GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Mda huuu Gwajima akiwa Live amesema ni rahisi kwa CCM kushinda uchaguzi ila ni ngumu zaidi kuongoza Taifa ambalo lina mpasuko uliotokea kutokana na maumivu ya Uchaguzi.

Akauliza utawezaje kuendelea au kuleta maendeleo kama tokea siku uape unaanza kukutana na upinzani?

Akasema CCM ina wanachama zaidi ya Milion 15+ isiogope iwape Chadema Reforms ambazo wanaona zinawezekana kufanyika kwa wakati huu.

#TUTAKUWEPO🇷🇼🇹🇿

---
Wakuu,

Naona Gwajima kaamua kuunga mkono No Refoms No Election

Mbunge wa Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Josephat Gwajima, amesema ni muhimu chama chake kikafanya marekebisho madogo yatakayowezesha CHADEMA kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Akizungumza na leo kwa njia ya mtandao, Gwajima amesema ushindi wa kweli hauwezi kupatikana bila kuwa na mshindani wa maana. Amesisitiza kuwa kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, chama hicho hakina sababu ya kuogopa ushindani wa kisiasa.

Ameeleza kuwa ni vyema kuangalia hali ya nchi baada ya uchaguzi, akionya kuwa ni hatari kwa wapinzani kupigwa kabla na baada ya uchaguzi, kwani jambo hilo linaathiri maendeleo ya taifa.

Jinga lao! Hivi yeye akiwa mbunge wa mchongo na MNEC akiwa na baba yake mwendazake walishindaje uchaguzi? na walitala vipi? Naye aliyasema haya.
Mdini mkubwa huyu!! Safari hii hatoboi. Ubunge ndio kashaukosa na makanisa ndio kwish nei.
Ana matatizo ya ubongo/akili apelekwe MILEMBE.
 
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi kama kushinda mtu ashinde kwa Haki na Kama kushindwa basi mtu ashindwe kwa Haki"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
Huyu ni mnafiki. Kwa nini hakukataa kugombea pamoja na kwamba kura za maoni Kawe hakushinda na wala kwenye uchaguzi hakumshinda Halima? Huyu kaona hakuna mbeleko tena iliyokuwepo 2020 ndo maana kaamua kujilipua. Kwa sasa hakuna reforms zaidi ya zilizofanyika. Kilichopo mbele yetu ni uchaguzi tu.
 
Back
Top Bottom