Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kwa sababu Victor tunashindwa kumnunua ndo maana hela inaniuma. Bila hivyo hata wangetoa zote me sina shida
Unafikiri Arsenal hawana hela y kumnunua Gyokeres , sema anachofanya Arsenal ni utoto, ameshajua mchezaji mawazo yake yote yapo Arsenal ndio mana hajishuhulishi kubagain, mana wametofautiana buku jero tu, sasa Arsenal wanashindwa kutoa hiyo buku jero kweli?
Ni sawa na msela kuzimikiwa na Mtoto mkali, hutumii pesa nyingi na wala hubembelezi sana.
 
Sijaona wa kumzuia kuchukua kiatu
Chances created by odegard zinaenda kumpata mtu sahihi
IMG-20250722-WA0000.jpg
 
Unafikiri Arsenal hawana hela y kumnunua Gyokeres , sema anachofanya Arsenal ni utoto, ameshajua mchezaji mawazo yake yote yapo Arsenal ndio mana hajishuhulishi kubagain, mana wametofautiana buku jero tu, sasa Arsenal wanashindwa kutoa hiyo buku jero kweli?
Ni sawa na msela kuzimikiwa na Mtoto mkali, hutumii pesa nyingi na wala hubembelezi sana.
Mtoto mkali akikuzimikia kuna jeuri na kiburi flan hivi vinakujaga daah, akichoropoka ndo akili inakukaa sawa. Litatukuta Arsenal tuje tulie kilio cha mbwa koko, tusije tu tukaishia kwa Nikolo Jackson
 
Kama mnataka si mumsajili Sasa mbona mnamsumbua tu mtu kawaganda kama kunguni msajilini watu wafocas na sajili nyingine tumechoka kila saa victor victor
Hata sisi tumechoka bro. Tunawaona kama Sporting ni wahuni wahuni na wanatufanyia uhuni. Tayari wanajaribu kuwaita Manchester United na timu za Saudi ziingilie dili ambalo tunaona kama asilimia 90% tumeshakubaliana na mchezaji ameshasema anataka kuja kwetu.

Habari za mitandaoni nazo si zakuaminika sana maana huenda hakuna anayejua ukweli. Kuna tetesi kutoka Portugal kuwa Arsenal na Sporting wanatofautiana €2.5m tu, huku kuna zingine zikidai Sporting wanataka add-ons ziwe rahisi kichizi yaani, mfano €2.5m Gyokeres akicheza mechi 20 ( nafikiri ilisema za premier league). Sasa mtu asiye na history mbaya ya majeraha, anayeletwa kuwa 1st choice striker, mechi 20 upewe €2.5m ni kipengele cha kueleweka kweli?

Naamini uhuni wanaofanya Sporting ni mkubwa kuliko tunavyoambiwa. Fair play kwao pia lakini. Wanajua wanamchezaji wanaotakiwa kumuuza kwa bei za kina Ekitike na Darwin Nunez, ila wanatuuzia kwa kama 2/3 ya hizo bei, hivyo wanataka kupata kila shilingi inayoweza kupatikana kwake.
 
Arsenal wajitahidi kusajili wasije wakaanza kulia bure; msimu ukianza ni moto utawaka kwelikweli. Haiwezekani timu imekaa misimu miwili mfululizo kwenye 2nd position bila ubingwa.
Timu zingine wanataka kuwatoa hapo na pia kuchukua ubingwa ikiwezekana ila nyie kama vile hamjajiandaa kuwa namba 1.
 
Game ya kwanza tunaanza na nyumbu🤣🤣🤣
Shida sio kumfunga Manchester.....embu ona akili za watu wa arsenal ..mnasajili kumfunga Manchester.? Ubingwa mtakua hivyo hivyo mnausikia kwenye Bomba ... mnakimbiza weeee mwisho wa siku mnakuja hapa kulialia ...mnafikiri kuchukua epl ni kama unachukua toilet paper kwenda kunya....
 
Usiishi kwa mazoea blaza, shauri yako! Jua mnaenda kukutana na Bingwa wa vitimu vyote vya hapa duniani. Usiseme sijakutahadharisha. Muulizeni mbabe wenu PSG
Uzuri siku zinasogea...nyny hata twende tukacheze mbinguni hamtufungi😀😀...Kila msimu tukianza tunajua kabisa kwa uchqche tuna point 4 kutoka kwa majirani zetu Chelsingeli....na tumemchukua madueke madunduka safari hii tunabeba alama 6 kabisa....
 
Ninyi ni wachumba tu ,hamna ubavu wa kupambana na majike shupa ya timu ya wanawake ya pale Stamford Bridge ,acheni kujitoa ufahamu ,yaani Chelsea ni serial winners timu ya wanawake na wanaume ,timu yetu ya wanawake msimu huu ulioisha wamebeba trebble yaani vikombe vitatu , imagine . Ninyi timu yenu ya wanawake ni kubinua makalio tu uwanjani

Nilisahau kukuuliza...

Hivi unajua kuwa timu ya wanawake ya Chelsea hata haimilikiwi na Chelkenge? Mliiuza hiyo timu ili kujikomboa na msala wa PSR. Chelsea Women FC imebaki jina tu na wamiliki wapya wakiamua wanweza kuiita hata Yanga Queens.

Hapa utaona umuhimu wa timu kuwa vizuri kifedha. Arsenal bado inamiliki timu yake ya wanawake na inajiendesha vizuri kiasi cha kuweza kulipa £1m kwa Olivia Smith. Sijui hawa wamiliki wapya wa Chelsea Women wakoje ila huenda sasa timu haitaweza kujiendesha kwa kutegemea misaada ya wamiliki wa timu ya wawanaume na huenda ikashuka kiwango kwa kukosa wachezaji bora.

Hapo si kuna uwezekano wa kupitwa na akina Liverpool, Manchester United na Arsenal?
 
Back
Top Bottom