Arusha hakuna ukarimu kwa wateja

Arusha hakuna ukarimu kwa wateja

Ukiongelea Dar es salaam unaongelea pwani ya Swahili,Ni mojawapo ya sehemu ulipoanzia ustaarabu.Kuhusu huko kwingine sidhani kama ustaarabu umewapitia karibu wao wanachojali ni pesa tu.
 
Nenda Iringa utasikitika na kucheka at the same time,

unaingia kwenye duka la nguo muuzaji kakaa nje anakutazama unavyoingia, unamuita akuuzie anakutajia bei akiwa hapo-hapo nje tena kanuna balaa inabidi ujiondokee zako.
 
Arusha kuna influence kubwa sana ya nairobi kutokana na ukaribu wa miji hii miwili.
ni kweli kuna ukaribu lakini kwenye medani za customer care kuna umbali mkubwa sana hata baadhi ya sekta walizoajiriwa wakenya ndani ya arusha ukiingia utaona utofauti mkubwa na wengine ambao wako tofauti katika care ya mteja ni wahindi waliopo hapo ukiingia kwenye biashara zao ni wakarimu kwa wateja
 
Arusha ni pasua kichwa!!! ukitaka kuamini arusha nuksi ulizia bei ya kitu halafu usinunue!! utapewa msonyo wa hatari!!!
 
Kwasis ambao tumezaliwa Arusha tunaona n Sawa lakin nyie wakuja lazma mtaona tofaut ,hata hivo nakubaliana na mtoa Mada
 
Hiyo ni fursa, fungua na wewe biashara uonyeshe hiyo hospitality unayoisemea upige pesa.
 
Nenda Iringa utasikitika na kucheka at the same time,

unaingia kwenye duka la nguo muuzaji kakaa nje anakutazama unavyoingia, unamuita akuuzie anakutajia bei akiwa hapo-hapo nje tena kanuna balaa inabidi ujiondokee zako.
Umenitangulia kaka.Nilitaka kumwambia aje Iringa akutane na kuburi cha wahehe.Umeenda dukani na 10,000/= unataka kitu cha 4,000/= utamsikia muuzaji anakujibu bee hugo guchenji mi sina jiendeage tu.
 
Jamaa amesema haoneagi mtu, na jamaa ni CDM kabisa huyu ila kaamua kuwaambia wenzake ukweli tu. Hivyo kuna ka ukweli flani ktk malalamiko yake

Naishi Arusha, haya ni ya ukweli kabisa, Dar kwenye migahawa wapo fresh sana, sana sana, mara wakuite bocy, watabasamu, wakuulize etc, Arusha? NO WAY, sehemu nyingi hiyo hakuna, Ila HOTEL Kubwa ukaribu upo wa training! Kuna ukaribu wa utamadumi, na mazingira na wa Darasani, Dar mnao social, utamaduni na proffesional, ndivyo mlivyoumbwa
 
Tatizoo wafanya biashara wakishafanikiwaa kidogo tu.....washalizikaaaa huku
 
Malingumu
Ama kweli katika mji wa vipofu mwenye chongo ni mfalme. Mkuu we sina uhakika kama umeshatoka nje ya nchi ila kwa wakaa nje ya Tanzania sidhani kama kushambulia baadhi ya maeneo ya Tanzania kwa poor hospitality ni halali. Mkuu ukitoka nje ukaingia Tanzania ndo utajua maana yake . Ki ujumla kama nchi hili eneo ni muhimu litendewe haki tunahitaji kubadirika kama kweli tuna mpango wa kujiandaa kuukabiri ushindani tuko verypoor eneo hili
 
Wakati nasoma shule pale Ilboru kuna siku (weekend) tulienda kutembea mjini, basi tukazungukaa mpaka tukafika mitaa ya Kilombero kuna mitaa wanauza viatu.
Tukafika kwa jamaa mmoja hivi alivalia kibishoo, mwenzetu mmoja akaulizia bei ya kiatu alichokipenda, yule muuzaji akajibu "madogo nyie piata tu, hivi viatu hamuwezi bei yake" daah yule mwenzetu kumbe yuko vizuri mfukoni akamwambia ninaweza kununua vitu vyote hapa, acha dharau, taja bei. Muuzaji kataja bei mwenzetu akamwambia hiyo bei haifikii hichi nilichova....

Jamaa wengine wanadharau aisee
Mkuu umenikumbushia mbali, Ilboru ulimaliza mwaka gani?
 
Mtoa Uzi amenigusa kweli kweli nimekaa sana mikoa ya Tanzania na jirani zetu K ,kweli hapa Arusha mteja hana thamani kabisa unaenda hotel I ya kawaida kabisa muhudumu anakuja amekunja uso na hana ukarimu wowote ukitaka kulipa mpaka upige miluzi kumwita muhudu ili ulipe bill yako .hawana menu list kwenye meza ukiuliza kuna nn wanaataja wali ugali nayama kuku mchuzi machalari na mengineyo halo sasa kama computer yako haishiki unaachwa unashanga tu.
 
Back
Top Bottom