Gwajima alipoita waandishi wa habari katika kujibu tuhuma alizotoa Dr Slaa, mategemeo ya watanzani yalikuwa makubwa sana kusikia majadiliano yao yalivyokwenda mpaka Lowasa kuingia CHADEMA. Badala yake Gwajima kapoteza dakika 53 kueleza mambo ya jikoni kati ya Dr Slaa na Mke wake. Kweli kampeni za mwaka huu zimeingiliwa!
Napenda ikumbukwe Dr Slaa alieleza kuwepo kwake katika mchakato wa kumleta Lowasa ndani ya CHADEMA, na akaenda mbali zaidi kueleza wapi alitofautiana na viongozi wengine hatua kwa hatua. Matarajio yangu ni kuwa Gwajima angejibu hatua kwa hatua wapi walitofautiana na wapi walikuwa pamoja. Kumbuka kuwa Gwajima alikiri kuwa aliitwa kama mpatanishi, hii inamaanisha dhahiri kuwa kulikuwa na kuhitilafiana kwa viongozi hao. Kwa bahati mbaya Gwajima hajatamka hata sababu moja ya kuhitilafiana kwao. Badala yake anatupa udaku wa jikoni kwa Dr slaa na mkeo, hii ni hatari sana kwa siasa za Tanzania.
Ni nani kati yenu mlioowa ambao hamna matatizo ya unyumba huko majumbani kwenu? Ni mwl nyerere hakuwa na matatizo na mkeo, au Alhaj Mwinyi, au Mkapa na Kikwete? Sijawauliza ya Mbowe, Bob Makani, Lowasa, Ndesamburo au Lipumba? Jamani tuachane na siasa za udaku.
Kazungumza mengi, toka mashetani mpaka Jikono Lakini si siasa, ni ulaghai mtupu. Eti anasema Enyi, maaskofu Katoliki, protestant, Pentakost na Mashekhe huyu Dr Slaa akiwagusa msimjibu niachieni mimi, wewe ni nani? Acha kila mmoja ajibu kwa nafsi yake usiwajibie watu. Jamani msikubali Gwajima awatawale ni shetani mkubwa huyu.
Azungumzia juu ya usalama kumlinda Dr Slaa. Hii ni haki yake na ni haki ya kila mtanzania anapohisi usalama wake uko hatarini. Mimi namkosoa Gwajima na najua hawezi kunidhuru kwanini nikawaite usalama waje kunilinda? Hata yeye akijisikia kuwa usalama wake uko hatarini aende kwa usalama watamlinda. Hatuna usalama watakao walinda watanzania 40 milioni wasiotishiwa usalama wao.
Nahitimisha kwa kusema huyu Gwajima ni mnafiki, mzandiki, mdini, mpotoshaji, mzabizabina, muongo na anaingia katika maeneo ya siasa ambaye hana uwezo nae. Namashaka hata kama anauwezo wa kuendesha mambo ya kidini. Bali ninauhakika kuwa huyu Gwajima ni baba wa MASHETANI.