Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Oya unazingua mzee, eti boko haramu😅

Soka la wanawake kwanza ninacholipendea ni uhakika wa magoli, yaan huku hakunaga kupaki basi hata kama timu zilizokutana zina tofauti kubwa sana kiubora... na ndio maana unaona timu kama barcelona kushinda 7-0, 9-1, 6-2, ni kawaida sana.

Mechi ya leo tumeingia uwanjani huku Lyon akiwa tayari ana faida ya ushindi wa 2-1, lakini kachezea goli 4 pale pale kwake kwa sababu alikuwa anashambulia licha ya kuwa na matokeo, ingekuwa ni mechi inayowakutanisha wanaume kwa haya matokeo pengine tungeshuudia mechi ikimalizika 0-0 huku mechi ikitawaliwa na mbinu chafu za kupoteza muda na kupak bus.

Kingine ni nadra sana kuona mechi za wadada zikigubikwa na maugomvi ugomvi kama kile ulichoona jana kikifanywa na akina Rudger.
Arsenal yaenda shimoni
Baada ya kuona Liverpool ananyanyua kwapa tena ndani ya miaka michache tu
Huku arsenali akiwa mshindwa sugu, Mwaka wa 20
No epl

Kaenda kutafuta faraja kwenye soka la akina Dada ambalo hata sisi akina dada hatuna mzuka nalo.
 
Siku za nyuma ilikua nadra sana kukuta updates za kina dada, msimu unaenda kuisha kapa ghafla saivi humu kila mtu analeta updates za arsenal women 😂😂
Wewe kule kwenye jukwaa lako ulikuwa unawasifia sana tu wanawake wenu na kupost picha za matokeo yao. Baada ya wao kupotezwa na wanawake wa Man U, Chelsea na Arsenal, ukawatelekeza.

Huku habari za wanawake huwa zipo sana tu. Imetokea bahati nzuri tu kuwa wanawake wetu wamepiga comeback kadhaa za kibabe WCL msimu huu na kufika fainali so habari zetu za jana jukwaa hili ni zao kidogo.

Utakuja kugundua kuwa kabla ya kupoteana na kupitwa na Chelsea, Arsenal ndiyo ilikuwa kinara wa boli la wanawake England na Arsenal ina kila nia ya kurudi juu kutawala soka la England na Ulaya kwa ujumla, yaani kuanzia timu za vijana na watoto, wanawake mpaka wanaume. Arsenal pia iko mstari wa mbele kabisa ikifanya juhudi ya kukuza soka la wanawake

Unachoona si kwa bahati mbaya bali kwa juhudi za club hivyo sisi tunaenjoy tu matunda ya juhudi hizo.
 
Mkikosa UEFA sijui mtatuambia nini nyinyi
watadai kufika semi final au final kwao ni overachievement, maana malengo yao msimu huu ilikua ni kufika quarter-final.
Halafu hizi kima tukiziitaga ni misukule kuna watu hua wanalalamika humu kua huo ni udhalilishaji wa kijinsia.
1710748027241.jpg
 
watadai kufika semi final au final kwao ni overachievement, maana malengo yao msimu huu ilikua ni kufika quarter-final.
Halafu hizi kima tukiziitaga ni misukule kuna watu hua wanalalamika humu kua huo ni udhalilishaji wa kijinsia. View attachment 3318427
🤣🤣🤣


Kwenye sala zao waombe sana tukose Kombe la Europa league

Otherwise watatuambia msimu huu walikuwa wanafanya nini sasa🤣🤣🤣
 
Ndg usidanganyike kama Barcelona anamuonea mbambe wa england Chelsea ambaye anamfunga arsenal kila kukicha na team zote za england , arsenal wanawake atafungwa sio chini ya kamba 5 nafikiri ndio fainali laini Kwa Barcelona kuwahi kutokea na ataendelea kuchukua kombe hili Kwa mwaka wa tatu mfululizo na kuna dalili akafikisha miaka sita mpaka Saba hakuna team ya kuizuia Barcelona hata mwakani.Hii ni Kwa wale tunaofuatilia soka la wanawake tunaongea team iliyofungwa mechi mbili au tatu tu misimu mitatu ya mashindano yote hii ndio Barcelona women .
Naelewa unachozungumza ndugu, pia hata mimi nimfuatiliaji wa soka la wanawake.

kwa msingi wa hoja yako, kumbuka hata sisi tumetoka kumfunga Lyon tena nyumbani kwake ambaye hajapoteza mechi hata moja tangu msimu unaanza, na huyo Lyon amekuwa ni mbabe wa barcelona miaka nenda miaka rudi, ni mwaka jana pekee tu ndio barcelona alimfunga Lyon, sasa kama tumeweza kumnyanyasa Lyon tena kwa kichapo heavy, basi tunaweza kumfunga na huyo barcelona kwenye hiyo fainali, na hasa ukizingatia hakuna kombe lingine tunalotarajia zaidi ya WCL makombe ya ndani yote chelsea amejimilikisha.
 
Arsenal yaenda shimoni
Baada ya kuona Liverpool ananyanyua kwapa tena ndani ya miaka michache tu
Huku arsenali akiwa mshindwa sugu, Mwaka wa 20
No epl

Kaenda kutafuta faraja kwenye soka la akina Dada ambalo hata sisi akina dada hatuna mzuka nalo.
Hujui tu, Arsenal Women wanacheza soka safi na la kuvutia kuliko hata liverpool ya akina Mo salah.

Karibu jumatano wanacheza na Aston villa ujionee burudani, na sio mpira wa kuchoshana kama ule uliozoea kuuona pale anfield ambapo akina Luis Diaz muda wote ni kukimbia tu, na kuna muda wanakimbia mpaka wanasahau mpira.
 
Ni aibu kubwa wanaume ligi imewashinda mnabadilisha gia hewani kujidai ni mashabiki wa ligi ya kina Mama😂
Wewe unawivu tu kwa sababu wanawake wenu si lolote si chochote kwenye boli huku wakwetu ndiyo vinara. Hapa najua wote mnaomba Barcelona watuchape ili mpate la kusema.
 
Hujui tu, Arsenal Women wanacheza soka safi na la kuvutia kuliko hata liverpool ya akina Mo salah.

Karibu jumatano wanacheza na Aston villa ujionee burudani, na sio mpira wa kuchoshana kama ule uliozoea kuuona pale anfield ambapo akina Luis Diaz muda wote ni kukimbia tu, na kuna muda wanakimbia mpaka wanasahau mpira.
Sisi tunashabikia mechi za wanaume wa shoka
Nyie ligi ya akina Mama, mmemkacha Aterta
Basi badilisheni kabisa thread
Iwe arsenal queens😂
 
YOur fellow fools opted out hawajasema kitu
Inasikitisha sisi ndio tunawaona nyie wehu kumbe nyie hamjitambui ndio fools, kuwa shabik wa Arsenal lazima kuna fuse zinakua zimepga shoti mahala.

Hapo na msimu huu mtatoka patupu, mtakuja kumsifia Arteta kuwa mmetolewa kwnye hatua nzuri, hizo ni akili??
 
Back
Top Bottom