GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

GE2025 Askofu Gwajima: Kutawala Nchi wakati imemeguka kwa makovu ya Uchaguzi ni kazi ngumu sana, tuwape Reforms CHADEMA

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,498
Askofu Gwajima amesema, "Kushinda Uchaguzi ni jambo jepesi lakini kuitawala Nchi na kuiletea Maendeleo iliyomeguka meguka kutokana na Makovu na Majeraha ya Kiuchaguzi ni kazi ngumu sana, sisi kama CCM tunaweza kuamua kuendelea [na Uchaguzi] na tukashinda lakini jaribu kuwaza tangu siku unapo apishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapo maliza Miaka yako Mitano, maendeleo utayaletaje?"

"Nashauri kwamba CCM ina Wanachama zaidi ya Milioni 10, tuamue kuwaruhusu CHADEMA kuwapa reforms zinazowezekana kwa sasa, tungie nao kwenye Uchaguzi kama kushinda mtu ashinde kwa Haki na Kama kushindwa basi mtu ashindwe kwa Haki"

Soma > Askofu Gwajima: Mimi Sihami CCM, tunabanana humu humu mpaka paeleweke
 

Attachments

  • AAA.mp4
    39.3 MB
Wakuu,

Naona Gwajima kaamua kuunga mkono No Refoms No Election

Mbunge wa Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Josephat Gwajima, amesema ni muhimu chama chake kikafanya marekebisho madogo yatakayowezesha CHADEMA kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Akizungumza na leo kwa njia ya mtandao, Gwajima amesema ushindi wa kweli hauwezi kupatikana bila kuwa na mshindani wa maana. Amesisitiza kuwa kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, chama hicho hakina sababu ya kuogopa ushindani wa kisiasa.

Ameeleza kuwa ni vyema kuangalia hali ya nchi baada ya uchaguzi, akionya kuwa ni hatari kwa wapinzani kupigwa kabla na baada ya uchaguzi, kwani jambo hilo linaathiri maendeleo ya taifa.

 
Mda huuu Gwajima akiwa Live amesema ni rahisi kwa CCM kushinda uchaguzi ila ni ngumu zaidi kuongoza Taifa ambalo lina mpasuko uliotokea kutokana na maumivu ya Uchaguzi.

Akauliza utawezaje kuendelea au kuleta maendeleo kama tokea siku uape unaanza kukutana na upinzani?

Akasema CCM ina wanachama zaidi ya Milion 15+ isiogope iwape Chadema Reforms ambazo wanaona zinawezekana kufanyika kwa wakati huu.

#TUTAKUWEPO🇷🇼🇹🇿

---
Wakuu,

Naona Gwajima kaamua kuunga mkono No Refoms No Election

Mbunge wa Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Josephat Gwajima, amesema ni muhimu chama chake kikafanya marekebisho madogo yatakayowezesha CHADEMA kushiriki kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Akizungumza na leo kwa njia ya mtandao, Gwajima amesema ushindi wa kweli hauwezi kupatikana bila kuwa na mshindani wa maana. Amesisitiza kuwa kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, chama hicho hakina sababu ya kuogopa ushindani wa kisiasa.

Ameeleza kuwa ni vyema kuangalia hali ya nchi baada ya uchaguzi, akionya kuwa ni hatari kwa wapinzani kupigwa kabla na baada ya uchaguzi, kwani jambo hilo linaathiri maendeleo ya taifa.

 
Akiongea na watanzania, Mbunge wa jimbo la Kawe, Josephati Gwajima amesema sio vyema kushinda bila kuwa na mshindani. Hivyo yeye kama mwanachama wa CCM ameshauri CCM ifanye mabadiliko kidogo kisha wawaruhusu CHADEMA kuingia kwenye Uchaguzi.

Amesema kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, suala litakuwa jema kwa kuwa CCM ina wanachama wengi. Askofu Gwajima amesisitiza zifanywe reforms chache zitakazowaruhusu chadema kuingia kwenye uchaguzi kisha waje wawashinde kwenye uchaguzi.

Amesema ushindi inabidi uangalia nchi itakuwaje baada ya uchaguzi. Maana ni vigumu kupigwa kjabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi ambapo italeta ugumu kwenye kuleta maendeleo baada ya uchaguzi.

Suala la No Reforms No Election ni suala la CHADEMA ambao wametishia kutoshiriki uchaguzi ikiwa hakutakuwa na mabadiliko. Askofu Gwajima amesema sio jambo jema kuwa na mgawanyiko baada ya uchaguzi badala yake kuwe na umoja utakao patikana kupitia reforms za kawaida.

Ameongea akiwa na msisitizo wa "Kuwachapa" kwa maana ya kuwashinda wapinzani baada ya kuwapa reforms watakazozihitaji.
 
Akiongea na watanzania, Mbunge wa jimbo la Kawe, Josephati Gwajima amesema sio vyema kushinda bila kuwa na mshindani. Hivyo yeye kama mwanachama wa CCM ameshauri CCM ifanye mabadiliko kidogo kisha wawaruhusu CHADEMA kuingia kwenye Uchaguzi.

Amesema kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, suala litakuwa jema kwa kuwa CCM ina wanachama wengi. Askofu Gwajima amesisitiza zifanywe reforms chache zitakazowaruhusu chadema kuingia kwenye uchaguzi kisha waje wawashinde kwenye uchaguzi.

Amesema ushindi inabidi uangalia nchi itakuwaje baada ya uchaguzi. Maana ni vigumu kupigwa kjabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi ambapo italeta ugumu kwenye kuleta maendeleo baada ya uchaguzi.

Suala la No Reforms No Election ni suala la CHADEMA ambao wametishia kutoshiriki uchaguzi ikiwa hakutakuwa na mabadiliko. Askofu Gwajima amesema sio jambo jema kuwa na mgawanyiko baada ya uchaguzi badala yake kuwe na umoja utakao patikana kupitia reforms za kawaida.

Ameongea akiwa na msisitizo wa "Kuwachapa" kwa maana ya kuwashinda wapinzani baada ya kuwapa reforms watakazozihitaji.
The final level of being smart is just pretending you don’t know anything to make your life easier.
 
Akiongea na watanzania, Mbunge wa jimbo la Kawe, Josephati Gwajima amesema sio vyema kushinda bila kuwa na mshindani. Hivyo yeye kama mwanachama wa CCM ameshauri CCM ifanye mabadiliko kidogo kisha wawaruhusu CHADEMA kuingia kwenye Uchaguzi.

Amesema kutokana na wingi wa wanachama wa CCM, suala litakuwa jema kwa kuwa CCM ina wanachama wengi. Askofu Gwajima amesisitiza zifanywe reforms chache zitakazowaruhusu chadema kuingia kwenye uchaguzi kisha waje wawashinde kwenye uchaguzi.

Amesema ushindi inabidi uangalia nchi itakuwaje baada ya uchaguzi. Maana ni vigumu kupigwa kjabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi ambapo italeta ugumu kwenye kuleta maendeleo baada ya uchaguzi.

Suala la No Reforms No Election ni suala la CHADEMA ambao wametishia kutoshiriki uchaguzi ikiwa hakutakuwa na mabadiliko. Askofu Gwajima amesema sio jambo jema kuwa na mgawanyiko baada ya uchaguzi badala yake kuwe na umoja utakao patikana kupitia reforms za kawaida.

Ameongea akiwa na msisitizo wa "Kuwachapa" kwa maana ya kuwashinda wapinzani baada ya kuwapa reforms watakazozihitaji.
Wataacha kuiba kura au biz az yuzho
 
Back
Top Bottom