Askofu Bagonza: Makonda ni tatizo, dalili mbaya au suluhisho?

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Paul Makonda ni zaidi Katibu Mwenezi wa chama Tawala. Tumewahi kuwa nao wengi na wapo wengi wa vyama vingine. Hakuna kama Makonda uzuri na kwa ubaya. Kwa nini?

1. Kama Makonda ni tatizo basi halina suluhisho. Kwa sababu ndani ya chama tawala huyu ndiye ameonekana. Na kama huyu ndiye bora zaidi, waliobaki wana hali gani?

2. Kama Makonda ni dalili ya tatizo basi dalili huwa hazina tiba. Tusubiri ugonjwa wenyewe ndipo tujue tiba. Mgonjwa anayetetemeka kwa homa, kumfunika blanketi zito si kutibu ugonjwa. Ni kusaidia mayai ya vimelea yaanguliwe na mgonjwa atakuwa na hali mbaya zaidi.

3. Kama Makonda ni Suluhisho basi ni lile la “Bomoa yote tutajenga kesho”. Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe. Yeye amekuwa suluhisho zaidi ya dawa ya rangi mbili inayoua vimelea vyote mwilini.

AMESAIDIA SANA:

- Sasa tunajua hali yetu si njema. Hakuna utawala wa sheria wala wa mfumo.

- Sasa tunajua hasara za kukaa gizani. Ukikosa upinzani bungeni na mabarazani, ukakosa uhuru wa habari, ukakosa wana harakati huru, unastawisha CHAWA kila mahali.

- Sasa tunajua wananchi wanaona bora dikteta kuliko demokrasia, yaani bora shibe ya gerezani kuliko njaa ya uraiani.

- Sasa tunajua wenye shida wanataka mtu si taasisi wala mfumo.

- Sasa tunajua kila suluhisho linazaa tatizo. Ukifuga mbwa mkali wa kulinda wezi, kuna siku atakuzuia wewe usiingie nyumbani kwako.

- Sasa tunajua hakuna bunge huru, hakuna mahakama huru, hakuna DPP huru, hakuna AG huru - ila kuna Chama huru.

HEKIMA: Kuna mbwa akiwinda na kukamata mawindo, huwezi kumfukuza eti anaharibu ngozi. Atakula kitoweo chote na mwenye mbwa atakula mchicha siku hiyo.
 
IMG_7492.jpg
 
Paul Makonda ni zaidi Katibu Mwenezi wa chama Tawala. Tumewahi kuwa nao wengi na wapo wengi wa vyama vingine. Hakuna kama Makonda uzuri na kwa ubaya. Kwa nini?

1. Kama Makonda ni tatizo basi halina suluhisho. Kwa sababu ndani ya chama tawala huyu ndiye ameonekana. Na kama huyu ndiye bora zaidi, waliobaki wana hali gani?

2. Kama Makonda ni dalili ya tatizo basi dalili huwa hazina tiba. Tusubiri ugonjwa wenyewe ndipo tujue tiba. Mgonjwa anayetetemeka kwa homa, kumfunika blanketi zito si kutibu ugonjwa. Ni kusaidia mayai ya vimelea yaanguliwe na mgonjwa atakuwa na hali mbaya zaidi.

3. Kama Makonda ni Suluhisho basi ni lile la “Bomoa yote tutajenga kesho”. Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe. Yeye amekuwa suluhisho zaidi ya dawa ya rangi mbili inayoua vimelea vyote mwilini.

AMESAIDIA SANA:

- Sasa tunajua hali yetu si njema. Hakuna utawala wa sheria wala wa mfumo.

- Sasa tunajua hasara za kukaa gizani. Ukikosa upinzani bungeni na mabarazani, ukakosa uhuru wa habari, ukakosa wana harakati huru, unastawisha CHAWA kila mahali.

- Sasa tunajua wananchi wanaona bora dikteta kuliko demokrasia, yaani bora shibe ya gerezani kuliko njaa ya uraiani.

- Sasa tunajua wenye shida wanataka mtu si taasisi wala mfumo.

- Sasa tunajua kila suluhisho linazaa tatizo. Ukifuga mbwa mkali wa kulinda wezi, kuna siku atakuzuia wewe usiingie nyumbani kwako.

- Sasa tunajua hakuna bunge huru, hakuna mahakama huru, hakuna DPP huru, hakuna AG huru - ila kuna Chama huru.

HEKIMA: Kuna mbwa akiwinda na kukamata mawindo, huwezi kumfukuza eti anaharibu ngozi. Atakula kitoweo chote na mwenye mbwa atakula mchicha siku hiyo.
Hehee
 
Kupambana na Makonda ni Sawa ni kutaka kumuua nyoka kwa kucheza na mkia.... wakati huku kichwa kinaendelea kutafuna.... Ni mwendo wa kungata na Kupuliza.... Fumba Fumbua miaka lukuki imepita na hakuna tofauti yoyote....
 
Nimemuelewa askofu Bagonza kuliko wakati mwingine wowote

Wananchi hawataki porojo za siasa wanataka matatizo yao yafanyiwe kazi papo hapo

Wakati wengine wakifanya siasa na maisha ya watu Makonda anatatua migogoro na shida za watu moja kwa moja

Sasa Watanzania wanakaribia kwenye nchi ya ahadi kwa jeshi la mtu mmoja
Hakuna chama kikundi wala mfumo
Hapa makonda tuu
 
Paul Makonda ni zaidi Katibu Mwenezi wa chama Tawala. Tumewahi kuwa nao wengi na wapo wengi wa vyama vingine. Hakuna kama Makonda uzuri na kwa ubaya. Kwa nini?

1. Kama Makonda ni tatizo basi halina suluhisho. Kwa sababu ndani ya chama tawala huyu ndiye ameonekana. Na kama huyu ndiye bora zaidi, waliobaki wana hali gani?

2. Kama Makonda ni dalili ya tatizo basi dalili huwa hazina tiba. Tusubiri ugonjwa wenyewe ndipo tujue tiba. Mgonjwa anayetetemeka kwa homa, kumfunika blanketi zito si kutibu ugonjwa. Ni kusaidia mayai ya vimelea yaanguliwe na mgonjwa atakuwa na hali mbaya zaidi.

3. Kama Makonda ni Suluhisho basi ni lile la “Bomoa yote tutajenga kesho”. Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe. Yeye amekuwa suluhisho zaidi ya dawa ya rangi mbili inayoua vimelea vyote mwilini.

AMESAIDIA SANA:

- Sasa tunajua hali yetu si njema. Hakuna utawala wa sheria wala wa mfumo.

- Sasa tunajua hasara za kukaa gizani. Ukikosa upinzani bungeni na mabarazani, ukakosa uhuru wa habari, ukakosa wana harakati huru, unastawisha CHAWA kila mahali.

- Sasa tunajua wananchi wanaona bora dikteta kuliko demokrasia, yaani bora shibe ya gerezani kuliko njaa ya uraiani.

- Sasa tunajua wenye shida wanataka mtu si taasisi wala mfumo.

- Sasa tunajua kila suluhisho linazaa tatizo. Ukifuga mbwa mkali wa kulinda wezi, kuna siku atakuzuia wewe usiingie nyumbani kwako.

- Sasa tunajua hakuna bunge huru, hakuna mahakama huru, hakuna DPP huru, hakuna AG huru - ila kuna Chama huru.

HEKIMA: Kuna mbwa akiwinda na kukamata mawindo, huwezi kumfukuza eti anaharibu ngozi. Atakula kitoweo chote na mwenye mbwa atakula mchicha siku hiyo.
Mkuu naona kichwa Cha makala kinataka kutofautiana na content.

Yaliyotiririkwa kwenye mainbody ni madini matupu, ila hiko kichwa Cha habari, hapana bhana.

Yeye Bishop Bagonza katika maudhui ya makala hii angelieleza moja kwa moja ubaya wa Makonda katika kuanika uozo wa Sirikali ya chama chake.

Ama amsifie kwa namna anavyochukua hatua hizo, ili naye mtoa mada tumpine kasimama upande upi.

Sisi tunamuona Makonda kama kafanya mema kututoa tongo tongo za hila tulizokuwa tukipakwa usoni na watendaji wa Serikali wakijisifu kuwajibika ipasavyo pamoja na kumsifia Rais kutwa kuchwa kwa namna ya kumwabudu iliyopitiliza.

Mawaziri na wateule wengine wote kugeuzwa mafurushi ya chawa kama watu waliojitoa ufahamu!

Hitimisho langu katika comment hii ni kwamba, Makonda tumuwekee alama ya 'mwenzetu' kwa namna alivyoweza kubainisha yote hayo yaliyomuwezesha Bagonza naye kuyachambua.
 
Nimemuelewa askofu Bagonza kuliko wakati mwingine wowote

Wananchi hawataki porojo za siasa wanataka matatizo yao yafanyiwe kazi papo hapo

Wakati wengine wakifanya siasa na maisha ya watu Makonda anatatua migogoro na shida za watu moja kwa moja

Sasa Watanzania wanakaribia kwenye nchi ya ahadi kwa jeshi la mtu mmoja
Hakuna chama kikundi wala mfumo
Hapa makonda tuu
Una Uhakika watu wametatuliwa shida zao?.Mimi nadhani alichokifanya Comred Paul Makonda ni kuwapa nafasi watu watapike nyongo zao yaani waseme ya moyoni lakini kutatuliwa shida zao sidhani,ukitaka kujua hilo ngoja arudi tena mwakani akafanye Ziara km hiyo utasikia watu wakitoa malalamiko yale ktk namna ile ile,Muda ni Mwalimu Mzuri.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom