Asante Mama yangu.

Asante Mama yangu.

fimboyaukwaju

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2020
Posts
6,108
Reaction score
8,128
Leo ni Mothers Day.Nakushukuru sana mama yangu,japo haupo duniani,sitakusahau kwa mema yako.Japo hukusoma japo darasa moja,kila nilipotoka shule ulikuwa ukichukua madaftari yangu kukagua tiki na kosa,na ulikuwa anahesabu tiki ni ngapi na kosa ngapi,na baba aliporudi jioni ulimwambia kama nimekosa nyingi au nimepata nyingi.Yote niliyofanikiwa ni kwa ajili yako.Mungu akupe mapumziko ya milele
 
Pongezi sana kwao , wale ambao mama zao wapo hai leo tuwabless na vipesa kidogo waJipongeze hata na vi bia viwili 🍺
20260427_221857.jpg
 
Kasherehekea au kakumbuka mazuri mama yake aliyomfanyia?
Uzuri hili bandiko haliondoi nguvu zake za kiume.
Asante kwa kumuelewesha,tena sijayaweka mema yote ya mama na maajabu ya mama.Hebu fikiri,akiwa msichana wa miaka 17 ambae hakuwahi kusoma japo darasa moja,akiwa hajui kusoma wala kuandika,lakini akaolewa na mzungu na ndio katuzaa sisi.
 
Asante kwa kumuelewesha,tena sijayaweka mema yote ya mama na maajabu ya mama.Hebu fikiri,akiwa msichana wa miaka 17 ambae hakuwahi kusoma japo darasa moja,akiwa hajui kusoma wala kuandika,lakini akaolewa na mzungu na ndio katuzaa sisi.
Hongera kwa kua chotara! Wamama wanajitoa muhanga sana kwaajili ya watoto wao
 
Mama yako alikuwa miongoni mwa mama bora.aliwakuza kwenye maadili na njia iliyonyooka.
Ni wamama wengi zamani walikuwa hivo
Usiniulize haya nimeyajulia wapi.hongera
 
Mama yako alikuwa miongoni mwa mama bora.aliwakuza kwenye maadili na njia iliyonyooka.
Ni wamama wengi zamani walikuwa hivo
Usiniulize haya nimeyajulia wapi.hongera
Ni kweli.Natamani kuandika japo uzi mfupi kuhusu mama alivyotulea,tulivyokua na kujitegemea na jinsi alivyotuaga kuwa anaondoka kuelekea ulaya na mumewe na kuniagiza mie nimtunzie ndugu zake
 
💘💝💕💖❣️❤️💞♥️💓🔥🔥🔥🥂
 
Upumbavu huu.... kwa hio mama yako anasoma hapa ?

Huu mda na nguvu ulotumia hapa , ungempa zawadi nzuri anayoipenda...... ! Pengine ungeonekana wa maaana ....

Sio kuja kujaza server hapa !

Unadhan wengine hatuna mama ? Hatuwapendi ?
 
Upumbavu huu.... kwa hio mama yako anasoma hapa ?

Huu mda na nguvu ulotumia hapa , ungempa zawadi nzuri anayoipenda...... ! Pengine ungeonekana wa maaana ....

Sio kuja kujaza server hapa !

Unadhan wengine hatuna mama ? Hatuwapendi ?
Umesoma kichwa cha habari umekimbilia kucomment
 
Punda wa Mkojani Mama ako hastahili siku moja muhimu kwa mwaka mzima.
Anastahili kuhesabiwa siku zake kuanzia siku, week, Mwezi hadi Mwàka.

Kwanini awe na siku moja tu, siku moja !!
 
Back
Top Bottom