Tatizo sio uwanja kuna je kuna facilities za kutosha? Kuna mahoteli? Kuna kampuni za utalii? Arusha kuna hotel nyingi, farm rest houses zakutosha kiasi kwamba itachukua almost 5 years Mwanza kuwa na facilities hizo.
Pia usfkiri watalii wanakuja Tanzania kwenda Serengeti tu, kwa taarifa yako Ngorongoro Crater ndo inapata wageni wengi na ni karibu na Arusha. Mgeni akianzia Arusha atapata nafasi ya kutembelea Ngorongoro, Tarangire, Manyara Arusha National Park, Mt Meru, Kilinanjaro, na Oldonyo Lengai na vivutio vingi njiani hadi kufika Serengeti kwa hiyo kufkiria uwanja wa ndege Mwanza utapunguza wageni Arusha ni ndoto. Hapo sijaongelea sababu za kijamii mfano pia kuna wazungu wengi ambao ni wakazi wa Arusha ambao pia huvuta wageni
Sent using
Jamii Forums mobile app