MAPUMA MIYOGA
JF-Expert Member
- Jan 30, 2013
- 3,792
- 2,369
Kwa kweli sasa hivi na-review ulutheri wangu. Makanisani kuna wahuni na wapiga dili tu miaka hii.Sure, Ndio maana wanapokea pesa kama za escrow etc. Kwa sababu wakitoka nje ya madhabahui wanakuwa watu Wa kawaida sio watumishi Wa Mungu. Na hawatakiwi kuonya juu ya maisha ya watu kama dhuluma, mauaji, tabia mbaya kwa sababu ni mambo ya jeshi la Polisi.
Naiangalia KKKT iliokuwa kinara wa kuboresha huduma za jamii, kama shule, vyuo, hospitali nk. Ni miaka mingi inapita makusanyo ya sadaka yapo lakini kanisa limebaki na vyuo, hospitali zile zile miaka yote. Hakuna tena mwendelezo. Kila dayosisi wanajilia vyao hawajui mapungufu na mahitaji ya waamini wao katika kila kona ya nchi hii hivyo wayafanyie kazi, sio kipaumbele tena??