Arusha sasa ni Salama - Kikwete

Arusha sasa ni Salama - Kikwete

hakika ujinga wa lema uliondoa amani ya arusha! sasa arusha pako swari na kila mtu anafanya kazi zake kwa amani!
 
Kama mzaliwa na mkazi wa Arusha, nina wasi wasi na hotuba ya JK kama aliongelea jambo alilo na uhakika nalo au kalishwa mapropaganda na watu wake wa UWT.

Kwanza ieleweke kwamba amani ilikosekana Arusha siku ile ya mabomu tu, siku iliyofuata kila mtu na shughuli zake kilichobaki ilikuwa 'intelejensia'.

Pili leo tumeamini kauli ya Lema kwamba ikulu ilihusika na yeye kuvuliwa ubunge na imedhihirika kwa JK kusema Arusha sasa iko salama, simply baada ya Lema kuvuliwa ubunge. Tunashukuru maana ndo kazidi kuizika CCM Arusha.

Ukweli ss wakazi wa Arusha siku zote tuko peace ila hawa maintelejensia ndo wanatuletea sifa mbaya.

Labda niseme ubaya wa Arusha ni kutopendwa kwa Magamba na ni waasisi wa M4C.
 
Dah! Sa huyu mtani wangu Mkwele anataka kumaanisha nini hapa......Watu wengine bana...
Hahaha mkuu wata li-censor na hili neno kama lile lenye 'r', hapa umeniacha hoi sana, maana ukiandika lile unapata stars sita ******.

Kikwete badala ya kuunganisha wanannchi yeye anawagawa huo si uongozi. President hatakiwi kufanya propaganda hiyo kazi angewaachia kina Nnauye. Unaposema Arusha kuna amani unatakiwa kueleza kilichosababisha amani itoweke na hatua mlizochukua kuirudisha kama serikali hapo ndipo unapata Credit kama President. Kauli kama hizi ndizo zilezile za kuendeleza vijembe. Kiongozi wa nchi unatakiwa clear to the point siyo meandering.
 
Mnafiki dunia nzima. Aman ipo siku zote Arusha wao ndo wanatuletea hali ya sintofahamu kwa kutupandikizia wasiotakiwa ili kuficha uovu wao. Hata atukenulie vip hapa arusha ajue si kwake ndio mana anakuja mara mbili mbili ndan ya siku moja anaogopa nn?. Arusha sio kwao bagamoyo huku tunaelewa every move tht he takes zamakafaz.
 
Vipi Mkuu wangu Crashwise, mlimpopoa kwa mawe?! Manake hapa wana-Arusha walikuwa wanajigamba kwamba siku Kikwete akitia mguu Arusha lazima apigwe mawe...je, mlifanya hivyo?! Au jamaa alihunduria mkutano huo thru Video Conference?! Ni katika kutaka kufahamu tu mkuu wangu!!!
Aliingia kimya kimya,alikuja akageza dara af akaja tena siku hiyo hiyo km mwizi
 
Kikwete ni mbabaishaji sana; kama raisi wa nchi bado anafanya kazi zake kama sisi watu wa hapa uwanja wa fisi ambao tunafikiria mambo yetu kwa kutumia mdomo badala ya kutumia akili. Hivi katika zile ahadi za uchaguzi ni ipi imeshatekelezwa
 
naomba jimbo ARUSHA MJINI litangazwe rasmi kwamba ni HURU, kikwete agombee UBUNGE na mama salma awe kampeni manager wake , watumie rasmilali zote za nji hii tulizowapa kwa mujibu wa katiba - ISEE HAWASHINDIIIIIII........ HAWASHINDI MANGIIIII..... achana na ile KITU, ILE KITU NI NOMAAAA............
 
Hukumu iliyomvua Lema ubunge ilikuwa handout toka ikulu. Lakini JK aelewe kuwa mwisho wa ubaya ni aibu.
 
Kwa uchunguzi wangu naona Lema maisha yake kisiasa yanahesabika sio bure naona wameamua kumshikia kooni.Hata hii rufaa sijui sina imani nayo tena.
 
Nadhani katika wapumbavu
Tanzania hii na wewe umo, huwezi ukatukana tusi baya kiasi hicho Rais wa
nchi.
Nyie CHADEMA mtabaki hivyo hivyo mpaka mwisho maana Ubaya hautoruhusiwa
kukanyaga patakatifu- Matusi yako ipo siku yatalipizwa, Take
care.

Kwani raisi anauatakatifu gani? Mali wa kwao wamempa kibano cha mbwa mwizi na na huyu wetu cha nazi anastahili!

We matatizo yote tuliyo nayo mfumuko wa bei, na taabu mbalimbali za wananchi wa Arusha, yeye anaamini yanaisha kwa lema kutokuwa mbunge! Headless chicken presidaa!
 
ni kweli maana mr maandamano now hana power amejitaid kukishawishi chama kifanye ziara ili apate posho kwa maana ana hali mbaya

Babako ndo ana hali mbaya na kwa taarifa yako kamanda lema hajawahi kuishi kwa posho na ndo maana hata vikao vilivyokua vya posho kama bunge na kamati zake alikua anahudhuria pale alipokua na hoja au kama ana cha kuongea cku hiyo...
 
Ni hatari sana kwa kiongozi mkuu wa nchi kwa majungu amani ipi iloyo potea arusha na ameirudisha nani mbona anakuja na kuondoka kama mwizi hapa . Mi naona yeye mwenyewe na ccm yake ndio hawana amani apa arusha.
 
Jamani pamoja na yote yaliyosemwa kwa hili tusipotoshe umma, nimesoma vyema hotuba yake ya leo na sijaona sehmu ambayo kikwete amebainsha aliyoyatoa mtoa mada. Tupingane lakini isifike wakati wa kuleta yale ambayo hayapo. Hebu someni hotuba yake kwanza ndiyo u-comment. sawa sisi ni wapinzani wake na chama chake cha magamba lakini isifikie hatua hii.

Aliyasema hayo kwa kinywa chake kupitia kituo cha ITV usiku wa jana... Na kama hiyo haitoshi hata mkuu wa mkoa magesa aliyasema hayo hayo wakati anaapisha wakuu wa wilaya wiki 2 zilizopita na vyombo vyote vya habari viliandika na kuzungumza
 
Back
Top Bottom