Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Energy drinks, trauma, short on target standard and now aura
Mtaongea yote ila sisi tuna neno Moja juu yenu ARSENAL HATABEBA UBINGWA AS USUAL.
Arsenal nimekubali ni wazee wa standard wamekaa nafasi ya Kwanza kwa siku 200+ na Bado watakosa ubingwa . False hopes for 200+days .
Asee..
 
Kuna muda mpaka nashikwa na huruma , nembu Leo tusahau yote tujadili kiungwana tu wakuu.
Tatizo la timu yetu ni Nini ?? Katika game ya 31 tulikua tunaongoza kwa difference ya point 9 zikiwa zimebaki game 7 , only 7 games to go tukakubaliana kila mmoja ashinde games zake, ghafla tu saivi ni goals difference ndio tunaongelea from 9 points ahead.

Ukitaka kuamini mashabiki wa arsenal ni wendawazimu still wanaamini watashindaa hili kombe kwa goal difference kutoka kwenye 9 points ahead.
Nyinyi msimu huu hili jukwaa ni either libadilishe jina liwe false hopers au muendelee na jina lenu ila kwa shartii Moja tu tuwaite kwenye HQ za JF tuwachape viboko hadharani.
Maana mtaueleza Nini tuwaelewe?
Dah
Technologia
 
Mmevunja rekodi nyingine ya kuchukua ubingwa ila hamjatoa mchezaji bora wa ligi sababu ya magoli ya kona wadau. Big Up
Acheni kupotosha watu, na inaonesha nyie sio wafuatiliaji wa kina wa Ligi Uingereza, ni wakurupukaji tu hamjui hamna data zozote watoto wa elfu10, Mimi ni Liverpool fan, lakini nikupe taarifa hii...
Klopp na Liverpool yake walichukua ubingwa Epl msimu wa 2019/20 baada miaka 30 na Mchezaji Bora wa msimu wa Ligi alikuwa kiungo mchezeshaji wa Mancity Kevin De Bruyne, hebu kabla kuongea muwe mnakuja na taarifa Sahihi za uhakika.
 
Martinelli bado ana kitu miguuni mwake abaki kwa msimu mmoja au miwili
Mkuu labda una mapenzi binafsi....ila kwa muda alopata wa kucheza Martinelli mpk sasa....kiukweli kabisa kwa pale Arsenal uwezo wake umeishia pale....yaani hafundishiki zaidi....akienda ligi nyingine atang'aa ila sio EPL....aondoke aje Rodgers wasaidiane na trossard pale
 
Uefa ya kwanza mliichukua mwaka gani masta, tuweke records sawa !
1994 - UEFA Cup Winners Cup, Coppenhagen. Arsenal tulishinda 1-0 dhidi ya Parma ya Italia.

Hili kombe lilikuwa linapambaniwa na timu zilishoshinda vikombe vya ndani vya ligi za Ulaya kama vile FA Cup ya England, Copa del Rey ya Spain, etc.

Mwaka 1999 hili kombe lilikuja kufutwa na kujumuishwa na shindano lingine, Europa League baada ya mfumo wa Champions League kubadilika na kuanza kuchukua timu za nafasi za juu, badala ya washindi wa vikombe vya ndani tu. Tukitaka 'kujimwambafy' saaana tunaweza kusema tuna ka Europa au ka pre-Europa kamoja.

Mwaka 1995 tulifika fainali katika kutetea ubingwa wetu ila tulipigwa 1-2 na Real Zaragoza ya Spain.

1780134054412.png
 
Liver wamemfukuza kipara. Nitacheka wakimtaka Alonso na Alonso akikubali
 
1994 - UEFA Cup Winners Cup, Coppenhagen. Arsenal tulishinda 1-0 dhidi ya Parma ya Italia.

Hili kombe lilikuwa linapambaniwa na timu zilishoshinda vikombe vya ndani vya ligi za Ulaya kama vile FA Cup ya England, Copa del Rey ya Spain, etc.

Mwaka 1999 hili kombe lilikuja kufutwa na kujumuishwa na shindano lingine, Europa League baada ya mfumo wa Champions League kubadilika na kuanza kuchukua timu za nafasi za juu, badala ya washindi wa vikombe vya ndani tu. Tukitaka 'kujimwambafy' saaana tunaweza kusema tuna ka Europa au ka pre-Europa kamoja.

Mwaka 1995 tulifika fainali katika kutetea ubingwa wetu ila tulipigwa 1-2 na Real Zaragoza ya Spain.

View attachment 3597505
Hendry eeh, unajua nakuheshim, hicho kikombe unaona kinafanana na hichi?
images.jpg

Au na ww umeshaanza kutumia vinywaji vya dereva boda?
 
Back
Top Bottom