Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kwenye soka la kisasa unaweza ukawa na vingi sana ila kama ukiwa hauko available mda mwingi thamani yako inashuka

Partey alikua mzuri

Jesus alikua mzuri

Tulikua na Tomiyasu

Hao wote injury imefanya tuwape mkono wa kwa heri

dah.. mwamba tomiyasu ,huyo mtu majeraha yamemuathiri mno kiwango chake.
 
Guardiola ameondoka city lakini hajaondoka na magoli 20 ya Haaland.

Mourinho aliondoka chelsea lakini hajaondoka na magoli 10 ya Drogba.

Badala yake Guardiola na Mourinho tunawahukumu kwa trophies walizopata na walipozifikisha timu. Siyo mchezaji.

Tutake tusitake kuna muda kocha atafanya uamuzi wa kuondoa mtu ambaye sisi tunakubaliana ni mzuri ila kwa kocha ataona anamchelewesha kufika anapotaka.

Amorim alimtema Sancho na Rashford, Liverpool ilimuachia Mane na Firmino, Arteta akamuachia Aubameyang, Ramsdale n.k.
 
Leo saa 05:00 tuna game na Brighton.

UkIsema ufocus na matokeo pekee inaweza isikusumbue akili lakini nataka ujue kwamba sisi dhidi ya Brighton imekua ni vita endelevu kwakua yameshatokea yafuatayo;

Mwaka 2022 goli la Martinelli lilikataliwa baada ya VAR kujizungusha muda mrefu sana.

Mwaka 2024 Rice aligewa kadi ya pili ya njano ambayo ilitolewa huku akiwa ametoka kukatwa mtama na mchezaji wa Brighton. Kwenye mechi hii hii mchezaji wa Brighton aliunawa mkono ila VAR ikagoma kutoa penati.

Inawezekana tukio unalolikumbuka kwa karibu ni la mwaka 2025. Saliba anaruka kichwa anaupata mpira kisha anagongana na Joao Pedro. Refa akaweka penati, shida ni kwamba Saliba alianza kuugusa mpira.

Ni kivipi VAR na Refa waliona inabidi iwe penati hiyo ni juu yao.

Tulivyowafunga moja bila kocha wao alinukuliwa akisema Arsenal haichezi mpira, ni timu moja tu ilikuja kucheza mpira leo.

Akasema ilitakiwa tugewe njano nyingi kwa kupoteza muda, kisha akasema Arsenal inajitengenezea kanuni zake za mpira ndiyo sababu inashinda mechi.

Alikua anatumia muda mwingi kumuambia kamisaa Gabriel anastahili yellow au mchezaji fulani anastahili yelly. Hii ilisababisha agombane na Arteta wakiwa kwenye touchline.

Jana hajaongea shombo, ameongea kwa adabu tofauti na kawaida yake. Mashabiki wengine wanaamini Fabian alikua anasumbuliwa na utoto na media zilikua zinafanya kusudi kumchokoza ila sasa hivi amekua kwenye kazi ndiyo sababu kabadilika.

So with Brighton tunacheza na timu iko vizuri lakini tunatakiwa kudeal na perception na vita za nje ya uwanja
 
Tukiondoa hayo mengine these guys are not bad.

Kenge walishinda nne kwa tatu ila walikua dominated kila kona, Brighton aliondoka na possession ya 70+ dhidi ya kenge, 60+ dhidi ya leeds, 50+ dhidi ya nyumbu.

Ninaamini hata leo game plan ni ile ile, dominate and suffocate mpaka ujikute huwezi tena kuzuia mashambulizi.

Our midfielders ndiyo wataleta impact kubwa sana ya nini kitatokea kwenye hii game. They're physical and we are as well, nahitaji long shots takers, wings ziwe na pace na pasi za one two zifanywe kwa wingi.

Kikosi kikitoka tutaona zaidi
 
Hawa Spurs wakaoge Maji ya bahari

Mechi ya 5 hii hata bao moja hakuna 🙌

Dakika 79 hii, mashabiki wamekasirika wanaamua kuondoka uwanjani 😅
 
IMG_20260919_161825_629.png
 
Kikosi kimetoka Timber ameanza, na Bruno ameanza.

With Bruno tuna physical na technical presence kwenye kiungo na hapohapo tuna long shots taker. Pia ni mzuri wa long balls huyu jamaa.

Wingers ni walewale, Tzolis na Saka, AM ni Odegaard.

Hata hivyo nafikiri ilibidi Gyokeres awepo kama Bruno yupo kwakua Bruno siyo mvivu kufanya through balls na long balls.

Kikosi cha Brighton kipo vizuri pia wana Paschal, Kostoulas, Gomez na Cuyper. Wana defense ambayo ina CB pairing inayojuana huku Vuskovic akiwa na sifa ya ziada ya ball playing defender.

On paper kila timu ina chance so kinachobaki ni kwa makocha kua superior technically. Kama tutaacha possession na kufocus na ushindi ni sawa pia kwakua Tzolis ana pace ya kutumika kwenye transition au counter. Shida ni kwamba hatuna mwingine in practice ingawa on paper wapo Odegaard na Saka.

ST wetu bwana Kai sina cha kumsemea. Ambacho ni weakness kwake yeye anakigeuza na kuscore. So tusubiri tuone.

Baada ya hii game tunaenda kwenye international break so ni muhimu kushinda hii mechi kivyovyote.

Let's go
 
Kikosi kimetoka Timber ameanza, na Bruno ameanza.

With Bruno tuna physical na technical presence kwenye kiungo na hapohapo tuna long shots taker. Pia ni mzuri wa long balls huyu jamaa.

Wingers ni walewale, Tzolis na Saka, AM ni Odegaard.

Hata hivyo nafikiri ilibidi Gyokeres awepo kama Bruno yupo kwakua Bruno siyo mvivu kufanya through balls na long balls.

Kikosi cha Brighton kipo vizuri pia wana Paschal, Kostoulas, Gomez na Cuyper. Wana defense ambayo ina CB pairing inayojuana huku Vuskovic akiwa na sifa ya ziada ya ball playing defender.

On paper kila timu ina chance so kinachobaki ni kwa makocha kua superior technically. Kama tutaacha possession na kufocus na ushindi ni sawa pia kwakua Tzolis ana pace ya kutumika kwenye transition au counter. Shida ni kwamba hatuna mwingine in practice ingawa on paper wapo Odegaard na Saka.

ST wetu bwana Kai sina cha kumsemea. Ambacho ni weakness kwake yeye anakigeuza na kuscore. So tusubiri tuone.

Baada ya hii game tunaenda kwenye international break so ni muhimu kushinda hii mechi kivyovyote.

Let's go
Tutawapokea Brighton jinsi watakavyokuja, waje kihuni tunaruka nao maje kisatqarabu basi tutawafundisha soka safi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom