Askari watwangana hadharani

Askari watwangana hadharani

Hili ni la kuchekesha we unasikitikaje?

Matukio kama haya ndio yanafanya mtaa uchangamke....mie huwa nikikuta hivi njiani nasimama hadi mwisho wa show
Hata mimi nitasimama maana itakuwa ni kitendo cha kustajaabisha, sana!
 
LEO NIMEENDELEA KUJIFUNZA, JWTZ WANACHUKIWA SANA NA RAIA, WACHUKUE NAFASI HII WAJIOSHE MBELE YA MACHO YA RAIA
 
Ngumi napenda sana sanaaaa, hasa kupiga ngumi kali na za haraka paap alafu unakwepa una move step back una dance unapiga kali kaliii nzito na kukwepa, ngumi mchezo mzuri sana na unaleta heshima sana.. Ujue kukwepa kuliko cobra alafu ujue kupiga haraka kama paka, utagonga watu hata 5 na watakimbia wote
The great Mohamed Ali anakwambia dance like a butterfly sting like a bee
 
Waulize FFU wanawajua vzr pale Ukonga huwa wanakula mkong'oto kinoma na hao KM
 

Attachments

  • Screenshot_20190520-084811_1.png
    Screenshot_20190520-084811_1.png
    132.4 KB · Views: 34
  • Screenshot_20190520-084931_1.png
    Screenshot_20190520-084931_1.png
    116.7 KB · Views: 38
Fikra potofu hizo ukomandoo Ni mafunzo maalum ya kupambana na kujihami na maadui, kuvuka vikwazo mbalimbali na si vyeo, komando huwezi mjua kwa sura au tabia Bali Hadi utokee mtiti ndipo utaweza note kitu tupo nao kitaa na Ni watu very humble
Komando hakai kitaa kizembe
 
Wache wapigane hata wapasuane pumbu zao,sisi tuwasaidie nini?
Kabisa..
maana hao mabaka wanavyoonea raia huku mitasni ..wakipatikana ..watu wanafurahi sana!
Wana tabia za kulazimisha kuwa wapo juu ya kila kitu!
 
Huku kwetu juzi kati...walikitwa baa wamelewa halafu wameanzisha ugomvi...mabaka hao!
Raia wakawafumua mbaya halafu wakaita polisi ...
nao wakavunja hadi mabega ...
Siku ya pili wanajeshi wakaenda polisi kutoa onyo ..eti watu wao wamepigwa so watafanya doria wao..badala ya polisi!
Wakajibiwa acheni sifa na ujinga kwanza@
 
Hao ni (KM) ni sawa na (FFU) au (MP).
Alafu kuwa mwanajeshi au askari wa jeshi lolote haimaanishi ndio unajua kupigana.

Kupigana ni uwezo wa mtu binafsi.
Unaonaje one day tuwaombe 'komite' jamaa wa Mlalakuwa. Mi najimudu kidogo kwenye mambo ya uraa dash balai na taisabaka 😜😜
 
Wewe ni raia huna mafunzo ya kijeshi kuwa mpole
Hakuna jipya..wapo wanayajua kuliko hao mabaka..sema mikakati tu kuwa haitakiwi waonekane sawa!
Maana mabaka yatakuwa hayana thamani..yatadharaulika hasa ukijumlisha na zile tabia za kikuda za wengi wao!
Wakitoka..kuleee..wanajiona kama wao ni zaid ya hata raisi.
Kumbe ni walinzi wetu tu!
 
Kwani wanajeshi sio wztu?
Ina maana hawazidiwi?
Nyie ndio mnaopandwa michwani.na kuchukuliwa mpaka wake zetu...mmeaminishwa mwanajeshi kaumbwa kwa chuma?
Anatoka hukuhuku uraiani..tena wengine wanaingizwa kidugu..
Wapo mpaka mashoga ..tena kibao.
 
Magereza wanapambana na wafungwa sugu wauaji wabakaji makatili sembuse
Mmezidisha chumvi kuwasifia hawa jamaa. Hao watu hatari, sugu wanafikaje huko gerezani? Kumbuka mtu mpaka kufikia kufungwa ni hatua zipi zinakuwa zimepitiwa hapo katikati.

Katika mkondo wa sheria gereza ni chombo cha mwisho kumshughulikia mkosaji.Wapo waliomkamata, amekaa sero za polisi, amepelekwa mahakamani amerudishwa mahakamani mpaka anahukumiwa huyo mtu anakuwa si tishio tena.

Ukiangalia mifumo ya kule gerezani haimfanyi mtu kufanya lolote na akafanikiwa, labda atoke nje ya gereza. Kiujumla mtu aliyeko gerezani kama mifumo ya kule ikifuatwa haimfanyi mfungwa/mahabusu kuwa tishio kwa askari magerezaukilinganisha na anapokuwa nje ya gereza.
 
Magereza mara nyingi wanatoewa jkt,halafu hakuna wanaojiheshimu kama magereza anajua tu utamkuta magerezani hangaiki na raia wa mtaani kama polis
 
Back
Top Bottom