Arusha hakuna ukarimu kwa wateja

Arusha hakuna ukarimu kwa wateja

Hao wana tabia za wakenya,ukisema naomba kitu fulani wanadhani unaomba bure,kumbe ndo lugha ya watz walio wengi
 
Nazani unaiongelea Zanzibar kwa Arusha big NO! Nakubali chache hazikosekani na labda bahati yako mbaya ukawa unatembelea hizo sehemu zenye huduma mbaya..

Lakin Arusha ni sehemu yenye huduma nzuri, wachakarikaji wengi, ushindani ni mkubwa wa biashara.So kila mtu anajitahidi kutoa huduma bora ili kuwavutia wateja wengi.

Pia sehem nzuri zenye huduma na bidhaa bora zinajulikana usijiendee tu sehem ni sehem.ova
Huijui chuga wewe.
 
umefika iringa mkuu? Kule unauliza shati sh ngapi anajibu 25 afu anaendelea na mambo yake sasa gusa kupunguziwa bei jibu utakalopata we acha tu
 
Ukijidai ku bargain bei ya kitu ndio utakoma. ..

Utaambiwa "Hiyo Hailipi" ...
 
Ni kweli kabisa mkuu, hawa jamaa wa huku sijui wakoje wenyew ubabe tu hata ktk biashara. Mm na waambiaga sio ustaalabu huo
 
Na ujanja wangu wote ukijumlisha na uchakaramu wangu wote kuna Siku humu humu niliwahi kusema kwamba hakuna Mkoa ninaouogopa na kuuheshimu nchini Tanzania kama wa Arusha kuna ambao mlikuwa hamnielewi ila sasa naona taratibu naanza kueleweka kwa matukio ambayo yanawatokeeni wengine.

Wewe kama Mkoa tu ' Malaya / Makahaba ' wanaojiuza wana mibonge ya Mibisu ' mbavuni ' unategemea kuna ' Customer Care ' hapo? Huo Mkoa ukiishi inakubidi na Wewe kidogo ' Fyuzi ' zako zilizomo ndani ya Medulla Oblangata yako ziwe ama zimelegea au zimeachia ndiyo utauweza la sivyo kila siku utakuwa na ' majeraha ' tu.

Shikamooni Arusha.
 
ok mkuu, ulikuwa pcb nini.. mi nilikuwa o level kipindi hicho,
Ha haa wewe ndiye ulikuwa unashinda mtegoni? Mimi nilikuwa najichimbia chumba cha pale mtegoni (dereva wa Nissan ya shule aliweka saloon yake mle
 
Unataka kubembelezwa?
Kama mteja utanunua kama siyo pita hivii...usituletee marinjirinji bwasheee
 
Unataka kubembelezwa?
Kama mteja utanunua kama siyo pita hivii...usituletee marinjirinji bwasheee
Yaani kuna watu waajabu wanakuja kununua pipi ya shilling 50wanataka uwabembeleze uwalambe na miguu ,utadhani waliombwa waje kununua
Kama wanaona Huduma mbaya wapite wima waondoke sio kutiana nuksi asubuhi asubuhi
 
hawa jamaa wameshazoeshana hivyo. mie nimekaa miaka minne Arusha. Mteja akienda dukan anamwambia mwenye duka nipe kitu flan wakat huku Dar tunasema naomba. ni tabia ambayo wamezoeshana na wenyewe wanasema mwenye pesa ndo mwenye kauli
 
hawa jamaa wameshazoeshana hivyo. mie nimekaa miaka minne Arusha. Mteja akienda dukan anamwambia mwenye duka nipe kitu flan wakat huku Dar tunasema naomba. ni tabia ambayo wamezoeshana na wenyewe wanasema mwenye pesa ndo mwenye kauli
Kwakweli mi mwenyewe maswala yakwenda dukani nakuanza kusema naomba naona ni ushamba na ukijijini huwaga sifanyi hivyo
Niombe kwani nachukua bure?
Huwa nasema nipatie kitu Fulani basi maswala ya kusema asante sisemagi kwani kanipa bure ?
 
ARUSHA.
Ukipanda hiace muombe konda mapema una miatatu hata ukitoa msimbazi au blue atakata ile miatatu.

pia utakumbana na dadazako wa kimeru hawa hawana samahani au pole ni fully ukorofi kwenye hizo biashara km ukinunua soksi za mtumba..!!
 
Huna hela unataka ubembelezwe,tafuta pesa sela,mbaya sana wanaume kuomba kubembelezwa na mwanaume mwenzako,Wote mnataka kufanya mbadilishano afu unataka mmoja wapo awe mpole kwako

Lakini mbona me naona hakuna mkoa ambao una watu wenye lugha za kibiashara kama hiyo mikoa ya kaskazini au ulitaka upigiwe magoti
 
Back
Top Bottom