Arusha imekuzwa kuliko ilivyo!! ( Overrated )

Arusha imekuzwa kuliko ilivyo!! ( Overrated )

Dk Mpango aliitaja mikoa mitano yenye ahueni ya umaskini wa kipato kuwa ni Dar es Salaam (5.2), Kilimanjaro (14.3), Arusha (14.7), Pwani (14.7) na Manyara (18.3).
Nafikiri wale wanaosema Dar maisha magumu inabidi waache sasa kubana pua. Hio ripoti inaonesha Dar ndio kuna kiwango kidogo cha umaskini asilimia 5.2. Wa pili klm asilimia 14.3 kuna tofauti karibia asilimia 10 nzima.
 
Wanabodi habari zenu
Nilikuwa sijawahi kufika Arusha, tangu nikiwa sekondari mpaka chuo nimesoma na machalii mbalimbali toka mkoa huo wa Arusha, wamekuwa wanapasifia sana kama si mno.

Hata wadau mbalimbali waliowahi kufika wamekuwa wanapasifia sana ni pazuri na pamejengeka vizuri hata kufikia hadhi ya kuitwa " Geneva of Africa ". Pia uwepo wa makao makuu ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, uwepo wa machimbo ya madini na sekta ya utalii imechangia sifa za Jiji hilo la Arusha kuzagaa mikoa mingine hali inayofanya kila mtu atamani kufika Arusha akiamini ni pazuri kama alivyohadithiwa.

Mungu si Athumani, nikapata safari ya kwenda Arusha wiki iliyopita, MAMA YANGU!! Sikuamini macho yangu, ni sehemu moja ya kawaida sana tena sana. Kwanza hapo wanapopaita Mjini ni pa kishamba sana, Stand ya mabasi ni kawaida yaani hata stand ya daladala ya Mbezi ni nzuri.
Majengo yenyewe ni ya kuhesabu hapo katikati ya mji.

Nikaingia sasa maeneo kama Sakina, Moshono, Njiro pakawaida sana, nikaamini mkoa ni mkoa tu!! Jiji kama lile kuna hiace zile fupi ndio zimejaa mpaka kero, huko Ngaramtoni kuna vumbi ambalo sijawahi kuliona kabisa. Bei ya vitu ndio usiseme yaani kitu cha kuuzwa elfu 5 utaambiwa elfu 30. Hata viwanja vya kijanja vya kujirusha Arusha ni vya kuhesabu na ushamba mwingi sana.

Kitu pekee cha kujipongeza na kujisifu kwa watu wa Arusha ni uwepo wa mbuzi choma kwa Mrombo, baasi hiko ndio nimeona tu!! Kwa maneno mengine Arusha ni overrated region.

Hujitambui wewe gebwe.
 
Arusha hela ngumu kupatikana halafu bidhaa zipo juu mno nakumbuka mwaka jana nilienda kwenye msiba nilipofika nikaona kutembea tembea mtaani na raba muda wote sijazoe ikabidi nimwambie mwenyeji anipeleke sehemu nikanunue sandals akinipeleka kwenye soko flan hivi local aisee kuuliza bei naambiwa 45k wakati quality ileile hapa mjini dar unaipata kwa 15k hahaha hela nilikuwa nayo lakini ikabidi nighairishe zoezi moyoni nikasema kwa hizo bei mtawakamata haohao wa arusha
Tunauwezo wa kununua ndo mana tunakamatwa.siku nyingine uje na hela za kutosha,mana inaonekana ungenunua hizo raba ungeomba lift kurudi kwenu
 
Alichokiandika mleta mada ni kitu cha ukweli kabisa....isipokuwa tu ni ubishani wa mtu kwao.....

Kabla ya hujafika Arusha unajenga picha kubwa sana ya jijj la Arusha lakini ukifika huko unarudi na picha ndogo sana ya mkoa wa Arusha.....
Mkuu umemaliza kila kitu kilichobaki ni ubishi kwa wazawa wa huko.
 
Hua nashangaa sana mtu analazimisha kua masikio yanatoa makamasi wakati anajua pua ndio inatoa.Kama Mkoa wako ni wa ovyo usijipooze kwa kulazimisha mikoa mingine hiwe kama wako.
 
Hayo ni mapenzi yako hakuna anaekuzuia, kwa Tz Arusha na moshi ni mikoa isiyonivutia kabisa kuishi, labda mikoa ya Iringa mbeya na Dar tu
Wanging'ombe?? Hahahaaa kuna mtu anafananisha Arusha na Iringa na Mbeya kweli mmetoboka.
 
Arusha kuna vitu ving vizur kuliko mwanza...but mwanza kuna harakat shaz kuliko chuga....msukumo wa biashara ni mkubwa sana mwanza...mbeya ndo hamna kabisa
 
Nimezaliwa arusha, nimetembea majiji yote ya afrika mashariki, kiuhalisia majiji haswa ni nairob na dar, haya mengine yoote, mombasa, mwanza, ars, kisumu, hamna tofaut kabisa, kampala naweza ilinganisha na mombasa , arush inaongelewa sana kwa sababu za kitalii, diplomacy, tanzanite na vingine na ndio kinachoifanya watu kudhan ni pa kipekee na tofauti sana but ni sawa na miji mingine inayokuwa, hamna cha mwanza wala nini kote hamna jiji!
Asante!!
 
Hahaa, ulitakaje kwani?!
Huku ni mkoani tuachie jiji letu wenyeji ndio twajua uzuri na utamu wake!!
Bakia huko unakokuona pamekucha maana huo ndio mtazamo wako! Hata hapo unapopaona pamekucha ni pa kishamba tu kwa wengine!!
We call it " Povu "
 
Na walioukuza zitakuwa haziwatoshi nadhani!

Clinton Bill ndio aliyetoa nickname ya Arusha kuwa ni Geneva of Africa!! Tafakari...!

Kwa Tanzania ni Arusha na Moshi tu ndio mikoa inayonivutia kuishi au kuweka makazi!!
Wachagga katika ubora wenu
 
non sense........ afuu next tym uje na mkwanja wa kufika adii ngurdoto sio kuishia kwa morombo........ usituletee umaskini wako uku
 
Back
Top Bottom