Askofu Malasusa na Waraka wa Leo

Askofu Malasusa na Waraka wa Leo

Michango ya Sadaka ikipungua madhara mojawapo ndio kama haya
 
Leo kwenye makanisa yote ya kkkt mashariki na pwani umesomwa waraka ambao ni kama umemsafisha askofu malasusa na wakati huohuo kama halmashauri kuu imekiri kuwa alichofanya malasusa ni kosa, sasa najiuliza kwa nn askofu hakuwaomba radhi tu maaskofu wenzake badala ya kuendelea na misimamo ambayo itazidi kuligawa kanisa, kama amekiri kuwa haikuwa lengo la dayosisi kuzuia waraka ule, why now wanakuwa kama wanawaomba waumini msamaha!?, Hili jambo dayosisi waliangalie kwa umakini,
Askofu Malasusa ni msariti km Yuda, hapaswi kuonewa aibu, ni lzma aombe radhi km yule wa Mtwara, asilete kiburi ndani ya kanisa kwani Kiburi ni dhambi kubwa! Mwenye Akili timamu, alimwona Askofu Malasusa ni msariti pale alipokwenda Airport. Viongozi wa Dini wanapaswa kuwa makini na kujiepusha na mitego ya wanasiasa maana hawa watu wana hira mbaya, viganja vyao vya mikono vimejaa damu za watu wasiyo na hatia! Ninawashangaa viongozi wa Dini wanaojiweka karibu na Utawala huu uliojaa dhambi ya utekaji wa watu na uuwaji wa watu wa Mungu wasiyo na hatia. Ukiona Kiongozi wa Dini anauunga mkono utawala huu basi ni mmoja wao ktk kumwaga Damu ya watu wasiyo na hatia! Kiongozi mwenye Roho ya ki-Mungu hawezi kuchangamana na waovu wa aina hii
 
Chadema inamtumia Dr Shoo kuingiza siasa Kanisani!
Una ushahidi au unajiropokea tu ili uonekane nawe upo? Jifunze kuwaheshimu viongozi wa kiroho kwani wao ndio chaguo la Mungu na sio hao wanasiasa unaowaabudu na kuwatukuza! Isitoshe askofu unayemtuhumu hakuuandika waraka ule akiwa chumbani kwake bali walikubaliana maaskofu wote. Mpe heshima yake na muombe msamaha!
 
Yahani malasusa anaona ni sahihi raia kupotea, kuuliwa, kupigwa risasi hadharani na kundi la makofuli la wasio julikana!!! Askofu kabisa!!!
 
Nilikuwa kanisa la KKKT Usharika wa Kariakoo leo ujumbe hajapokelewa positively....baada ya waraka kusomwa washarika walikuwa kimya tu na Mchungaji akaendelea na mambo mengine
 
tuliopo huku nakapanya mnatunyima uhondo
 
Malasusa kama aliweza kupokea amri toka kwa Makonda hadi akafikia kutamba kuwa "katika Mkoa wangu hakuna cha waraka wala matamko" alikubali kudhalilisha kanisa hivyo asiendelee kuwayumbisha waumini
Ni mambo ya kusikitisha sana
 
Back
Top Bottom