HENRY14
JF-Expert Member
- May 13, 2021
- 3,593
- 6,932
Yes.ila rodrigo anakupa vyte kasoro ukabaji tu
Ila ukabaji ni muhimu sana kwenye top levels za EPL na timu haziwezi kukubali kuwa na wachezaji wasiowajibika kisawasawa uwanjani. Kule mabeki wanakaba kibabe haswa na bado wanashambulia kama mawinga na mastriker hivyo unahitaji wachezaji wako wote wawe tayari kushiriki katika ulinzi ili kusaidia mabeki wako. Arsenal iankuwaga na defense bora si kwa sababu ya mabeki tu bali kwa sababu kina Kai na Odegaard na wengine kule mbele wanawajibika haswa, kama siyo kwenye 1v1 marking basi pia kwenye kujipanda kuziba mianya na kutengeneza overloads ( 😀 😀 😀 mambo ya dark arts) bila kuchoka.
Rodrygo, Vini na Mpappe walichangia kiasi kikubwa sisi kuwachapa kwa sababu ya ukabaji hafifu wao. Na ndiyo sababu mimi binafsi nitaanza na Martinelli ili kuhakikisha tunamtawala adui katika kila idara halafu Rodrygo aingie baadae wakati mpinzani yuko hoi. Nafikiri pia zile enzi za subs 3 tu hii mbinu ingefaa zaidi kuliko enzi hizi za subs 5 ila bado inasaidia.