL kuanza direct flights to Mumbai

Ukienda huko kwa watalii wachache ndio wataongezeka...!!walikuwa hawaji partly because hakukuwa na direct flight.
Direct flight sio kizuizi cha kufika popote duniani, awamu iliyopita Emirates na Qatar zilikuwa zinaingia Mbili kwa siku na zimeshona,siku hizi zinakuja trip moja na hazishoni
 
Watalii hawashindwi kuja sababu ya kukosa ndege shida ni Yale makodi waliyoyaweka kwenye utalii,MBONA awamu iliyopita walikuwa wakija wengi sana kuliko awamu hii na kulikuwa hakuna ndege
Weka statustics za awamu iliyopita na hii hapa tuone
 
Nadhani hii route ni nzuri sana kwa kuanzia. Kla nikipanda ndege kutoka Doha, Addis Ababa etc inakuwa imejaza wachina na wahindi. Wakipata route ya direct to Dar wataitumia
Wanaoingia kwa wingi kwa siku ni wachina na wahindi kwa dar to India kwa direct fly ni mda mfupi sana hauzidi masaa matano,sio mbaya kuanzia,then nyingine iende direct to china
 
Weka statustics za awamu iliyopita na hii hapa tuone
Nenda body ya takwimu utazikuta,Emirates na Qatar zilikuwa zinakuja Mbili kwa siku zimeshona siku hizi zinakuja moja na abiria sio wengi,
 
Direct flight sio kizuizi cha kufika popote duniani, awamu iliyopita Emirates na Qatar zilikuwa zinaingia Mbili kwa siku na zimeshona,siku hizi zinakuja trip moja na hazishoni
Hivi kumbe Emirates zilikuwa zinatua JNIA mbili kwa siku kipindi JK? Hilo nimelifahamu leo, seriously!!!
 
Hivi kumbe Emirates zilikuwa zinatua JNIA mbili kwa siku kipindi JK? Hilo nimelifahamu leo, seriously!!!
Ndio walileta ndege 2 kuanzia 2014 hadi 2016 wakajitoa
Ilikuwa ya usiku na mchana
 
Hii ni Good timing maana tumeongeza kivutio kingine hapa nchini siku za hivi karibuni. Naamini wahindi wengi wanashauku kubwa ya kuja kuangalia mbwa koko (viumbe vipya)
 
Yaani mtu aache Emirates, Qatar na Etihad zenye Warembo na Huduma nzuri vile aje kupanda ATC yenye Wahudumu wazembe hivyo. Halafu KQ pamoja na bidii zote za kutangaza na lobying washindwe ATCL iweze !!! Endeleeni kuongeza hasara.
Mkuu uko negative mno sijui kwa nini.Kwani hao EMIRATES walianza vipi?
 
Ni shida sana ndege za moja kwa moja kwenda india, nimeshaenda mara kibao lazima upitie dubai ama abudhabi ni usumbufu sana. Na abiria ni wengi. Nakumbuka nliahirisha safari yangu siku moja ilikiwa saa 12 jioni, baadae nikaresume saa tatu usiku nikaambiwa ndege imejaa ilikuwa direct flight to bangarole
 
Tatizo letu
1. Tuko na mawazo hasi kila wakati hata jema lifanywe tutaliona baya na hiyo imetuathiri mpaka katika maisha yetu ya kawaida mtu akifanya hata jambo zuri tunaponda yaani utafikiri tumerogwa aisee.
2.Maneno mengi mno tunaongea sana vitendo sifuri tubadilike wandugu.Kwani hayo makampuni makubwa kama EMIRATES walianza kila kitu wanaweza? Au ndio vile tunapenda kusifia vya wengine vyetu tunaponda? Vijana tubadilike.
3. Vijana ifike wakati tubadilishe mindset sio kila kitu negative negative tu haitokaa ikatusaidia. Nia aibu kwa kijana kuwa na NEGATIVE ATTITUDE kila wakati utafikiri zuri hata moja hakuna.HATA SHETANI ALIWAHI KUWA MALAIKA.
 
Back
Top Bottom