GE2025 Asanteni Simba yangu kwa kuturejeshea furaha japo ya muda

GE2025 Asanteni Simba yangu kwa kuturejeshea furaha japo ya muda

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
373,018
Reaction score
864,149
Kuna kitu kilichokuwa kimekosekana nchini..

Furaha ya kweli, Furaha ya asili
Furaha halisi

Furaha at free will..! Furaha ya hiari

Watu Leo wamerindima na kufefea vibe kama lote toka moyoni

Makusanyiko ya hivi karibuni pamoja na kuwa na rangi yenye kumaanisha uhai.. Lakini yalikuwa makusanyiko mfu.. Yaliyobeba mirindimo ya ufu! Nyuso zilizochoka! Taswira zinazoakisi., maswali, hofu na sintofahamu.. Ni kama kusanyiko la makaburini kwenye ibada ya mazishi

Baada ya miezi kadhaa ya huzuni, fadhaa majonzi na ukiwa leo Tanganyika imeonesha tabasabu.. Waliojaribu kupiga simu kwa maslahi binafsi walipotezewa vibaya sana! Nadhani wamejifunza kwa njia ngumu.

Pia soma Mashabiki wa Simba wagoma kumshangilia Rais Samia akitoa salam katika tukio la Simba day

Vibe la ushindi halikuwa kubwa kama vibe la kukutana rangi zote, imani zote, itikadi zote! Bila kupangiwa bila kutishwa bila kuongozwa

SIMBA DAY imelifanya taifa litabasamu.. Nimeona watanzania wakiwa na furaha isiyo na vigezo wala masharti wala mabunduki na umbwa ya kutisha

Asanteni sana SIMBA kwa kutukumbusha furaha iliyopotea
IMG-20250910-WA0058.jpg
 
Tumejaza uwanja kwa ticket za kununua 🔥🔥🔥🔥🦁🦁🦁🦁

kuna timu huko mtaani inagawa ticket 🎟 na jezi kama kifungashio 😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom