Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

January top 6 teams after 2games.
FB_IMG_17675659284273967.jpg
 
Mwezi nyuma Arsenal ikasuluhu mpaka akawa kaiacha City kwa points mbili. Mashabiki pinzani, wote siyo wa City pekee, wakasema ikifika January Pep ataanza kushinda mechi nonstop. Na mpaka hapo tayari Arsenal katema kombe.

Hapo ilikua Game Week ya 17.

Wakasema Rodri anarudi na City n mentality monsters.

Rodri akarudi.

January ikaja.

Mentally monsters wakaanza wao dhidi ya Forest saa tisa na nusu na Arsenal ikacheza baadaye saa kumi na mbili. Mentality monsters wakapata goli la ushindi dakika za jioni.

The agenda started immediately. Ikasifiwa attitude na mentality.

Arsenal didn't fold, ikaipiga Brighton 2 kwa 1 tukakaa kimya.

GW 19. Arsenal akaanza na kumpiga Villa. Mentality monsters wakashindwa kuhandle pressure wakasuluhu dhidi ya Sunderland.

GW 20. Arsenal anamfunga Bournemouth, mentality monsters wanasuluhu na Chelsea isiyo na kocha.

Kilichofuata jana? Agenda ni "Mechi bado zimebaki nyingi sana" "Kwanza City mabeki hawapo"

Nani anakumbuka CB wetu starter amekaa nje kwa muda gani? Halafu aliyechukua namba yake naye akaumia, RB akaumia, siku CB wetu anarudi LB anaumia. Rice akawekwa RB, Hincapie anacheza LB sasa hivi.

Nani anakumbuka kwamba hakuna aliyesema mechi bado nyingi wakati Arsenal imeiacha City kwa points mbili? Zaidi ya mimi humu JF.

Unaelewa nikisema dawa ni kufocus na timu yako? Unajua kua kila mtu hua anakua mjinga makusudi ikatokea inaongelewa Arsenal?

Umegundua viazi viazi vingi vya humu hata kulog in JF havitaki?

Anyway, J5 City ana Brighton. Alhamis Arsenal ana Liverpool.

Observe.
 
Dakika ya 94 Gakpo anapata goli anavua jezi ili asherehekee ushindi.

Dakika ya 95 anagewa kadi ya njano ya kusherehekea ushindi.

Dakika ya 96 Gakpo anatolewa, anaingia beki kuimarisha ulinzi.

Dakika ya 97 Fulham wanasawazisha.

Mpira unaisha dakika nne zaidi. Unaisha dakika ya 101 ingawa ziliongezwa dakika 7.

Kanjibai kasema huu mwaka atapuna watu hadi rambirambi. Mnaobet mjihadhari, aliongea kwa jeuri na kujiamini sana siku hiyo
 
Nngeshangaa pamoja na mafanikio ya maressa amefukuzwa then amor ndo abaki 😂 bado arteta akikosa ubingwa huu mwaka wanamla kichwa
 
Damu nzito kuliko maji.

Jana wakati game linaanza, makenge yalikuwa yanaimba wimbo wao ule ule, wafungwe ili watukomoe Arsenal.

Na kweli, yalivyopigwa chuma, makenge yakaanza kushangilia bhana.

Dakika ya 94, wakati Fernandez anarudisha kamba, bhana weee, yasianze kushangilia tena.

Kweli damu nzito kuliko maji!
 
Damu nzito kuliko maji.

Jana wakati game linaanza, makenge yalikuwa yanaimba wimbo wao ule ule, wafungwe ili watukomoe Arsenal.

Na kweli, yalivyopigwa chuma, makenge yakaanza kushangilia bhana.

Dakika ya 94, wakati Fernandez anarudisha kamba, bhana weee, yasianze kushangilia tena.

Kweli damu nzito kuliko maji!
Walichokifanya jana ndio kenge jinsi walivyo.
 
Kuna tatizo kubwa sana pale unyumbuni, game nyingi nyumbu wanacheza oya oya au kama vipi vipi
Sina uhakika kama amorim ndio amewaambia wacheze hiv ninavyoona mimi hapa
Niliandika hii comment

BREAKING NEWS: Rúben Amorim has just been SACKED by Manchester United.

Decision made this morning.

IMG-20260105-WA0007.jpg
 
Yaani wakajifanya kusema wapo nyuma yake na yeye akasema wanamsapoti leo kapigwa chini
 
Yaani wakajifanya kusema wapo nyuma yake na yeye akasema wanamsapoti leo kapigwa chini
Kazi ya umeneja ni ngumu ukizingatia team zina vitengo vingine vingi ambavyo vinafanya maamuzi kwa ajili yako.
 
Dogo mimi nime anza kuangalia mpira nyumbani since 2003, mzee ali leta tv za hitachi na Panasonic.

2010 nime angalia fainali za kombe la dunia mwenyewe, nikiwa sebuleni.

Leo hii 2026 naangalia nitakacho, arsenal sio ya maduwanzi boya wee.
Dogo kumbe wakishua enzi hizo unacheki Tv kwenu mna mpaka madishi wakati wengi wakiwa analog na Tv mpaka kwa jirani wachache.

Mimi nimeanza 2008 enzi hizo nipo darala la kwanza
 
Dogo kumbe wakishua enzi hizo unacheki Tv kwenu mna mpaka madishi wakati wengi wakiwa analog na Tv mpaka kwa jirani wachache.

Mimi nimeanza 2008 enzi hizo nipo darala la kwanza
Aisee kumbe humu tupo na watoto, yaani 2008!! upo darasa la kwanza mi ndio napata mtoto wa kwanza, achana na zilizonywewa P2 kipindi nasoma, kama sivo ungeweza kuwa umri wa mwanangu.
 
Back
Top Bottom