Asilimia 40 ya bidhaa nchini ni feki

You are entitled to your opinion, kama mtu fake ni fake tu msitake kumsafisha wakati hana usafi wowote.

yeah and its not a must to agree with it.what is fake btw?do we have anything fake in the world of our ordinary experience or even outside of it?
 
Hata kwenye wale samaki ambao aliingizia Serikali hasara ya shilingi 1.2 billioni kama gharama za kuwahifadhi pia alikuwa na plan nzuri tu!


Kesi si bado iko mahakamani?Ulitaka agawe kidhibiti mapemaaaa?
 
Mtarajiwa,

..kwanini unafikiri ni wazo baya kumshauri Magufuli arudishe nyumba aliyojitwalia?
 
Kesi si bado iko mahakamani?Ulitaka agawe kidhibiti mapemaaaa?

Kidhibiti kinaweza hata kupigwa picha na kutumika mahakamani badala ya kuliingizia Taifa hasara ya shilingi 1.2 billioni. Kwani ilivyoamuliwa kuwagawa samaki wale ina maana kesi imekwisha? Maamuzi yake shakalabaghala, kama kiongozi hafai kabisa.
 
Mtarajiwa,

..kwanini unafikiri ni wazo baya kumshauri Magufuli arudishe nyumba aliyojitwalia?



Sifikiri ni wazo baya isipokuwa mara nyingi unapozungumzia utendaji mzuri wa Magufuli hoja ya ma critic wake siku zote ni nyumba nyumba nyumba....hawana nyimbo zaidi ya hii!
Sasa mimi nataka kuwaambia kwamba Magufuli hakuamka tu asubuhi na kuamua nyumba za serikali ziuzwe isipokuwa yalikuwa ni makubaliano na mawaziri wenzake na Mkuu wa nchi na isitoshe alikuwa na mpango endelevu wa ujenzi wa nyumba mpya za serikali akianzia Dodoma makao makuu.
Na hata kama alipotoka kwenye nyumba kama wanavyodai vipi hawaoni vision ya Magufuli na ujasiri mwingine katika maamuzi yake yenye maslahi kwa taifa?Washasahau kuwa ni yeye ndiye alimshauri Mkapa watenge kidogo pato la ndani liende kwenye barabara?Washasahau alivyoirekebisha Tanroads iliyokuwa na wakurugenzi wanaojilipa 10M kwa mwezi?washasahau barabara zote alizozisimamisha?Washasahau magari ya serikali yaliyokuwa na namba binafsi huku yakitumika kubeba nyasi,kupeleka vimada saloon ...washasahau..the list goes on and on..
Sasa mseme basi nani kama Magufuli katika CCM ya sasa?
 
Mtarajiwa,

..hivi kujitwalia zile nyumba unaita mpango endelevu?

..vipi kuhusu ubabe wake kule Mwanza kuvunja kile kituo cha mafuta ambapo mahakama imeamuru serikali ilipe shilingi bil 14.7?

..you know, I like Magufuli lakini mara nyingine naona kama vile huwa anaamka vibaya.

..kuhusu suala la nyumba, naona Magufuli anapaswa kuonyesha mfano na kurudisha nyumba aliyojitwalia. unajua kuna wanasiasa wachache ambao hufanya uamuzi mbovu lakini wakapata nafasi ya kujirekebisha.

..Magufuli anayo nafasi ya kujirekebisha ktk wizi na hujuma alioshiriki.
 
WATANZANIA wamekuwa wakilishwa samaki kutoka nje ya nchi wasio na viwango, imefahamika.

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. John Magufuli, alisema hayo jana baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika viwanda vitatu vinavyotengeneza nyavu za uvuvi jijini Dar es Salaam.

Sambamba na kuingizwa nchini kwa samaki hao pia Waziri aligundua kuwapo kwa viwanda zaidi ya 30 ‘feki’ jijini vinavyodaiwa kuzalisha nyavu hizo kwa ajili ya kuvulia samaki huku vilivyosajiliwa rasmi ni viwili peke yake.

Alimtaka mmiliki wa kiwanda cha Imara Fishnets kuteketeza shehena nzima ya nyavu zilizomo kiwandani hapo kwa maelezo kuwa ni haramu na hazikidhi viwango vya sheria ya uvuvi nchini.

Hali kadhalika alitoa siku moja kwa viwanda hivyo feki vya kuzalishia nyavu, kuhakikisha vinachoma bidhaa hizo na kuacha mara moja biashara hiyo.

Dk. Magufuli alipata taarifa za viwanda hivyo jana baada ya kufanya ziara ya ghafla katika viwanda vya Imara, Alpha na Asmara ambavyo hujishugulisha na biashara ya bidhaa za uvuvi na pamoja na mambo mengine alijionea uzalishaji wa nyavu haramu na kuingizwa kwa samaki wasiokuwa na viwango vya afya kutoka nchi za nje na kuuzwa nchini kwa matumizi ya binadamu.

Akiwa katika kiwanda cha Imara, aliambiwa kinazalisha tani 16,000 za nyavu hizo kwa mwezi na kuuzwa Malawi, Kongo, Zambia na nchini kwa ajili ya uvuvi haramu, huku zikiwapo zingine kutoka China na India.

“Nyavu haramu ni marufuku, lazima wenye viwanda wazingatie sheria, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Jeshi la Polisi tusaidieni kuwachukulia hatua, la sivyo nchi itakuwa shimo la taka, maofisa wavuvi katika ofisi za manispaa jitahidini kufanya ukaguzi katika maduka ili kudhibiti hali hiyo,” alisema Dk. Magufuli.

Aliongeza kuwa katika kiwanda hicho huzalisha nyavu za milimeta nane, inchi moja na nusu, inchi moja na robo tatu, inchi nne pamoja na sentimeta nane wakati kwa sheria za uvuvi, nyavu inatakiwa kuanza na inchi sita.

Hata hivyo, mmiliki huyo Shenaz Halari, alisema huuza nyavu hizo katika duka lake lililopo mtaa wa Indira Gandhi jijini.

Alisema amekuwa akifanya biashara na nchi jirani na kwamba anaiomba Serikali itoe ufafanuzi zaidi kuhusu ubora wa nyavu na wapate mwongozo wa zinazoruhusiwa.

“Sisi tumekuwa tukifanya biashara, kama Serikali itatwambia kwamba tusifanye tena, sawa, lakini hatuko wenyewe wapo wengine zaidi ya 30 ambao nao huuza bidhaa haramu vilevile,” alisema Shenaz.

Katika kiwanda cha Alpha alishangazwa na wamiliki wa kiwanda hicho kuagiza tani zaidi ya 2,200 za samaki kwa mwaka kutoka Yemen, Japan na India zinazodaiwa kutokidhi viwango vya afya na kuuzwa kwa matumizi nchini.

Waziri aliambiwa pia na wamiliki hao kuwa hata katika nchi hizo samaki hao hawatumiwi na binadamu kama chakula.

Katika hatua nyingine, alikitaka kiwanda hicho kuhakikisha kuwa kinatazama upya maslahi ya wafanyakazi ambapo ilidaiwa kuwa kila mmoja hulipwa Sh. 3,100 kwa siku, huku kiwanda kikiwa na wafanyakazi zaidi ya 120.

Ofisa Ugavi wa Kiwanda hicho, Joshua Meshack, alisema kiwanda hicho hulazimika kuagiza samaki nje ya nchi kutokana na soko la samaki wa nchini kuwa dogo.
 
DK magufuli leo aliamua kuitokea kampuni moja inayofanykazi ya kuhifadhi samaki;pale alipokuta vibua vinaagizwa toka yemen na japa ambavyo hutumika kwao kama chambo ya kuwapata"TUNA"
Baada ya kullamika kwa nini wanawalisha chambo watanzania samaki walioshindikana huko kwao walikiri na kuomba samahani na kuahidi tani 2250 waliyoagiza aitakuja tena,...
wakti huo huo alifumania kampuni moja inayofanya kazi ya kutengeneza nyavu haramu;hilo nalo amewaaapia ata deal nao sambamba;

kazi unayo baba;mwaka wako

Mungu yuko nyuma yako

Mimi mbona hii siielewi. Hiyo kampuni ya kuhifadhi samaki inaletaje samaki wa kuwauzia watanzania) Na hivi tatizo la hao samaki ni kuwa wanatumika kama chambo na si kingine? Sasa walitegemea Tuna wale nini kama sio samaki wenzao? Mbona tunakula mahindi ambayo hayo hayo kwa wenzetu wanlisha ng'ombe? Mbona sisi hatuli chura lakini kwa wenzetu ni chakula cjha hali ya juu? Kama samaki wanalika (hawajaharibika au kuwa na sumu), bei yao inakubalika heri watanzania wawale kuliko ma-panki!

Kwelnye hilo la nyavu si kuna idara inahusika? Kwa nini asiwaachie wafanye kazi yao badala ya kutoa vitisho?

Hapa ni kutafuta umaarufu na si kingine.

Amandla......
 
Magufuli aliteuliwa kama waziri wa Vitoweo ...kwa mujibu wa JK wakati anamteua.

Sasa kama amelaza da,mu mpka vibua vikawa vinaagizwa matani kwa maelifu ,na kwa waliosikiliza TV yule mama wa kihindi alisema kuwa anawafahamu wafanyabiashara zaidi ya 30 wanaoagiza pia sasa hapa alikuwa wapi?

Tuache kuwasifia wati kijinga.
 
Siye Wadanganyika tunachekesha sana. Huyu bwana alihusika kwa karibu sana na maamuzi ya uuzwaji nyumba ambayo yameliingizia Taifa hasara kubwa sana kwa kuwalipia Wafanyakazi mabilioni ya shilingi kwa gharama za kuishi mahotelini. Miezi michache iliyopita kaliingizia tena Taifa hasara ya shilingi bilioni 1.2 kwa gharama za kuhifadhi samaki, lakini pamoja na maamuzi haya mabovu ambayo yameligharimu Taifa pesa chungu nzima bado kuna wadanganyika wanamuona huyu bwana anastahili sana kuwa "Kiongozi" wa nchi yetu kitu ambacho kinanistaajabisha sana. Hivi mtu afanye nini mpaka tuweze kusema huyu kama kiongozi hatufai kutokana na mambo kadhaa wa kadha? Naona kuna watetezi wa Magufuli wamemwaga hapa kwa fujo ili kumpigia debe magufuli.
 
DK magufuli leo aliamua kuitokea kampuni moja inayofanykazi ya kuhifadhi samaki;pale alipokuta vibua vinaagizwa toka yemen na japa ambavyo hutumika kwao kama chambo ya kuwapata"TUNA"
Baada ya kullamika kwa nini wanawalisha chambo watanzania samaki walioshindikana huko kwao walikiri na kuomba samahani na kuahidi tani 2250 waliyoagiza aitakuja tena,...
wakti huo huo alifumania kampuni moja inayofanya kazi ya kutengeneza nyavu haramu;hilo nalo amewaaapia ata deal nao sambamba;

kazi unayo baba;mwaka wako

Mungu yuko nyuma yako

Kwa hili nampongeza Magufuli ingawa hatua zimechelewa kuchukulia. Nadhani watu wengi wa Dar watakuwa wanalifahamu hili tatizo la vibua. watu walikuwa wanapata madhara walipokuwa wakila hawa samaki. Watu wengi walijua ni vibua toka hapa kwetu waliozoeleka. lakini watu walikuwa wanchubuka ngozi baada ya kula hawa samaki. Watu walikuwa wakisema ni vibua toka Msumbiji nk.
 
Kwa hili nampongeza Magufuli ingawa hatua zimechelewa kuchukulia. Nadhani watu wengi wa Dar watakuwa wanalifahamu hili tatizo la vibua. watu walikuwa wanapata madhara walipokuwa wakila hawa samaki. Watu wengi walijua ni vibua toka hapa kwetu waliozoeleka. lakini watu walikuwa wanchubuka ngozi baada ya kula hawa samaki. Watu walikuwa wakisema ni vibua toka Msumbiji nk.

Kama hao vibua walikuwa wanahatarisha afya za walaji kwa nini wauzaji hawakufunguliwa mashtaka? Mnaamini kweli watakubali kuingi hasara ya kuharibu samaki waliowaagiza kutokana na kauli tu ya waziri? Mimi ningemwelewa kama angeagiza kimya kimya mamlaka husika zichunguze ubora wa hao samaki ili kama ni wabovu basi wahusika wapelekwe mbele ya sheria na tamko rasmi litolewe kupiga marufuku uagizaji na uuzaji wa samaki wa aina hiyo! Sio hizi propaganda.

Amandla......
 
Kwa hiyo Mkuu wake hata kama anaboronga na nchi inaenda mrama, yeye anaangalia pembeni tu bora liende! basi turidhike tu na kumpigia makofi kwamba ni kiongozi bora! Kiongozi bora huwa hakai kimya kama anaona nchi inaenda mrama lazima atatoa sauti yake ili kuinusuru nchi, kukaa kwake kimya ni kuonyesha kuridhika na utendaji wa boss wake ambao unalalamikiwa kila siku na Watanzania walio wengi.




Yaani wewe hapo unachoongea hukifahamu, kama ungekuwa unafahamu maana ya uongozi bora na ufuatialiji,
Jiulize kwani muheshimiwa Kikwete kafanya aliyo ahidi?
je ni kiongozi gani anayetekeleza kwa vitendo unaemfahamu taja jina lake hapa zaidi ya Magufuli,
Je wewe Bosi wako akikuamuru ufanye kitu utakataa? na ukikataa then kazi huna fikiri kabla ya kuseba
angalia sehemu mbili tofauti

Katika viongozi bora Dr magufuli ni boraa kuliko wote kwani jambo lililo ndani ya uwezo wake anatekeleza vilivyo.
 
Kama hao vibua walikuwa wanahatarisha afya za walaji kwa nini wauzaji hawakufunguliwa mashtaka? Mnaamini kweli watakubali kuingi hasara ya kuharibu samaki waliowaagiza kutokana na kauli tu ya waziri? Mimi ningemwelewa kama angeagiza kimya kimya mamlaka husika zichunguze ubora wa hao samaki ili kama ni wabovu basi wahusika wapelekwe mbele ya sheria na tamko rasmi litolewe kupiga marufuku uagizaji na uuzaji wa samaki wa aina hiyo! Sio hizi propaganda.

Amandla......

Fundi Mchundo!
Let us agree to disagree as usual. You seem to become matured now. Kama Pombe Magufuli is not creeping cheap politics anatakiwa atumie team work na members wa Baraza la Mawaziri kwani maswala haya yana dimension pana. To be realistic kuna haja ya kuangalia upya sera tuliyokumbatia ya soko huria kichwa kichwa kuanzia enzi za Ruksa kupitia kwa jambazi Mkapa na leo tunaye fisadi Kikwete.
Hivi kwa nini tusirudie zile enzi za kutumia import licence na mipesa kupitishiwa Benki badala ya huu utamaduni wa kubeba cash kufanya transaction zetu. If we go back into the old good days unaomba leseni ya kuagiza vibua inabidi ipitishwe kwenye Wizara ya Vibua of course hutapewa leseni and therefore hapa hutamlaumu TRA wa TFDA wala TBS kwani hapa hakingii hata kiberiti au pipi but because mmekuwa vipofu vibua wapo kwenye ghala Vingunguti halafu Pombe anamnukulia Mama anayeagiza nyavu sheria ambayo she is not even interested kusikiliza. Kwa hapo we need to go back kwenye REGULATATED ECONOMY/MARKETS kwa taarifa yenu those wise people like OBAMA wameshaanza kwani wewe Jakaya na Pombe wako why are you so shy au mmekula yamini na wahindi!!!!
 
Siye Wadanganyika tunachekesha sana. Huyu bwana alihusika kwa karibu sana na maamuzi ya uuzwaji nyumba ambayo yameliingizia Taifa hasara kubwa sana kwa kuwalipia Wafanyakazi mabilioni ya shilingi kwa gharama za kuishi mahotelini. Miezi michache iliyopita kaliingizia tena Taifa hasara ya shilingi bilioni 1.2 kwa gharama za kuhifadhi samaki, lakini pamoja na maamuzi haya mabovu ambayo yameligharimu Taifa pesa chungu nzima bado kuna wadanganyika wanamuona huyu bwana anastahili sana kuwa “Kiongozi” wa nchi yetu kitu ambacho kinanistaajabisha sana. Hivi mtu afanye nini mpaka tuweze kusema huyu kama kiongozi hatufai kutokana na mambo kadhaa wa kadha? Naona kuna watetezi wa Magufuli wamemwaga hapa kwa fujo ili kumpigia debe magufuli.

Hakuna issue ya kuchekesha, isipokuwa watu wanaangalia kiongozi anathubutu kusimamia maamuzi mazito. Katika serikali ya sasa JPM ameonyesha uwezo huo wa kujaribu kusimamia kwa karibu majukumu yake na hiyo inafanya aonekane ni kiongozi mzuri kuliko wengine.
 
..mimi ningemshukuru sana Magufuli kama angejutia makosa yake kwa kuuza zile nyumba za serikali.

..halafu ningemuona shujaa kama angeamua kurejesha serikalini nyumba aliyojitwalia ktk zoezi lile.

..waandishi wa habari mkikutana na Magufuli muulizeni kwanini harejeshi nyumba yetu aliyojitwalia?

Jokakuu hapo kidogo naomba mwongozo... ni waziri peke yake ndiye aliyepitisha huo mpango wa kuuza nyumba?

Kumbuka maamuzi kama yale hutokea juu' na zaidi ujue kwamba Mkapa na wenzake (hata mashemeji na watoto wa mashemeji) walipata nyumba? a loyal servants kuna sehemu huwa anatekeleza tu sera... nahisi ndicho kilichomkumba Dr. Magufuli, that being said; tukumbuke pia kwamba yeye ni mtu na he is bound to make mistakes!!

Tumpongeze kwa haya anayofanya wakati tukigeuka nyuma na kurejea alipojikwaa kuweka mambo sawa
 
Tanzania ni dampo la bidhaa za kila aina na sasa samaki waliovuliwa nje na kuwekwa kwenye maboksi wanaingizwa kila siku bila ya kukaguliwa na mamlaka za afya ili kujua kama wanafaa kwa matumizi ya watanzania. Hizi mamlaka zilikuwa wapi wakati wote huo mpaka waziri atoe tamko? Leo hii ukienda Ferry bado utakuta wanauzwa bila ya matatizo, wanaoumia ni walaji.
 
Kwa hiyo Mkuu wake hata kama anaboronga na nchi inaenda mrama, yeye anaangalia pembeni tu bora liende! basi turidhike tu na kumpigia makofi kwamba ni kiongozi bora! Kiongozi bora huwa hakai kimya kama anaona nchi inaenda mrama lazima atatoa sauti yake ili kuinusuru nchi, kukaa kwake kimya ni kuonyesha kuridhika na utendaji wa boss wake ambao unalalamikiwa kila siku na Watanzania walio wengi.

Bila shaka hiyo ni shauku ya kuonyesha msimamo na si kupata fursa ya kusaidia walio wengi kwa muda mrefu. Nyumba sawa kachukua na si halali, alikuwa na uwezo wa kuigomea tokea wakati wa Mkapa. Unaonaje kama angetupwa nje tangu wakati huo, faida tuzipatazo kwa wakati huu kutoka kwake tungezipata? Natamani nageendelea kubaki wizara ya miundombinu lakini yawezekana wanamtoa ili kumkomoa na yeye anachukulia kuwa huko nakopelekwa kumelala na anapafanya pawe live

Bravo Dakta Magufuli
 
Back
Top Bottom