kwa wale wote waliosoma seminari za nyegezi, makoko ,sengerema na pia shule zilizo chini ya jimbo kuu la mwanza kama bukumbi, st joseph girls seminary na sumve naamini mtamkumbuka vema baba askofu anthonius mayalla alipenda sana elimu na aliwekeza muda wake mwingi katika suala hili na zaidi ya yote aliwapenda mapadre wake sana na kuwalea vizuri hivyo kupunguza migogoro ya mapadre na askofu wao ukilinganisha na majimbo mengine kweli tutamkosa sana, natoa pole kwa wafuatao pia,FR R.NKWANDE, FR.KUBEJA, FR.NINDILO WALEI WOTE, WASEMINARISTI WOTE, NA WAAMINI WOTE.MUNGU AMLAZE BABA MAYALA MAHALI PEMA PEPONI AMINA.
R.I.P Askofu Mkuu Anthony Mayalla! Mungu aliyekupa karama na aliyekuteua kuchunga kondoo wake wa Jimbo Kuu la Mwanza na kabla ya hapo Jimbo la Musoma, yeye mwenyewe akupokee katika makao yake ya milele. Binafsi nakukumbuka sana kwani nimetumikia chini yako na ni wewe uliyenipa sakramenti ya Kipaimara!
Ninamkumbuka ArchBishop Mayala kwa suala moja tu. Kuwadharau mapadre wazawa wa Jimbo la Musoma. Hadi leo hakuna Padre MZALIWA wa Jimbo la Musoma amekuwa ASKOFU. Kwa nini?
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na kuwapa nguvu na faraja ndugu, jamaa, marafiki na waumini wote katika kipindi hiki kigumu kwao~AMEN
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.