Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,727
- 218,289
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba yale Maandamano yaliyoletwa na Mungu , ya kupinga Dhiki , Ufukara , Ugumu wa Maisha , Bei kubwa ya bidhaa zote ikiwemo Vyakula , pamoja na kupinga miswada mibovu ya sheria za uchaguzi , Maandamano yanayoandaliwa na Chama chenye Maono CHADEMA , Sasa yameingia Arusha .
Wataalam wa kuhesabu namba baada ya kujua kwamba Maandamano hayo makubwa yamepangwa kufanyika tarehe 27 /02/2024 na baada ya kufahamu kwamba leo ni 21/02/2024 , Wamedai kwamba zimebakia siku 6 tu kabla ya shughuli hiyo kubwa kufanyika .
Usiondoke JF , maana mtumishi wako Erythrocyte atashiriki na atakuletea kila kinachojiri , ikiwemo taarifa za wote wanaoingilia Maandamano hayo kwa shari kama alivyofanya Biteko Mbeya .