Arusha - Je tunaridhika na utendaji wa Godbless Lema?

Arusha - Je tunaridhika na utendaji wa Godbless Lema?

Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha

Ilikuwa nianze na mambo mengine ila nimeona niahirishe kwanza nichangie hoja yako. Hoja umeifikiria vizuri ila nahisi umeshindwa kuipresent. Unauliza kama mnaridhika na utendaji wa Lema na kama anatimiza majukumu mliyomhitaji ayatimize. Je majukumu mliyompa ni yapi???ungeyataja hapa ili mchangia mada anayetaka kupima utendaji wa Lema imuwie rahisi. Lakini kwa kuficha majukumu mliyomhitaji kuyatimiza unakuwa hujafanya sawa mana huwez pima chochote hapa mana perceptions zetu kwa majukumu ya wabunge zinatofautiana sana na wengi wetu hatujui majukumu ya mbunge. Kimsingi wengi wanadhani mbunge ni mfadhiri, hii si sawa.

Aidha, umesahau kuwa Madiwani walikula kiapo cha kuutumikia Umma wao wenyewe na sio kwa kupitia ushawishi wa Lema. Kumbuka hapo Arusha kuna madiwani hadi wa CCM so ukitaka kumbana Lema kwa utendaji mbovu wa madiwani unakuwa hujamtendea haki. Maana hukumchagua diwani wa CCM kwa kushawishiwa na Lema,madiwani wa CDM ok ingawa napo hupaswi kuliweka hivyo. Kila mtu diwani/mbunge ana majukumu yake aliyoapa kuyasimamia ktk kipindi chake. So mtight kila mtu individually.

Lakini naona central question ulitakiwa kuuliza wanaarusha kama wanaridhika na utendaji wa Serikali ya Kikwete. Kumbuka jukumu la Lema ni kuisimamia serikali, kutunga sheria Bungeni, kuwakilisha interests za wananchi wake bungeni na kuhamasisha/kusimamia shughuli za maendeleo, so kama Serikali haina cha kufanya kwenye maendeleo nadhan kumnyooshea Lema kidole huwa tunakosea sana. Kuna dhana potofu iliyojengeka miongoni mwetu ya kudhania Mbunge ni mfadhiri. Jukumu kubwa la Lema ni kutunga sheria bungeni, nadhani kazi hii ameifanya kwa kuchangia hoja mbalimbali ktk misaada ya sheria mbalimbali kupita wabunge wengi tu pale mjengoni. Kuhusu jukumu lake la kuibana Serikali, hapo ndo usiseme na kwenye maendeleo sina takwimu za kutosha ila kupitia hapa JF tulielezwa he is doing well. Labda utabanaishe majukumu gani mengine zaidi ya haya mlitumana huko mtaani ndo tutaweza kukuelewa otherwise, utaonekana ni mjenga chuki miongoni mwa jamii sifa ambayo ni haipaswi kumilikiwa na kijana wa karne hii.

Kwa heshima naomba kuwasilisha.
 
aah kaka maisha hayaendi hivo bana! hili ni jamvi la weledi. maswali yako wazi na ni vizuri ukitoa hoja kuliko kuwa mkali tu. hata hivyo kama wewe sio mkazi wa jimbo la Arusha hili halikuhusu maana huna cha kujibu. waachie basi wanaoishi Arusha wajibu kulingana na muono wao.

tulia dawa yako ipenye!!,bado doz kukamilika huu ni mwanzo tu!Tumewachokaje?Ni zaidi ya saratani ya mifupa mtajibebaje?
 
kama lema angeweza kufanya kazi kwa uhuru hapa A town basi tungekuwa mbali..lakini kuna jitihada kubwa za kumkwamisha lema na ndio maana hata last year alipomwalika mkuu wa mkoa kama mgeni rasmi kwenye mfuko wa mbunge wa kusomesha wale watoto 600..hakutokea RC..na utaona hata swala la umeya imetumika nguvu kubwa kumuweka ili kuficha uovu na watu waendelee kula..ni jukumu letu kuendelea kumsapoti lema huku tukiendelea kupunguza gambaz kwenye levo zote za uongozi..ni hayo tu
 
Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha

mkuu umewashika pabaya wadau wengi sana hapa jamvin. Usitegemee kuna mtu atachangia kwa kumkosoa LEMA ambaye arusha wanamwona kama ndiyo raisi wao.Mungu mtu.

Kiukweli maisha ya arusha ni magumu sana vijana ambao ninguvu kazi wanaishia kunywa gongo(pure),banana,viroba na mbege,bila kusahau bangi.
Wavutaji wa unga ni wachache sana hawana uwezo wa kumudu gharama zake.

Mi ningeomba woote mnaompinga na kumtusi na kumtuhum mwanzisha thread kuwa mchimbi hembu anikeni mazuri yaliyokwisha fanywa na huyo kilema juu ya arusha.
Acheni kupenda vibaya.

Hakuna zuri likosalo kasoro.
 
Mkuu umeongea point sana . Kwakweli hali mbaya sana hasa upande wa barabara na ajira kwa vijana . Nafikiri 2015 tutajua chakufanya.

Barabara za lami katika Tanzania zilizokwisha tengenezwa, ziliopo kwenye matengenezo na mikataba ambayo imesha sainiwa na zipo njiani kuanza kutengenezwa ni zaidi ya barabara za awamu zote ukichanganya pamoja. Ajira ndio usiseme. Bodaboda peke yake zimeajiri kuliko ajira zilizowahi kutolewa na awamu zote kwa pamoja.

Hapo huna hoja, tafuta lingine.
 
aah kaka maisha hayaendi hivo bana! hili ni jamvi la weledi. maswali yako wazi na ni vizuri ukitoa hoja kuliko kuwa mkali tu. hata hivyo kama wewe sio mkazi wa jimbo la Arusha hili halikuhusu maana huna cha kujibu. waachie basi wanaoishi Arusha wajibu kulingana na muono wao.
Mkuu hata wewe sio mkaazi wa arusha kwani kwa hayo maswali yako yaonyesha kabisa un chuki binafsi na mh lema.

Kwa sisi wana wa arusha tunaridhika naye kwa yote anayotupigania. Lema ametuonyesha kuwa kiongozi si mungu mtu. Lema amejishusha kwa wananchi wake na hapo tunaweza kumfikia kiurahisi na hata kumueleza shida zetu ana kwa ana.

Hay ya kuhusu utendaji wa lema naomba tuachiwe wana wa arusha!
 
Asijidanganye mtu kuwa mbunge wa upinzani anaweza kutimiza ahadi zake za kampeni, atachokifanya zaidi ni kufatilia yaleyale yatakayotimizwa na Serikali iliyopo madarakani, na sera zitakuwa ni za chama tawala.

Cha ziada atakachokifanya ni kupiga porojo tu.

wakati huo huo wale wa chama tawala wanachofanya ni kuanzisha miradi yao kwa kutumia rasilimali za wananchi..na pia kuwa mbali na wananchi mpaka msimu wa uchaguzi utakapowadia..
 
Bucho unaonekana unaijua A-Town, kumbe nimegundua wewe ni wa kuja, au la una lako jambo!
Kam aupo Arusha kwa sasa utakuwa umeona mabadiliko katika barabara kadha za mji!...
1.Hujaona bara2 ya round about ya Unga Ltd kupitia FIRE kwenda kuunganisha East Africa Hotel ikiwa inajengwa?
2.Hujaona eneo la Makao Mapya bara2 zile zikiwa matengenezo?
3.Huoni bara2 ya Ngarenaro to Majengo ikiandaliwa kwa upanuzi?
Ni kweli hazi-meet demand ya barabara, lakini huwezi kufanya kazi hizi overnight!
We should learn to appreciate!

PakaJimmy,
Yote hayo ulioyaandika yameletwa na Lema Kupitia miradi gani?
 
mkuu umewashika pabaya wadau wengi sana hapa jamvin. Usitegemee kuna mtu atachangia kwa kumkosoa LEMA ambaye arusha wanamwona kama ndiyo raisi wao.Mungu mtu.
Kiukweli maisha ya arusha ni magumu sana vijana ambao ninguvu kazi wanaishia kunywa gongo(pure),banana,viroba na mbege,bila kusahau bangi.
Wavutaji wa unga ni wachache sana hawana uwezo wa kumudu gharama zake.
Mi ningeomba woote mnaompinga na kumtusi na kumtuhum mwanzisha thread kuwa mchimbi hembu anikeni mazuri yaliyokwisha fanywa na huyo kilema juu ya arusha.
Acheni kupenda vibaya.
Hakuna zuri likosalo kasoro.
labda wewe sema au toa wazo mbadala ulitaka Lema afanyeje; afungue makampuni, maduka, viwanda, nk kisha aajiri vijana

Mbona unaelezwa kazi za mbuge huelewi

Sasa tuna omba mfanyo wa mbunge 1 tu wa chama chote chote aliyetengeza ajira na kuajiri vijara wengi kihivyo ili tufanye comparison au tumwambie Lema aaige
 
Kitu ambacho ni kigumu kukielewa ni siasa za Lema pamoja na wafuasi wake wa Arusha.

Inasikitisha sana kuona mbunge amepanda juu ya gari huku amelala gari linakwenda mwendo kasi huku wafuasi wake wanashangilia.

Sijui Wananchi na wa kazi wa Arusha wanaitaji nini kutoka kwa Lema.
 
Ahsante. umekuja na barabara. wengine wekeni mengine basi.

asante..kikubwa zaidi ni kwamba lema amejenga confidence na morali ya hali ya juu kwa vijana..na kwa sasa polisi wamekuwa na nidhamu kwa raia.. hata wamama wa sokoni wana sauti siku hizi kwa sababu wamefunguka na kujitambua..
 
Kitu ambacho ni kigumu kukielewa ni siasa za Lema pamoja na wafuasi wake wa Arusha.
Inasikitisha sana kuona mbunge amepanda juu ya gari huku amelala gari linakwenda mwendo kasi huku wafuasi wake wanashangilia.
Sijui Wananchi na wa kazi wa Arusha wanaitaji nini kutoka kwa Lema.
umeanza kuhatibikiwa nilikuwa nakuamini sana ngja nikuvumilie kidogo labda umepost hii kwa bahati mbaya tu
 
Mkuu umeongea point sana . Kwakweli hali mbaya sana hasa upande wa barabara na ajira kwa vijana . Nafikiri 2015 tutajua chakufanya.

Lazima muwe waelewa,sio kila kitu mpaka mtafuniwe ndio muelewe,vichwa mmejaza mawe au?tatizo la ajira na barabara ni janga la taifa,na si Arusha peke yake,ya kulaumiwa ni serikali ambae ndie mtunga sera na mtekelezaji wa wa maendeleo ya majimbo yote nchini!lazima muelewe majukumu ya mbunge na wajibu wa serikali,jinsi mnavyomlaumu Lema mnaonyesha wazi mna chuki nae binafsi,na mmekua wavivu kwenye vichwa vyenu kuahinisha wajibu wa mbunge na wajibu wa serikali!msiwe wavivu wa kufikiri,mtashindwa jiletea maendeleo hata yenu binafsi
 
hebu tuambie kwanza utandaji kazi bora ya hao wabunge wa ccm unaowaona wanafanya kazi nzuri kuliko Lema?
Mada yako inaonyesha wazi wazi chuki binafsi na Lema

tatizo lenu wanachama wa cdm huwa hampendwi kuguswa !
Angekuwa wa ccm hapo page ingekuwa inahamia ya 15. Tengenezeni ushawishi ndio jamaa aone hajaweka swali la msng !
Sio kukimbilia kusema umekaa kimagambamagamba.
 
Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha

KAKA/DADA MKUBWA NADHANI KABLA HUJAANZA KULETE UMBEA WAKO HUMU JAMVINI UNGEJIULIZA CCM YENU IMETULETEA NINI KWA MIAKA YOTE HIYO?
 
Hii nchi demokrasia na haki sawa itatoka wapi?? Ikiwa mtu kama Mkapa anatuambia tusipomchagua mbunge wa ccm tusahau maendeleo na mabadiliko demokrasia iko wapi? Ni neno baya na tusi na udhalilishaji kumwambia mtu haki yako nitakupatia baada ya kukulawiti, ndicho wanachofanya ccm, na serikali yao, kutulaghai tuchague tunayemtaka then wanasema hatupati pesa, sielewi.
 
asante..kikubwa zaidi ni kwamba lema amejenga confidence na morali ya hali ya juu kwa vijana..na kwa sasa polisi wamekuwa na nidhamu kwa raia.. hata wamama wa sokoni wana sauti siku hizi kwa sababu wamefunguka na kujitambua..

Mkuu hao unaowafafanulia unafikiri hata wanaelewa ilo?bado wanahitaji shule sana waweze kujitambua na kutambua haki zao
 
tatizo lenu wanachama wa cdm huwa hampendwi kuguswa !
Angekuwa wa ccm hapo page ingekuwa inahamia ya 15. Tengenezeni ushawishi ndio jamaa aone hajaweka swali la msng !
Sio kukimbilia kusema umekaa kimagambamagamba.

Mkuu umepitia hoja zote za watu na ukaona kua mleta mada hajajibiwa hoja yake??japo mleta mada sidhani kama ana uhakika na kile alichokusudia kumkosoa Lema!maana inaonyesha wazi uwezo wake wa kujua wajibu wa mbunge na majukumu ya serikali ni zero
 
Back
Top Bottom