Arusha hakuna ukarimu kwa wateja

Malingumu

JF-Expert Member
Apr 5, 2012
616
429
Habarini wana wa nchi wenzangu,

Naomba leo nishee jambo kidogo kuhusu hili jiji la Arusha.

Ni takribani mwaka sasa nimekuwa katika jiji hili la Arusha kikazi, kabla ya hapo nilikuwa naishi Dar. Waswahili husema "mteja ni mfalme", hii kauli nahisi inatofautiana katika viwango vya kuthibitika kati ya eneo ya eneo.

Niwe specific kidogo kwamba hapa nazungumzia hasa maisha ya chini na ya kati, yale ya juu ya kwenda hotels za nyota 5 huko sinazo sana taarifa zake. So hapa ni kwa maeneo ambayo nimekuwa nikienda sana( mama ntilie, muuza mihogo, migahawa ya kwaida, pubs, vioski, duka la bidhaa za vyakula, ETC)

Ni hivi kwa kipindi hiki cha mwaka mmoja nilichokaa nimegundua kuwa kuna utofauti mkubwa kati ya maeneo niliyowahi ishi say Dar es Salaam na huku katika ukarimu kwa wateja.

Mara nyingi ukienda sehemu ama kununua bidhaa au kupata huduma thamani yako huonekana ndogo, sijajua hawa wauzaji huwa wanawaza nini, lakini unaweza enda dukani au mahali upate kinywaji lakini hata karibu huipati, yani neno karibu limekuwa gumu kwa watoa bidhaa wengi wa huku, sijajua wakilitamka linawapunguzia nini.

It happened zaidi ya mara 8 kwamba nimeenda katika mgahawa nipate chakula lakini badala ya mtoa huduma anikaribie na kunisikiliza mimi nimekuwa ndiyo wa kumkaribia mtoa huduma na kumwambia kuwa nataka huduma gani(hayupo bize wakati huo) sidhani hata kidogo kama hili ni sawa.

Kiukweli iliponitokea siku za mwanzo nilifikiri ni baadhi au wachache tu wako hivyo ila kadiri siku zilivyosonga nikaja gundua asilimia kubwa ya wafanya biashara huku Arusha hawana ukarimu kwa wateja wao, iwe ni duka la bidhaa za kawaida, pubs, vioski, migahawa au pengine ni nadra sana kukarimiwa kama mteja (poor hospitality).

Najua wengine mnaweza pinga ila mimi sioneagi mtu kama wale wengine nimejaribu kuwaambia kile ambacho kwa sehemu nimeona kipo huku Arusha.

Ndugu zangu wana Dar es Salama nawamisi sana kwa ukarimu wenu wa biashara, huku mambo ni tofauti kabisa.

Haki Mungu hakupi vyote watu wa Arusha kuna vitu wamejaliwa lakini pia kuna vitu hawana, hiki ni kimojawapo kati ya vile wasiokuwa navyo.

KAMA WATANZANIA KUNA MAMBO YAPASWA TUAMBIANE ILI TUREKEBISHANE, VINGINEVYO TUTAPIGWA BAO SANA KIBIASHARA NA MAJIRANI ZETU NA UKIANGALIA WAKUBWA WASHADONDOSHA SAHIHI KWENYE FREE TRADE AREA YA AFRICA.

DONE
 
Arusha ni pesa tu ndio muhimu, huwa wananishangaa nikienda dukani nikimaliza kununua nasema ahsante, unaonekana muungwana kuliko, karibu kwa huku sahau hata huende hotel kubwa kwanza hizo kubwa nyingi ni self service hata salamu ya muhudumu hutoipata labda wewe uamue kuweka ukaribu nae, hata ile sijui punguzo dukani Arusha hii wewr mteja ndio ujishushe uonekana kweli hela huna ndio bei ishuke sio muuzaji hili jiji hili halina maana kabisa, endelea kukaa zaidi utaona mengi sana huo utangulizi tu haaaa haaa
 
Hao si wafugaji wanyama na asli ya mfugaji ana adopt tabia za wanyama awafugao pià hata kuishi porini kwa muda wa miaka mingi pia kizazi hadi kizai kina copy hiyo ingawa sasa ivi ni mji mkubwa kimuonekano na kibisshara tofauti na uku pwani,mkuu vumilia tu ndo tabia zao hoa,
 
Tatizo lako umeenda seheem iliyo busy wateja wengi sehem kama hizo popote pale huduma huwa ivyo hata stendi kipindi cha december unaingia had ndani hakuna mtu anakuuliza unaenda wapi
 
kuna siku nilienda kwenye mgahawa.sio huko arusha.
nimekaa kwenye kiti.
wahudumu wananiangalia tu.
na Mimi nikatulia kimya kama dakika tano.
nikaamua kuondoka.
NIKAJISEMEA KIMOYO MOYO.
huu mgahawa hautadumu.
mbona WALIKUJA KUUFUNGA..
biashara yoyote ukimdharau tu mteja.
jua utaanguka.
 
arusha ukarimu niliuona kwenye mgahawa wa warabu/wahindi sikumbuki vizuri ila wabongo sasa duh

kwenye maduka ya simu vikevile ukijifanya mchaguaji sana utapewa kauli ambayo utatamani utukane tusi zito kwa kireno ila basi tu...
 
Wakati nasoma shule pale Ilboru kuna siku (weekend) tulienda kutembea mjini, basi tukazungukaa mpaka tukafika mitaa ya Kilombero kuna mitaa wanauza viatu.

Tukafika kwa jamaa mmoja hivi alivalia kibishoo, mwenzetu mmoja akaulizia bei ya kiatu alichokipenda, yule muuzaji akajibu "madogo nyie piata tu, hivi viatu hamuwezi bei yake" daah yule mwenzetu kumbe yuko vizuri mfukoni akamwambia ninaweza kununua vitu vyote hapa, acha dharau, taja bei. Muuzaji kataja bei mwenzetu akamwambia hiyo bei haifikii hichi nilichova....

Jamaa wengine wanadharau aisee
 
Wakati nasoma shule pale Ilboru kuna siku (weekend) tulienda kutembea mjini, basi tukazungukaa mpaka tukafika mitaa ya Kilombero kuna mitaa wanauza viatu.
Tukafika kwa jamaa mmoja hivi alivalia kibishoo, mwenzetu mmoja akaulizia bei ya kiatu alichokipenda, yule muuzaji akajibu "madogo nyie piata tu, hivi viatu hamuwezi bei yake" daah yule mwenzetu kumbe yuko vizuri mfukoni akamwambia ninaweza kununua vitu vyote hapa, acha dharau, taja bei. Muuzaji kataja bei mwenzetu akamwambia hiyo bei haifikii hichi nilichova....

Jamaa wengine wanadharau aisee
safi sana. niliona pia clip moja ya mchina alienda kubadilisha simu yake ya iphone kwasabb ilileta hitilafu muuzaji akamzinguaaaaa

jamaa akawaambia kurudisha simu hapa haimaanishi sinauwezo wa kununua nyingine. Akasepa baadae akarudi na burungutu la hela akanunua simu zote mle na pesa ikabaki alicho fanya simu alizo nunua akazivunja palepale na nyundo aliokuja nayo meza zote za kioo za kuuzia simu akavunja vunja na kulikua na desktop ya mac

nayo ikala nyundo kisha akawaachia pesa akaoanda zake kwenye gari la kifahari akaondoka
 
Nazani unaiongelea Zanzibar kwa Arusha big NO! Nakubali chache hazikosekani na labda bahati yako mbaya ukawa unatembelea hizo sehemu zenye huduma mbaya..

Lakin Arusha ni sehemu yenye huduma nzuri, wachakarikaji wengi, ushindani ni mkubwa wa biashara.So kila mtu anajitahidi kutoa huduma bora ili kuwavutia wateja wengi.

Pia sehem nzuri zenye huduma na bidhaa bora zinajulikana usijiendee tu sehem ni sehem.ova
 
Jamii za kifugaji nyingi sio wakarimu...
Sijafika Arusha ila huko naona ndio wamezidi.
Naendaga Musoma ni Tofauti kabisa na Masasi , yani ukienda masasi utatamani ukae huko moja kwa moja.. wana ukarimu sana...

Wengine wanyakyusa nmechangamana nao sana huku nnakoishi sijui huko kwao.. jamani ni wakarimu mnyakyusa ukimpa kitu hio asante yake mpaka unaweza kulia.
 
Eroo maeneo hayafanani, ustaarabu no asili ya watu wa pwani hasa, arusha imeathirika na Nairobi. Na haya hapo kuna idadi kubwa ya wakenya so tabia nyingi za wabongo zimemezwa na wakenya.

Kakangu anaduka hapo na huwa nakaa hapo wakati mwingine, yeye mtu akimwambia asantee baada ya kumhudumia anaweza kumjibu shit au wakati anataka kununua akimwambia naomba kitu Fulani atamjibu cha kuomba hakuna kipo cha kuuza.
Una haja ya kuwazoea, ndivyo walivyo ndugu zako hao.
 
Hao jamaa wa Arusha wanawaza pesa tu hapo hata ukimuuliza mtu njia ya kwenda kituo cha mabasi hana mda na wewe mda wote vichwani kumejaa pesaaa pesaa
 
safi sana. niliona pia clip moja ya mchina alienda kubadilisha simu yake ya iphone kwasabb ilileta hitilafu muuzaji akamzinguaaaaa

jamaa akawaambia kurudisha simu hapa haimaanishi sinauwezo wa kununua nyingine. Akasepa baadae akarudi na burungutu la hela akanunua simu zote mle na pesa ikabaki alicho fanya simu alizo nunua akazivunja palepale na nyundo aliokuja nayo meza zote za kioo za kuuzia simu akavunja vunja na kulikua na desktop ya mac

nayo ikala nyundo kisha akawaachia pesa akaoanda zake kwenye gari la kifahari akaondoka
Ni wapi,arusha au?
 
Back
Top Bottom