Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Ee Mungu nakushukuru umetuvusha nusu mwaka salama.
1. Maadui walikuja ili watuangamize, ukawatawanya! Asante sana Mungu.
2. Magonjwa yalitupata, ukatuponya nayo yote. Nakushukuru Mungu wetu.
3. Umebariki kazi za mikono yetu, tumepata pesa ya kununua mahitaji muhimu. Asante Mungu mkuu.
4. Tumesafiri huku na kule, na kukutana na ajali, hukutuacha tuangamie. Asante Mungu mwenye nguvu.
5. Ibilisi alituletea vishawishi na majaribu ya uzinzi, umetusaidia kumpinga na kumshinda. Asante Muumba mbingu na nchi.
6. Tumepita katikati ya mambo ambayo yangetufanya tutoe machozi sana, lakini Mungu umetuepusha nayo yote. Asante Mungu mwenye rehema.
7. Tumekutana na hali ngumu za kuvunja moyo. Kwa neema yako tumefarijiwa. Asante Mungu Mfariji
8. Umetupa mvua na chakula cha kutosha. Asante Mungu mwaminifu.
9. Katika ndoto zetu usiku, ulizungumza nasi na kutuonya. Asante Mungu Mtakatifu.
10. Katika nusu hii ya mwaka, tumesikia habari za vita na machafuko, zilizotufanya tusikitike. Umetukumbusha kuwa mwisho umekaribia, karibu Yesu atakuja kutufuta machozi. Asante Mungu mwenye pendo kuu.
Nakushukuru kwa Jina la Yesu Kristo. Amen
1. Maadui walikuja ili watuangamize, ukawatawanya! Asante sana Mungu.
2. Magonjwa yalitupata, ukatuponya nayo yote. Nakushukuru Mungu wetu.
3. Umebariki kazi za mikono yetu, tumepata pesa ya kununua mahitaji muhimu. Asante Mungu mkuu.
4. Tumesafiri huku na kule, na kukutana na ajali, hukutuacha tuangamie. Asante Mungu mwenye nguvu.
5. Ibilisi alituletea vishawishi na majaribu ya uzinzi, umetusaidia kumpinga na kumshinda. Asante Muumba mbingu na nchi.
6. Tumepita katikati ya mambo ambayo yangetufanya tutoe machozi sana, lakini Mungu umetuepusha nayo yote. Asante Mungu mwenye rehema.
7. Tumekutana na hali ngumu za kuvunja moyo. Kwa neema yako tumefarijiwa. Asante Mungu Mfariji
8. Umetupa mvua na chakula cha kutosha. Asante Mungu mwaminifu.
9. Katika ndoto zetu usiku, ulizungumza nasi na kutuonya. Asante Mungu Mtakatifu.
10. Katika nusu hii ya mwaka, tumesikia habari za vita na machafuko, zilizotufanya tusikitike. Umetukumbusha kuwa mwisho umekaribia, karibu Yesu atakuja kutufuta machozi. Asante Mungu mwenye pendo kuu.
Nakushukuru kwa Jina la Yesu Kristo. Amen