Arusha - Je tunaridhika na utendaji wa Godbless Lema?

tukiwa ni wakazi wa arusha tunakubaliana kwamba arusha ni ngome ya cdm. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa taifa. Lakini ndilo jiji pekee tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na lema ametimiza mangapi.
2.majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.je? Tukimlinganisha lema na felix mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya arusha?
4.je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
Naomba kuwakilisha

mbona hoja zako hazijajitosholeza moja umeshindwa kuonesha wazi ni kwa vp lema siyo aina ya mbunge anayehitajika either kwa kutuonesha sifa za mbunge ambaye tunamuhitaji pamoja na sifa alizonazo lema ambazo zinamtofautisha na aina ya mbunge ambaye tunamuhitaji.
Mbili umeshindwa kuweka wazi data ulizonazo juu ya utendaji wa lema ukilinganisha na data za utendaji za mbunge anayehitajika.
Tatu umeshindwa kuthibitisha uwezo wa kusimamia ahadi alizoahidi lema ukilinganisha na mbunge unayemuhitaji umeshindwa kuwathibitishi wana jf mbunge bora ni yupi badala yake umetuachi home work tukufanyie hatuwezi kuwa taifa la majungu tofauti zetu za kiitikadi zisifanye tuhukumu hata pasipo hukumika umeona wapi lema amesema anaenda polisi ili kusudi apate kura za huruma kutoka kwa wananchi je ni mara ngapi lema ameenda polisi? Je waraka aliouandika kipindi yuko mahabusu pamoja na sababu zake uliusoma?
 
aah kaka maisha hayaendi hivo bana! hili ni jamvi la weledi. maswali yako wazi na ni vizuri ukitoa hoja kuliko kuwa mkali tu. hata hivyo kama wewe sio mkazi wa jimbo la Arusha hili halikuhusu maana huna cha kujibu. waachie basi wanaoishi Arusha wajibu kulingana na muono wao.

Unaoneje ukiwaomba mods wakutengenezee jukwaa la wanaArusha make hata wewe unaonesha ukali na kukeleka na mchangiaji huyo!
 
Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha

utatawaliwa mpaka na vitukuu vya kina Sumari.
 
Mimi na mke wangu na watoto wangu tunakubari Lema kwa asilimia mia,LEMA kazidi kutupa ujasiri na leo hii hakuna mtu wa Arusha anayeonewa na serikali legelege ya CCM,Vilevile barabara zinajengwa kwa hiyo kwetu Mh Lema ni kila kitu.
 
Kuna mtu mmoja hapa naungana naye mkono kua endapo Lema angepewa ushirikiano basi jiji hili letu la Arusha tungekua mbali! Ni kweli kabisa lakini pamoja na Lema kutopewa ushirikiano katika kuleta maendeleo lakini tumeshayaona kama PJ alivyoeleweka na ukitaka kujua kwamba serikali ya ccm haipendi maendeleo angalia tokea utawala wa mbunge KINANA hakuna kilichobadilika Arusha, hususani mbunge Felix Mrema hali ni ileile! Ni bora tubaki na huyu kama mnavyomuita eti ni mvuta bangi pamoja na kumkwamisha huko lakini je tujiulize iweje sasa hivi ndio tuaona hali ya mabadiliko jiji la Arusha???

Apewe ushirikiano na nani? kwani nani anampa ushirikiano zitto?
 
tunaikomboa kwanza nchi ndio tuanze kuijenga. haijalishi kuwa nafanya nini kwa Arusha nashukuru kuwa umeainisha kuwa yuko bise, ndio ujue yuko bise na harakati za ukombozi. kwani hao wabunge wa ccm waliotuongoza kwa kipindi chote hicho unaridhika na mambo waliyoyafanya au ilitakiwa wawe wamefanya zaidi?
pia unapolalamimi kuhusu barabara wakati unakiri kuwa uko Arusha unakuwa muongo tembelea maeneo ya katikati ya mji uone jinsi barabara nyingi zimefungwa na wamekwisha anza kuchimba na kuja na kushindilia tayari kwa kuwekwa lami nafikiri ni mwanzo mzuri.
hata kama meya ni wa ccm lakini naamini katika vikao vyao sasahivi ufisadi wa miradi ya manispaa utapungua kwa kiwango kikubwa sana maana wako kina lema ndani ambao watafichua uovu wote wa miradi ya kifisadi ndani ya manispaa ndio maana walikuwa wanataka kufanya ule mradi wa kaloleni kwa nguvu na siri ili lema asijue maana una ufisadi ndani yake na ole wao wao sasahivi walete miradi yao ya kifisadi lazima itawekwa hadharini tu.
nafikiri sio lazima tumwone mbunge akija kusimama na jembe au fagio barabarani ndio tuseme anawajibika hata pinda kuna wakati alienda kupiga picha kwenye shamba lake akijifanya eti ni mkulima hakuna kitu hii biashara ya kukusanya waandishi wa habari na kuwapa posho wakupige picha eti uko unashiriki shughuli za maendeleo kama kupanda miti wakati unakuta ni mti mmoja tu umepanda na mingine imepandwa na wananchi hapo kwa lema hakuna.
lema na chadema kwa ujumla wamekuwa akiwafungua watanzania maskio na macho juu ya ufisadi unaoendelea na baada ya kuamka na kupambana ndipo sasa fedha tutakazoziokoa zitaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo.
Huwezi kutegemea kupata maji mengi mwisho wa bomba linalovuja, ili uweze kupata maji ya kutosha ni lazima uzibe sehemu zilizotoboka ndipo upate maji uanze kunyeshea kwahiyo kinachofanbyika sasa ni kuziba mianya yote ya uvujaji wa fedha za umma na ndiposa zielekezwe kwenye miradi ya maendeleo
 
We umetumwa na magamba suala la mpango mji wa arusha limetokana na uzembe wa viongozi wa ccm, pili yeye kama mbunge hawezi kukubali wananchi wake wavunjiwe nyumba kwa ajili ya upanuzi wa barabara bila fidia inayoendana na gharama za maisha sasa, japo uwajibikaji unaonekana. Ajira za kiuwaji katika mashamba ya maua mliyapora kwa wananchi enzi za wabunge wa ccm mbona huongelei??
 
Kitu ambacho ni kigumu kukielewa ni siasa za Lema pamoja na wafuasi wake wa Arusha.

Inasikitisha sana kuona mbunge amepanda juu ya gari huku amelala gari linakwenda mwendo kasi huku wafuasi wake wanashangilia.

Sijui Wananchi na wa kazi wa Arusha wanaitaji nini kutoka kwa Lema.

Nashindwa hata kukoment, nabaki kucheka kwa jinsi ulivyopinda kijana!

 
Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha

Natambua unajua msuguano wa kisiasa uliopo ndani ya Ar. Kama kweli wewe mpenda maendeleo wa jiji la Arusha nilitegemea ungeuliza tufanye nini ili kumsaidia mbunge wetu pamoja na uongozi wa mkoa ili tutatue matatizo ya Ar yetu.
 
Heshima kwenu wakuu.

Muanzisha hoja kauliza maswali mazuri bahati mbaya hajui siasa za JF unapotoa taarifa zenye mtazamo mbaya kuhusiana na kiongozi wa CDM.

Kwanza unatakiwa ujue kazi na wajibu wa mbunge.

Pili unatakiwa ujue pia kazi za mbunge wa upinzani.

Ndugu yangu mpingauonevu Mheshimiwa Lema ni mbunge wa upinzani.Madhaifu yote unayoyaona katika mji wa Arusha yanastahili kuelekezwa CCM kwasababu CCM inaendesha halmashauri ya jiji la Arusha,CCM inaendesha serekali kuu na serekali za mitaa.Ujenzi wa mabarabara unaouona katika mji wa Arusha hauna uhusiano wowote na Mheshimwa Lema,Uchafu uliozagaa katika jiji la Arusha hauna uhusiano wowote na Mheshimiwa Lema.Ikumbukwe CDM ina madiwani wachache sana baada ya kuwatimua madiwani wake na kuiacha CCM ikatamba katika halamashauri ya Jiji la Arusha.

Ni makosa makubwa sana kusema ujenzi wa barabara katika Jiji la Arusha ni kazi ya Lema.Ujenzi wa barabara ni matokeo ya mpago wa serekali kuu wa kuboresha barabara katika majiji yote Tanzania bara mpango huo unafadhiliwa na world bank na ulikubaliwa kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010 unachokiona sasa ni utekelezaji.
 
Heshima kwenu wakuu.

Muanzisha hoja kauliza maswali mazuri bahati mbaya hajui siasa za JF unapotoa taarifa zenye mtazamo mbaya kuhusiana na kiongozi wa CDM.

Kwanza unatakiwa ujue kazi na wajibu wa mbunge.

Pili unatakiwa ujue pia kazi za mbunge wa upinzani.

Ndugu yangu mpingauonevu Mheshimiwa Lema ni mbunge wa upinzani.Madhaifu yote unayoyaona katika mji wa Arusha yanastahili kuelekezwa CCM kwasababu CCM inaendesha halmashauri ya jiji la Arusha,CCM inaendesha serekali kuu na serekali za mitaa.Ujenzi wa mabarabara unaouona katika mji wa Arusha hauna uhusiano wowote na Mheshimwa Lema,Uchafu uliozagaa katika jiji la Arusha hauna uhusiano wowote na Mheshimiwa Lema.Ikumbukwe CDM ina madiwani wachache sana baada ya kuwatimua madiwani wake na kuiacha CCM ikatamba katika halamashauri ya Jiji la Arusha.

Ni makosa makubwa sana kusema ujenzi wa barabara katika Jiji la Arusha ni kazi ya Lema.Ujenzi wa barabara ni matokeo ya mpago wa serekali kuu wa kuboresha barabara katika majiji yote Tanzania bara mpango huo unafadhiliwa na world bank na ulikubaliwa kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010 unachokiona sasa ni utekelezaji.
Habari,
Ningeshangaa kama nisingekuona kwenye thread inayo mhusu lema hasa inaolenga mabaya ya lema, lakini nikupongeze kwani nimeona leo uko fair kiasi furani....
kwani binafsi na weza ujenzi wa barabara unaweza kuhusisha na lema....tuchukulie ile barabara ya kule njiro pesa yake ilishatolea miaka minne iliyo pita lakini tujiulize kwanini haikujengwa siku zote kwanini sasa....upanuzi wa barabara hapa hapa mjini /mbauda ni issue ya siku nyingi sana lakini baada ya upinzani tunaona harakati za ujenzi zikipamba moto.....nikuhakikishie tu kuwa ccm wako makini sana na utumiaji wa pesa za halimashauri ya arusha wakijua siku yoyote wanaweza kungoka pale na mabaa yataanikwa...
 
Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha
Morani wa kimeru mnaomlinda kaeni sawa yako majasusi wa magamba kama hili yanamtafuta mbunge wetu. Tumewakabithi ulinzi wote mkipata yeyote hata awe nani %&^*a *&a tutawalinda kisheria.
 
Apewe ushirikiano na nani? kwani nani anampa ushirikiano zitto?

Je unataka kufahamu au unataka kubishana....kama unataka kufahamu ni hivi mipango yote huanzia ngazi ya serikali za mitaa yaani kuanzia mwenye viti wa vitongoji linaenda kwa madiwani ambamo kimsingi lema, zitto na wabunge wengine wanaingia kwenye baraza la madiwani... sasa diwani au mbunge anaeza kuwa na nia njema kwenye mtaa au kijiji akakwamishwa na wenyeviti mfano diwani wa Elerai alikuja na pendekezo la sehemu moja iliyokuwa imetengwa kuwa soko wajenge dispensary lakini kwa mshango wa wengi kwa kuwa kwenye kampeni zake ali ahidi hilo na kwa kuwa wenyeviti walio wengi ni CCM wali mkwamisha na kuamua kujenga ofisi za kata badala ya dispensary......hizo ndizo siasa za arusha kwa sasa yaani za kukomoana....yaani kiongozi wa serikali ana fanya jambo ili watu wenye mtindio wa ubongo kama kama wewe waseme chadema hawaja fanya kitu....
 
Kinachokuhusu wewe ni kipi hasa?

Tukiwa ni wakazi wa Arusha tunakubaliana kwamba Arusha ni ngome ya CDM. Arusha ni jiji ambalo linaingiza pato la kutosha kwa Taifa. Lakini ndilo jiji pekee Tanzania ambalo halipangiki, halina barabara na wala haijulikani mpango wake wa kesho ni nini. Lakini kwa Mbunge wetu tunaona yuko busy na matukio yatakayomfanya awekwe ndani na polisi ili apate kura za huruma. Swali la kujiuliza
1. Majukumu ya mbunge ni yapi na Lema ametimiza mangapi.
2.Majukumu ya madiwani ni yapi na mbunge amewahamasisha madiwani wake kwa mangapi?
3.Je? tukimlinganisha Lema na Felix Mrema nani atakuwa amefanya mengi kwa maendeleo ya Arusha?
4.Je? Lema ndiye aina ya mbunge tunayemuhitaji?
naomba kuwakilisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom