Asilimia 75 ya Wanawake wanaofanya Uchunguzi wa Saratani Ocean Road wanakutwa na Ugonjwa

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,120
Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kinga wa Taasisi ya ORCI, Dkt. Crisprin Kahesa ambaye amesema, Watanzania wengi wanaogopa na hawapo tayari kupokea majibu ya vipimo vya Saratani jambo ambalo ni hatari
-
Amesema Wanawake wanaofika katika Taasisi hiyo hufanya uchunguzi wa Saratani ya Matiti na mlango wa Kizazi ambapo wengi wao wanakutwa tayari wana Ugonjwa uliofika katika hatua za mwisho
-
Kufuatia hali hiyo, ORCI imetangaza kutoa huduma za uchunguzi wa Saratani bure katika Maonesho ya Kimataifa ya 47 ya Biashara ya Dar es Salaam (DITF) pamoja na Elimu kuhusu Dalili, Matibabu na jinsi ya kuepuka Saratani
-
#JamiiForums #JFAfya #PublicHealth #JFHuduma #JFUwajibikaji
 
Back
Top Bottom