Bi Rosemarie, naona wewe ni mdogo sana. Huyo si Mwarabu. Ni Mfalme Haile Selassie Rastafari wa Ethiopia. Huyo mbwa alikuwa ni mlinzi wake.Huyo mbwa ni wa nani?na huyo mwarabu ni mkoloni au?
Hivi ninyi Tanganyika inawahusu/ inawakwaza nini? Sisi wenyewe ndani ya Tanganyika tumetulia, ninyi visiwani mnatupigia kelele rudisheni Tanganyika, rudisheni Tanganyika. Haiingii akilini.Nazidi kuwashauri mrudishe Utaifa wenu wa Tanganyika.
Kwani hata mwanamke akiolewa na kisha kuachika basi anarudia lile jina lake la zamani.
KARIB TANGANYIKA
Huyo mbwa ni wa nani?na huyo mwarabu ni mkoloni au?
Wakati hali ya muungano ikiwa tete hebu tuchukulie umeshavunjika alafu mchakato wa kugombea uwakilishi visiwani utakuwaje wale wa kule vs wa jamhuri si patakuwa hapatoshi au watakata tena yaongezeke majimbo ya uwakishi kwa hili naona bora watatue kero za muungano mana ukivunjika wengine wakirudi kule watakosa pa kugombea na kukalia benchi....ni mtazamo tu[/QUOT
kaka utata utoke wapi wabunge wa znz wanaokuja katika bunge la jamhuri wanachaguliwa kutoka katika majimbo yao walioshinda kama wabunge uko znz, so muungano ukivunjika wanarudi kuwa wabunge katika majimbo yao waliyoshinda znz kwa kifupi hawa wabunge wa znz waliopo katika bunge la jamhuri wanakofia mbili, mosi ni mbunge wa jimbo flani znz, pili anachaguliwa na baraza la wawakilishi kuiwakilisha znz katika bunge la jamhuri,
Dawa ya Muungano ni kuuvunja tu. MUUNGANO! Hauna faida. Wananchi wa Zanz hawautaki. Viongozi wa Zanz wanautaka, sio kwa sababu wanaupenda, bali kwa sababu unawapa vyeo na mafedha ya kumwaga. Angalia, kutoka Zanz kwa sasa (ka-sehemu kenye watu laki 8, mara tano ya mkoa wa Mwanza wenye watu takribani milioni 4) kuna Makamu wa Rais wa Muungano, kuna Mawaziri 7 na manaibu kadhaa, mabalozi lukuki, makatibu wakuu wa wizara, majaji, wabunge 80 nk; huku MWANZA kuna waziri mmoja tu, wabunge 10. Usawa uko wapi? HAKUNA, MUUNGANO UVUNJWE.
Alafu, Zanz hawachangii fedha za kuendesha Muungano huo, wao wanavuna tu mapesa.n Ni mafisadi hawa. Vunja MUUNGANO PLEASE
tuuvunje muungano na tujiandae kuona pemba ikitangazwa kuwa jamhuri huru na ugunja ikienda kuzima uasi wa pemba na wapemba kujaa tanga na mombasa wakikimbia vita na mengineyo mengi yaletwayo na military conflicts. ingawa hivyo tanganyika irudi ili muungano uwe wazi na kila upande ufanye mambo yake na machache ya muungano yaachiwe watendaji wachache kupunguza ukubwa wa serikali.
Wakati hali ya muungano ikiwa tete hebu tuchukulie umeshavunjika alafu mchakato wa kugombea uwakilishi visiwani utakuwaje wale wa kule vs wa jamhuri si patakuwa hapatoshi au watakata tena yaongezeke majimbo ya uwakishi kwa hili naona bora watatue kero za muungano mana ukivunjika wengine wakirudi kule watakosa pa kugombea na kukalia benchi....ni mtazamo tu