Nadhani mwenye majibu ya swali lako ni Gwajima ambaye ameuongopea ulimwengu kuwa Dr Slaa kawatukana Masheikh, Maaskofu, Maimamu na MapadreHivi kumkosoa mtu ni kumtukana?!
Kwani hayo masuala ya umri yanakuhusu nini?Wewe nae unajiita great thinker. Kwanza unaumli miaka mingapi pili wewe umeanza kumjua gwajima lini tatu wewe ni mgumba.
swissme
Sijasoma upuuzi wako ulioandika hapo, ila napenda kukuuliza swali moja, uliona sawa kwa Dr Slaa kutangazia dunia kuwa maaskofu wa Tanzania, kati ya 34, 30 wamepokea rushwa kutoka kwa Lowassa?
Lowassa ana madhambi yake ikiwemo ufisadi, lakini kuhusisha maaskofu na rushwa ni jambo hatari sana. Hivyo binafsi siwezi kujifanya mwendawazimu eti nimtete Dr Slaa kwa majibu anayopewa.
Tena kajikanyaga kweli. Kawaita mpaka walinzi wake ambao walikuwa wanafanya kazi ya kufuatilia maisha binafsi ya Dr SlaaDah!
huyu mchungaji naona kajikanyaga kweli, alikurupuka bila kuhusisha washauri, sasa hadi waumini wake amewaachia viulizo!
Hivi kumkosoa mtu ni kumtukana?!
Nimemsikiliza kwa makini jana Askofu wa Kanisa la Ufufuko na Uzima, Josephat Gwajima akitoa utetezi wake juu ya kile kilichoelezwa na Dr Slaa kuwa ni Ushenga baina ya ndoa ya Lowasa na CHADEMA. Kimsingi amekubaliana na yale yaliyoelezwa na Dr Slaa na kujitetea eti alikuwa anafanya hivyo kama wajibu wake wa msingi kwa wanasiasa. Eti kwamba wanasiasa wengi wanapotaka kugombea wanaenda kwa waganga wa kienyeji hivyo yeye alitaka kumuandaa Lowasa kiroho.
Jambo lililonishtua zaidi ni pale aliposema kuwa kama Dr Slaa ataendelea kuwatukana Maaskofu wa Kanisa Katoliki, Anglikana, Lutherani, TAG, Masheikh na Maimamu nk, hatakaa kimya bali atajitokeza kuwatetea. Kwamba Masheikh na Maaskofu wasijisumbue kumjibu Dr Slaa bali yeye ataifanya kazi hiyo.
Binafsi nimetafakari sana juu ya msimamo huu wa Gwajima. Nimejiuliza, ni wapi Dr Slaa kawatukana Masheikh na Maaskofu? Au kuwaambia kuwa baadhi yao wamepokea hongo toka kwa Lowasa jambo ambalo ni kweli ni matusi? Ni lini Gwajima amekuwa na urafiki na Maaskofu wa Kanisa Katoliki? Ni lini Gwajima amekuwa na Urafiki na Masheikh na Maimamu?
1. Gwajima aliwahi kumtukana Askofu Pengo wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam
2. Gwajima huyo huyo aliwahi kumtukana Askofu Balina wa Kanisa Katoliki jimbo la Shinyanga ambaye kwa sasa ni marehemu.
3. Gwajima pia aliwahi kumtukana Askofu Norbert Mtega wa Kanisa Katoliki, Jimbo kuu la Songea.
4. Gwajima pia aliwahi kuwatukana Masheikh na Maimamu wakati wanadai haki ya Waislam ya kuwa na Mahakama ya Kadhi ndani ya Katiba Mpya.
Kimsingi Mchungaji Gwajima katika hili hana moral authority ya kumnyooshea kidole Dr Slaa ambaye hajatukana. Yeye ndiye alipaswa kujikanya mwenyewe kwa matusi ambayo amekuwa akiporomosha kila siku kwa mahasimu wake kiroho na kisiasa.
Kitendo cha UKAWA kumwachia Gwajima awe msemaji kwa ajili ya kufanikisha ushindi ni vema kikaangaliawa kwa tahadhari. Hii ni kutokana na kujenga taswira isiyo sahihi kwa wapiga kura. Kama inawezekana viongozi wa UKAWA walifanyie kazi jambo hili. Huu ni ushauri wangu tu, kwa sababu sijui majukumu yake Gwajima ndani ya CHADEMA(UKAWA).
Sijasoma upuuzi wako ulioandika hapo, ila napenda kukuuliza swali moja, uliona sawa kwa Dr Slaa kutangazia dunia kuwa maaskofu wa Tanzania, kati ya 34, 30 wamepokea rushwa kutoka kwa Lowassa?
Lowassa ana madhambi yake ikiwemo ufisadi, lakini kuhusisha maaskofu na rushwa ni jambo hatari sana. Hivyo binafsi siwezi kujifanya mwendawazimu eti nimtete Dr Slaa kwa majibu anayopewa.
Viongozi wako wa dini ni malaika!? Mimi sio muumini wa Gwajima ila nilifurahi kitendo chake cha kumkemea PengoNashangaa eti kiongozi wa kiroho wa aina hii nae ana waumini tena wanatoa sadaka kubwa hadi ananunua Hammer na helikopta, kweli wajinga ndio waliwao!
Sijasoma upuuzi wako ulioandika hapo, ila napenda kukuuliza swali moja, uliona sawa kwa Dr Slaa kutangazia dunia kuwa maaskofu wa Tanzania, kati ya 34, 30 wamepokea rushwa kutoka kwa Lowassa?
Lowassa ana madhambi yake ikiwemo ufisadi, lakini kuhusisha maaskofu na rushwa ni jambo hatari sana. Hivyo binafsi siwezi kujifanya mwendawazimu eti nimtete Dr Slaa kwa majibu anayopewa.