Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,615
- 40,165
MWONGOZO WA KUHAMA CHAMA
Katika msimu wa Ligi yoyote, huwa kuna wachezaji kuhama club zao. Hata kwenye siasa, dini na hata ndoa, imeanza kuzoeleka watu kuhama au kuachana. Napendekeza Mwongozo wa kuhama:
1. Unapohama, tueleze uzuri wa unakokwenda, si ubaya wa unakotoka. Tayari tunajua utokako ni kubaya ndiyo maana umeondoka.
2. Tueleze uzuri na ubaya wako, si uzuri na ubaya wa watu unaoachana nao. Mapenzi yana upofu wa kudumu. Mwenye neno “MAPINDUZI” katika jina lake, anamshtaki mwenye harufu tu ya jina la “UHAINI”.
3. Jitahidi kukumbuka kuwa unayemwacha aliwahi kuwa mwema kwako (Baby) mpaka mkazaa watoto. Kwa ajili ya watoto, songa mbele kimya kimya.
4. Ukiweza hamia uendako kimya kimya, tutakuona ukiwa huko. Ukitaka kurudi, rudi kimya kimya. Usipoahidi kitu hudaiwi chochote. Maneno mengi yanamtisha mpenzi mpya.
5. KUMBUKA: Hakuna chuki ya kudumu wala mahaba ya kudumu. Mahaba ya kutongozea siyo ya kutunzia ndoa. Unakimbia kikwapa na kuangukia kwenye shombo.
Source fb page yake
Then akaweka picha hizi
Katika msimu wa Ligi yoyote, huwa kuna wachezaji kuhama club zao. Hata kwenye siasa, dini na hata ndoa, imeanza kuzoeleka watu kuhama au kuachana. Napendekeza Mwongozo wa kuhama:
1. Unapohama, tueleze uzuri wa unakokwenda, si ubaya wa unakotoka. Tayari tunajua utokako ni kubaya ndiyo maana umeondoka.
2. Tueleze uzuri na ubaya wako, si uzuri na ubaya wa watu unaoachana nao. Mapenzi yana upofu wa kudumu. Mwenye neno “MAPINDUZI” katika jina lake, anamshtaki mwenye harufu tu ya jina la “UHAINI”.
3. Jitahidi kukumbuka kuwa unayemwacha aliwahi kuwa mwema kwako (Baby) mpaka mkazaa watoto. Kwa ajili ya watoto, songa mbele kimya kimya.
4. Ukiweza hamia uendako kimya kimya, tutakuona ukiwa huko. Ukitaka kurudi, rudi kimya kimya. Usipoahidi kitu hudaiwi chochote. Maneno mengi yanamtisha mpenzi mpya.
5. KUMBUKA: Hakuna chuki ya kudumu wala mahaba ya kudumu. Mahaba ya kutongozea siyo ya kutunzia ndoa. Unakimbia kikwapa na kuangukia kwenye shombo.
Source fb page yake
Then akaweka picha hizi