Mwacheni Theo ni kifaa tosha pamoja na Gervinho, kuna siku mpira hukataa kutokana na formation ambayo prof anapenda wachezaji wacheze. Kumbukeni kwamba wingers huwa wanashamiri wakati full backs wanawasaidia kutoka nyuma hivi sasa kule nyuma both sides wazoefu wameumia, Sagna pamoja na Gibbs. Ramsey ni mzuri lakini sio kama Cesc hata Arteta naye hajaweza kumudu vizuri pale katikati. Kumbukeni kwamba Song hakuwepo hivyo tulikuwa na pengo kubwa sana ..... ..... ..... hivi sasa yeye ndiye mwenye pasi za uhakika hasa kwa RVP last two matches mnaweza kukumbuka jinsi alivyokuwa anashirikiana na RVP. Song is back next match.
Vijana wapo vizuri sana majeruhi yakiisha atakaporejea hususan Jack ndio mtaona kwa nini prof alikubali Cesc kuondoka, kijana ni moto wa kuotea mbali. Mechi ya jana tumeshinda na leo tumezidi kuwasogelea wapinzani wetu .... .... mwisho wa mwezi ndio tutakuwa half time. Ngwe ya pili mtaona jinsi EPL itakavyobadilika, we are there to win it!