Arusha sasa ni Salama - Kikwete

Arusha sasa ni Salama - Kikwete

Kwa hiyo lema alikuwa anavunja amani kwa mawazo yake?.
THE UNSEEN IS ILLUSTRATED BY THE SEEN.

Mkuu anaogopa Arusha kama Darfur. Mbona wakazi wa Ar hawana noma na mtu. wanaishi kwa amani tu. kazi ya ujenzi wa taifa inaendelea kama kawa kama dawa. Apeleke tu vikao huko, wenzetu waendelee kuvuna.
 
Jamani pamoja na yote yaliyosemwa kwa hili tusipotoshe umma, nimesoma vyema hotuba yake ya leo na sijaona sehmu ambayo kikwete amebainsha aliyoyatoa mtoa mada. Tupingane lakini isifike wakati wa kuleta yale ambayo hayapo. Hebu someni hotuba yake kwanza ndiyo u-comment. sawa sisi ni wapinzani wake na chama chake cha magamba lakini isifikie hatua hii.
 
JK NI KIGEU GEU SANA.......SOMA HIKI KIPANDE


Ndugu Wananchi;
Jambo lingine la kushangaza zaidi ni kule kutokea vurugu na ghasia hizi dhidi ya Muungano wakati ambapo Serikali imetoa fursa sasa kwa watu kutoa maoni yao kwenye mjadala wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Kama tujuavyo sote, Tume ya Katiba imekwishaundwa na inajiandaa kupita kote nchini kukusanya maoni ya wananchi juu ya Katiba mpya waitakayo. Kama mtu ana maoni yake kuhusu Muungano, hiyo ndiyo fursa ya kufanya hivyo. Utaratibu mzuri umewekwa kwa ajili yetu sote, vurugu za nini?




si ndiye huyu alisema swala la Muungano lisijadiliwe??
 
Jamani pamoja na yote yaliyosemwa kwa hili tusipotoshe umma, nimesoma vyema hotuba yake ya leo na sijaona sehmu ambayo kikwete amebainsha aliyoyatoa mtoa mada. Tupingane lakini isifike wakati wa kuleta yale ambayo hayapo. Hebu someni hotuba yake kwanza ndiyo u-comment. sawa sisi ni wapinzani wake na chama chake cha magamba lakini isifikie hatua hii.

matatizo ya kusoma kwa kuruka ruka yanakusumbua...hebu soma hapa chini



Ndugu Wananchi;
Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi na shukrani nyingi kwa ndugu zetu wa Arusha kwa kuwapokea vizuri na kuwakarimu vyema wageni wetu hao. Nawaomba waendelee na moyo huo mpaka watakapoondoka wote. Naomba kuwepo kwa mkutano huu kuwakumbushe umuhimu wa mji wenu kuwa tulivu. Miaka miwili iliyopita isingekuwa rahisi kwa watu au shirika kubwa la kimataifa kama Benki hii kuamua kufanya mkutano wake Arusha. Isitoshe hata sisi wenyewe tusingeshawishika kuomba au kukubali maombi ya namna hiyo. Lakini sasa imewezekana. Naomba kila mmoja wetu aweke azimio moyoni mwake la kuhakikisha kuwa hali ile haijirudii tena. Nyota ya Geneva ya Afrika lazima iendelee kuangaza. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo.
 
This is one of too low Mr Kikwete have ever give to his people, This means Mr Lema was right for every second and every minute had given a statement. Ni ukweli usiopingika sasa kuwa kuvuliwa ubunge kwa Lema kulikuwa na mkono wa rais. Hili jambo litampandisha chati Lema kuliko rais alivyo fikiria.

Nashindwa kuamini kuwa Lema alikuwa hatari nanma hiyo kwa utawala wa Jk.

I stand with Lema...
 
nadhani sasa kwa huu mda wanamalizia ishu zao, lema aliwabana inavyotakiwa na kwa kumpeleka honeymoon wanamalizia dili zao
 
anaogopa vitega uchumi vya Ridhiwani na Halfani kumegwa ,Mtu asiye nabusara kabisa Raisi gani asiyejua haki ya watu Polisi wauwe watu halafu yeye asichukue hatua anadhani hizo propaganda zitamsaidia au anawaagiza majaji wafanye atakavyo yeye yana mwisho kuna siku yatakuja kumpata mwanae pia hii dunia hakuiumba yeye
 
Ni wazi na kweli kuwa ikulu ilihusika na Hukumu ya Lema na hii Watanzania wengi tunaweza kuamini kauli hii ya Kikwete. Nina wasiwasi rufaa yake haitashughulikiwa haraka. Lakini ipo siku.
 
Jk kweli ana vituko vurugu za arusha chanzo ni yeye na ccm yake anafikiri tumesahau anachotakiwa kufanya ni kuwaomba msamaha watu wa arusha na Mheshimiwa Lema kwani siku zao kutawala Tz zina hesabika
 
Nilishasema na narudia kusema tena kuwa "Peace should never mean ONLY the absence of Guns and Bomb Blasts" It is more than that. Watu wako kimya lakini mioyoni mwao kuna kelele balaa. Mwambieni aende Arusha kuhutubia hadhara aone kama watu wa kumsikiliza hawatasombwa kwa malori kutoka vijijini!!!!!
 
Jk kweli ana vituko vurugu za arusha chanzo ni yeye na ccm yake anafikiri tumesahau anachotakiwa kufanya ni kuwaomba msamaha watu wa arusha na Mheshimiwa Lema kwani siku zao kutawala Tz zina hesabika

Ebo! Lema aombwe msamaha kama nani? Unaweza kuomba msamaha chalii mhalifu? unajipendekeza nini kwake?

Arusha without the so called MP Lema is a much much better place now!


rip dogo Lema.
 
Nilishasema na narudia kusema tena kuwa "Peace should never mean ONLY the absence of Guns and Bomb Blasts" It is more than that. Watu wako kimya lakini mioyoni mwao kuna kelele balaa. Mwambieni aende Arusha kuhutubia hadhara aone kama watu wa kumsikiliza hawatasombwa kwa malori kutoka vijijini!!!!!

ZINDUKA! You are underestimating the power of CCM!
 
"...Ndugu Wananchi;
Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi na shukrani nyingi kwa ndugu zetu wa Arusha kwa kuwapokea vizuri na kuwakarimu vyema wageni wetu hao. Nawaomba waendelee na moyo huo mpaka watakapoondoka wote. Naomba kuwepo kwa mkutano huu kuwakumbushe umuhimu wa mji wenu kuwa tulivu. Miaka miwili iliyopita isingekuwa rahisi kwa watu au shirika kubwa la kimataifa kama Benki hii kuamua kufanya mkutano wake Arusha. Isitoshe hata sisi wenyewe tusingeshawishika kuomba au kukubali maombi ya namna hiyo. Lakini sasa imewezekana. Naomba kila mmoja wetu aweke azimio moyoni mwake la kuhakikisha kuwa hali ile haijirudii tena. Nyota ya Geneva ya Afrika lazima iendelee kuangaza. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo..."

1. Miaka miwili iliyopita(June 2010 - June 2010?) kulikuwa na nini tofauti na sasa?
2. Je, serikali ilifanya bidii gani kuhakikisha panakuwa na hali nzuri ili iendelee kuwa mwenyeji wa mikutano na makongamano kama hayo?
3. (Yaliyopita si ndwele) tugange yajayo, maana yake ni kuwa kama ni makosa yalishafanyika na bidii za wakati huu ni kuhakikisha kuwa kasoro za nyumba hajirejei/hazijitokezi tena.Je, hii inatuambia kuwa zitafanyika bidii zote (kupitia Mahakama ya Rufaa) na hata kwenye uchaguzi wa marudio na hata uchaguzi wa 2015 kuhakikisha kuwa " makosa yaliyofanyika miaka miwili iliyopita hayarudiwi tena"?
 
matatizo ya kusoma kwa kuruka ruka yanakusumbua...hebu soma hapa chini



Ndugu Wananchi;
Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi na shukrani nyingi kwa ndugu zetu wa Arusha kwa kuwapokea vizuri na kuwakarimu vyema wageni wetu hao. Nawaomba waendelee na moyo huo mpaka watakapoondoka wote. Naomba kuwepo kwa mkutano huu kuwakumbushe umuhimu wa mji wenu kuwa tulivu. Miaka miwili iliyopita isingekuwa rahisi kwa watu au shirika kubwa la kimataifa kama Benki hii kuamua kufanya mkutano wake Arusha. Isitoshe hata sisi wenyewe tusingeshawishika kuomba au kukubali maombi ya namna hiyo. Lakini sasa imewezekana. Naomba kila mmoja wetu aweke azimio moyoni mwake la kuhakikisha kuwa hali ile haijirudii tena. Nyota ya Geneva ya Afrika lazima iendelee kuangaza. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo.

Miaka miwili iliyopita (2010) kulikuwa na vurugu gani Arusha? Nenda kamdanganye mkeo, sie tushainyaka siku nyingi kuwa ni hao matahira wako wanaojiita polisi ndio wanao hatarisha amani hapa nchini.
 
Arusha itakuwa salama sana endapo mbunge wetu atarejeshwa, na meya wa kichina akapigwa chini.

Mungu ibariki Arusha
Mungu ibariki Tanzania
Munu ibariki CHADEMA
Mungu mbariki Lema

Mungu ulaani uonevu unaofanywa na serikali ya Kikwete,
na watu wote waseme Aaaamen!
 
Hata Zanzibar kawapa pole walioathirika na uamsho
 
asiishie tu kusema amani imerudi! Kwanza walioipoteza amani ni magamba na polisi wake. Pili atuambie kwa nini wamempora lema ubunge je hiyo ndo amani? Kama si busara za cdm kutulia hili analosema lingekuepo?!
 
Mnafiki dunia nzima. Aman ipo siku zote Arusha wao ndo wanatuletea hali ya sintofahamu kwa kutupandikizia mameya wasiotakiwa. Hata atukenulie vip hapa arusha ajue si kwake ndio mana anakuja mara mbili mbili ndan ya siku moja anaogopa nn?. Arusha sio kwao bagamoyo huku tunaelewa every move tht he takes zamakafaz.
 
Back
Top Bottom