GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi"
View attachment 3407981
Kuzuia mikutano ya hadhara wakati Magu ilikuwa sahihi kwako.Askofu mnafiki wewe
 
Magufuli alivuta wengi akawapa vyeo ambao mioyo yao haikuwahi kuipenda CCM na itaendelea hivyo

Mabaya machache ya Magufuli, yanashinda mazuri yaliyo katika uongozi uliopo sasa!

Maana yake, mazuri ya leo ni sawa na mabaya machache yaliyowahi kufanywa na awamu iliyopita

Lucas Mwashambwa unasemaje hapo?
 
Wenye data, gwaji alikuwa anamaoni gani ya NRNE kabla ya bunge kungwa
 
Akiongea na watanzania, Mbunge wa jimbo la Kawe, Josephati Gwajima amesema sio vyema kushinda bila kuwa na mshindani. Hivyo yeye kama mwanachama wa CCM ameshauri CCM ifanye mabadiliko kidogo kisha wawaruhusu CHADEMA kuingia kwenye Uchaguzi.

Amesema kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, suala litakuwa jema kwa kuwa CCM ina wanachama wengi. Askofu Gwajima amesisitiza zifanywe reforms chache zitakazowaruhusu chadema kuingia kwenye uchaguzi kisha waje wawashinde kwenye uchaguzi.

Amesema ushindi inabidi uangalia nchi itakuwaje baada ya uchaguzi. Maana ni vigumu kupigwa kjabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi ambapo italeta ugumu kwenye kuleta maendeleo baada ya uchaguzi.

Suala la No Reforms No Election ni suala la CHADEMA ambao wametishia kutoshiriki uchaguzi ikiwa hakutakuwa na mabadiliko. Askofu Gwajima amesema sio jambo jema kuwa na mgawanyiko baada ya uchaguzi badala yake kuwe na umoja utakao patikana kupitia reforms za kawaida.

Ameongea akiwa na msisitizo wa "Kuwachapa" kwa maana ya kuwashinda wapinzani baada ya kuwapa reforms watakazozihitaji.
Mbunge aliyetokana na kura fake
 
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
amesema kweli.
 
Kwahiyo hapo anaongea kama mbunge, mjumbe wa NEC CCM, Mchungaji au mwananchi huru tu?

Inabidi atambue kuwa kwenye kuongoza nchi huwa haikosekani kupingwa. Hata ukifanya reforms zozote zile usitegemee kila mtu kuunga mkono shughuli za maendeleo.

Gwajima anatakiwa kuwashawishi wana CCM kupitia vikao vya CCM, hasahasa yeye kama mjumbe wa NEC. Kama anaona hawezi kushawishi chama, na kama anaamini kuwa kuna makosa
makubwa yanafanyika, anatakiwa kujitoa CCM.

Anachofanya sasa ni kukihujumu chama. Haitawezekana kuendesha chama iwapo kila mtu ataanza kuongea kupitia press conference.
 
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
Mwamba amezeeka ghafra isee usigombane na system hata siku moja.
 
Mambo ninayo penda kuyasikia hayo 🤣
 
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
nonsense,
kuwapa reforms waropokaji kwani peremende hiyo?šŸ’
 
Mimi naona ameomba reform ili wakikubali tu aende chadema agombee urais huko.
 
Back
Top Bottom