Askofu Malasusa na Waraka wa Leo

Askofu Malasusa na Waraka wa Leo

Leo kwenye makanisa yote ya KKKT mashariki na pwani umesomwa waraka ambao ni kama umemsafisha Askofu Malasusa na wakati huohuo kama halmashauri kuu imekiri kuwa alichofanya Malasusa ni kosa.

Sasa najiuliza kwanini Askofu hakuwaomba radhi tu Maaskofu wenzake badala ya kuendelea na misimamo ambayo itazidi kuligawa kanisa.

Kama amekiri kuwa haikuwa lengo la Dayosisi kuzuia waraka ule, why now wanakuwa kama wanawaomba waumini msamaha?

Hili jambo Dayosisi waliangalie kwa umakini.


Haya majamaa ni highly unstable,ndio maana yanaendeshwa na serikali...

Sidhani likampuni kama RC lipo unstable namna hii!

Bakwata na KkKt ni highly unstable companies!Ndio maana serikali can toy up wit'dem like dummies!
 
Kuna baadhi ya watu bado wanadhani huko makanisani bado kuna waumini wapiga makofi watupu kwa kila jambo watakalo leta!
Kwa hili la kusoma nyaraka za kisiasa kanisani , badala la neno , bado wapiga makofi wapo aisee
 
Wewe mwenye kujua nihabarishe! Yaani wewe unajua kuliko maaskofu wenye waraka wao au ni hiyo njaa ya buku saba inakusukuma? Mwalasusa should step down from that day aliyokataa kuusoma waraka ule na asiing'ang'anie ofisi ya watu! Na kama unampenda utamfuata atakakokwenda!
Astep down kwa lipi? Nyaraka ndizo zilizompa uaskofu? sifa ya kua Askofu sio kusoma nyaraka za ufipa madhabahuni
 
Malasusa anatumika na serikali kufifisha mapambano ya kudai haki na usawa dhidi ya wanyonge wa nchi hii kupitia Kanisa ambalo ndio wajibu wake
Na alaaniwe, sio haya kusema haya kwani amejipambanua kinyume na Kanisa pamoja na watz wanaoumia katika nchi yao wazi wazi.
 
Malasusa anatumika na serikali kufifisha mapambano ya kudai haki na usawa dhidi ya wanyonge wa nchi hii kupitia Kanisa ambalo ndio wajibu wake
Hata kanisa nalo linapambana kwa sababu ya EL
Mambo sio mepesi kama tunavyoyaona kwa nje.

Kuna udini, Ukanda na Ukabila vimeingia katika nchi yetu
 
Malalusa ana kesi ya uzinzi wa kondoo zake, lazima ailambe miguu serikali ili imlinde ktk kashfa hizi.
 
ndie alienunuliwa na chadema kuandika waraka wa kisiasa , na kushinikiza usomwe kanisani , wakati kanisa ni madhabahu ya Mungu.
Waraka hakuandika yeye, waliandika maaskofu 29 wa KKKT Tanzania nzima, akiwemo huyo Malasusa, walisaini huo waraka maaskofu wote akiwepo huyo Malasusa kukubaliana na kilichoandikwa kilichokuwa kimebak ni kuwasilisha kwa waumini kwa njia ya kusomewa ambacho maaskofu watatu akiwemo huyo Malasusa hawakukifanya, lakini pia halmashauri kuu kwa mujibu wa barua yao tuliyosomewa Jana wamekiri na kuomba radhi kwa kuwaumiza waumini na kwamba halikuwa kusudio lao kufanya hivyo na wameomba kudumisha Aman na upendo na utulivu kwa kipindi hiki ambacho wanalishughulikia ili kumaliza hizo tofauti
 
  • Thanks
Reactions: ram
Waraka hakuandika yeye, waliandika maaskofu 29 wa KKKT Tanzania nzima, akiwemo huyo Malasusa, walisaini huo waraka maaskofu wote akiwepo huyo Malasusa kukubaliana na kilichoandikwa kilichokuwa kimebak ni kuwasilisha kwa waumini kwa njia ya kusomewa ambacho maaskofu watatu akiwemo huyo Malasusa hawakukifanya, lakini pia halmashauri kuu kwa mujibu wa barua yao tuliyosomewa Jana wamekiri na kuomba radhi kwa kuwaumiza waumini na kwamba halikuwa kusudio lao kufanya hivyo na wameomba kudumisha Aman na upendo na utulivu kwa kipindi hiki ambacho wanalishughulikia ili kumaliza hizo tofauti
Yesu kristo alikua pekeyake , katika kutetea ukristo , cha muhimu hapo si kuangalia QUANTITY bali kuangalia QUALITY , daudi alimpiga goliath akiwa pekeyake , wakati kukiwa na idadi kubwa ya wanajeshi walioshindwa kumpiga goliath , ndio maana israel mtu wake mmoja anafananishwa na watu mia ambao sio waisrael , malasusa anaweza kuwa pekeyake alieona , si sahihi , na katika uhalisia
akawa sahihi , kamanda shoo analazimisha mambo kwa mahaba yake na chadema , waumini waliowengi wameona mapungufu yake , huo waraka yeye ndio anashinikiza lakini baadhi ya maaskofu walisaini tu lakini wanamjua analazimisha mambo.ukweli utabaki kuwa kweli kanisala kilutheri chini ya kamanda shoo limetawaliwa na mahaba ya makundi fulani na si mahaba ya kristo
 
Sure, Ndio maana wanapokea pesa kama za escrow etc. Kwa sababu wakitoka nje ya madhabahui wanakuwa watu Wa kawaida sio watumishi Wa Mungu. Na hawatakiwi kuonya juu ya maisha ya watu kama dhuluma, mauaji, tabia mbaya kwa sababu ni mambo ya jeshi la Polisi.
Kanisani ni mahali patakatifu , pa kuhubiri neno la Mungu , sio pa maongezi ya watu na matakwa yao binafsi
 
Yesu kristo alikua pekeyake , katika kutetea ukristo , cha muhimu hapo si kuangalia QUANTITY bali kuangalia QUALITY , daudi alimpiga goliath akiwa pekeyake , wakati kukiwa na idadi kubwa ya wanajeshi walioshindwa kumpiga goliath , ndio maana israel mtu wake mmoja anafananishwa na watu mia ambao sio waisrael , malasusa anaweza kuwa pekeyake alieona , si sahihi , na katika uhalisia
akawa sahihi , kamanda shoo analazimisha mambo kwa mahaba yake na chadema , waumini waliowengi wameona mapungufu yake , huo waraka yeye ndio anashinikiza lakini baadhi ya maaskofu walisaini tu lakini wanamjua analazimisha mambo.ukweli utabaki kuwa kweli kanisala kilutheri chini ya kamanda shoo limetawaliwa na mahaba ya makundi fulani na si mahaba ya kristo
wape ukweli
 
nakama shoo aliweza kupokea amri kwa chadema ili kuingiza siasa ktk kkkt
Acha kuropoka, kwani akisemwa muuaji lazima msemaji awe katumwa na Chadema? Au unao ushahidi?
 
Astep down kwa lipi? Nyaraka ndizo zilizompa uaskofu? sifa ya kua Askofu sio kusoma nyaraka za ufipa madhabahuni
Wewe nawe ni dhaifu kuliko huyo dhaifu mwenzako! Alishiriki kila hatua hadi mwisho na kuweka sahihi siyo? Kitu gani kilimfanya asiusimamie kama walivyokubaliana? Nipunguzieni unaaa kidogo maana kujiita askaofu huku ukiwageuka wenzako ni zaidi ya unafiki. Kimemwasha nini sasa kuomba msamaha kwa waumini wa jimbo lake? Au hao wa ufipani unaodai nao wamemkalisha? Tumia makalio kukaa na sio kufikiri!
 
Halmashauri kuu ya Dayosisi inawezaje kutengua maamuzi ya Baraza la Maaskofu? Katiba ya kanisa ina upungufu na hii ni hatari kwa kanisa. Hata hivyo kauli ya bashite inadhihirisha Askofu anatumiwa na sirikali na pia anavujisha siri za kanisa.
 
Back
Top Bottom