GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
Moyo wa Gwajima upo Chadema hata kama kwa kutokupenda. Ni suala la muda tu.
 
Asante comrade Gwajima!

Reforms zifanyike Ili uchaguzi uwe halali na sisi ccm tushinde au kushindwa majimboni kihalali!!

KAZI na utu tunasonga mbele!
 
Lakini si walikataa wenyewe sasa tuwaulize wao wanasemaje hlf tutapata jibu
 
Mbona walishinda uchaguzi mwaka 2020 wakiwa wao tu CCM na Gwajima akiwa mbunge, haya mbona hakuongea? Ila kuna watu humu wanamuona shujaa ndio maaana waliamini kabisa lowasa analeta mabadiliko, ujinga mtupu
 
Mzee wa kugeuza Miskiti kuwa Sunday schools ameibuka tena.
 
Mbona walishinda uchaguzi mwaka 2020 wakiwa wao tu CCM na Gwajima akiwa mbunge, haya mbona hakuongea? Ila kuna watu humu wanamuona shujaa ndio maaana waliamini kabisa lowasa analeta mabadiliko, ujinga mtupu
Yaani huyu na Polepole hawana legacy ya kuongea haya kabisa.
 
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi kama kushinda mtu ashinde kwa Haki na Kama kushindwa basi mtu ashindwe kwa Haki"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
Hayo makovu alileta yeye
 
Back
Top Bottom