Nimejaribu sana kulinganisha hizi kondoms za roughrider, si kama zilizokuwepo miaka ya nyuma. Hizi za siku hizi kwanza kuzifungua toka kwenye kimfuko chake ni hadi utumie meno au kijiwembe, hazifunguki kirahisi. Pili zinaonekana kama zimebana na kwa kweli hazihimili vishindo kama zile za miaka takriban mitano iliyopita. Hapa nabaki najiuliza kulikoni, wajanja wameamua kujitajirisha kwa kufanya ufisadi wa kutengeneza kondoms feki kwa gharama ya maisha ya watanzania.
Kitu kingine nilicho na wasiwasi nacho ni haya maziwa ya Nido yaliyo na label ya Africa Kusini. Haya nayo siamini kama ni maziwa yanayostahili kutumiwa na watanzania wa leo. Ni kwamba ukiyatia kwenye maji ya moto yanatengeneza vijibonge vidogovidogo, hayayeyuki vizuri. Hata ladha yake inatia shaka. Hapa napo naona wahuni wa kibiashara wameshaingilia soko wanatutengenezea bidhaa feki. TBS mko wapi? Nyie ndiyo tegemeo la afya na maisha yetu pambaneni na hawa wahuni wasiojali maisha ya watu.