Tatizo la uhaba wa sukari kujirudia kila mara na kuyumbisha bei sokoni, nini suluhisho la kudumula kutatua tatizo hili?

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
380
763
Jana kulikuwa na malumbano ya hoja ikihusu TATIZO LA UHABA WA SUKARI KUJIRUDIA KILA MARA NA KUYUMBISHA BEI SOKONI, NINI SULUHISHO LA KUDUMULA KUTATUA TATIZO HILI? Waalikwa walikuwa kutoka Bodi ya sukari, kutoka Wizara ya Kilimo na wote waliingia mitini.

Yaliyozungumzwa pale yanatisha. Kumbe wanaotawala uagizaji wa sukari ni wafanyabiashara wachache na wanaamua na kupanga bei ya sukari. Kuna maeneo katika nchi hii bei ya sukari imefika mpaka Tshs.6,000 kwa kilo na Watawala wapo na hakuna kinachofanyika.

Juzi juzi waliweka bei elekezi hakuna mfanyabiashara anayefuata bei elekezi na Wananchi wamebaki kama hawana mtetezi. Nchi hii wananchi wana shida. Ziara ya Makonda imeibua mengi. Wengi wapepotelewa na wapendwa wao.

Wengine mpaka sasa wana miaka 3 hawajapatikana, Kesi za ardhi ni lukuki, wafanyabiashara wanaonewa katika ukadiriaji wa kodi zao mfano wa Igunga. Watawala wapo hakuna wanachofanya.

Tuliahidiwa treni ya mwendo kasi kwenda Morogoro ingeanza safari Januari, 2024 lakini mpaka sasa ni kimya. Watawala wapo hakuna kinachofanyika.

Jana walishauri kuwa Mhe. Rais avunje Baraza lake la Mawaziri na kuwateua wanawake wote inaonekana wanaume hawamsaidii.

Matatizo yote yanaelekezwa kwa Mhe. Rais yeye ndo Baba na Mama yetu inampasa achukue hatua za haraka.
 
Jana kulikuwa na malumbano ya hoja ikihusu TATIZO LA UHABA WA SUKARI KUJIRUDIA KILA MARA NA KUYUMBISHA BEI SOKONI, NINI SULUHISHO LA KUDUMULA KUTATUA TATIZO HILI? Waalikwa walikuwa kutoka Bodi ya sukari, kutoka Wizara ya Kilimo na wote waliingia mitini. Yaliyozungumzwa pale yanatisha. Kumbe wanaotawala uagizaji wa sukari ni wafanyabiashara wachache na wanaamua na kupanga bei ya sukari. Kuna maeneo katika nchi hii bei ya sukari imefika mpaka Tshs.6,000 kwa kilo na Watawala wapo na hakuna kinachofanyika. Juzi juzi waliweka bei elekezi hakuna mfanyabiashara anayefuata bei elekezi na Wananchi wamebaki kama hawana mtetezi. Nchi hii wananchi wana shida. Ziara ya Makonda imeibua mengi. Wengi wapepotelewa na wapendwa wao. Wengine mpaka sasa wana miaka 3 hawajapatikana, Kesi za ardhi ni lukuki, wafanyabiashara wanaonewa katika ukadiriaji wa kodi zao mfano wa Igunga. Watawala wapo hakuna wanachofanya. Tuliahidiwa treni ya mwendo kasi kwenda Morogoro ingeanza safari Januari, 2024 lakini mpaka sasa ni kimya. Watawala wapo hakuna kinachofanyika. Jana walishauri kuwa Mhe. Rais avunje Baraza lake la Mawaziri na kuwateua wanawake wote inaonekana wanaume hawamsaidii. Matatizo yote yanaelekezwa kwa Mhe. Rais yeye ndo Baba na Mama yetu inampasa achukue hatua za haraka.
Sukari kilo elfu 6
Mchele sasa kilo 3700
Maharage kilo 3700
Dagaa 8000
Unga 1800
Daladala badala ya kupandisha 100 kwa ruti wao wamejiamulia kupandisha 200. Mfano mbezi makumbusho ilikuwa 600 sasa ni 800..
Nyama kutoka 6000 hadi 9000 sasa.
Kingamuzi kutoka 21000 hadi 23000 ma kuendelea.
Ada za mashule zimepanda.
Shule za umma now bila mtoto kwenda na elfu 2000 haiwezekani.

Kila kitu kimepanda huku hali za mishahara sekta binafsi zikibaki vilevile na serikalini kiduchu kimeongezwa..

Cha kushangaza hakuna anayeshtuka sio serikali wala wapinzani wala wanaojiita watetezi wa haki za binadamu..
Wananchi wanaumia sana.malalamiko ni mengi sana mtaani.
sasa hapo tutasema tuna viongozi waliopo kwa ajili ya wananchi kweli.??
 
Kipindi cha jana kinatakiwa kirudiwe au kiwekwe kwenye youtube. Watanzania wote wanatakiwa kuungana kumuondoa mkoloni mweusi CCM.
 
Back
Top Bottom