Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Tuseme zile kelele za kumtukana Kroenke na Arteta kwa kutosajili dirisha dogo la januari zimeishia wapi?
Je, ikitokea kama zali mkabeba UCL bila striker bado mtaona kuna umuhimu wa kusajili striker dirisha lijalo?

Au ndio kusema na nyie mmefika mliopofika kama bahati tu kiasi kwamba mkiambiwa mrudie itakuwa kipengele?
Arsenal akichukua CL bila ST itakua ni generational story, considering majeruhi aliyoanza msimu na yakaendelea mpaka msimu unaisha.

Itakua ni achievement kubwa kwa kuzingatia hata kikosi chetu cha invincible kilishindwa hiki kitu. Itakua ni best story ya kuhadithiana muda wa jioni vijiweni. Ila ni inamaanisha kusajili kuko palepale

Kama nyinyi mkirudi CL kwa mlango wa nyuma wa kuchukua Europa. Itakua the best underdog story.
 
Kama nyinyi mkirudi CL kwa mlango wa nyuma wa kuchukua Europa. Itakua the best underdog story.
😛 😛 😛 Yaani we jamaa na United hampatani kabisa. Kwenye kila story ya man united lazima utafute neno la ajabu kutushusha tu.
Nakumbuka game ya kwanza tulivyokuwa tunawabana kabla hamjafunga yale magoli yenu ya bahati ya kona kicks, katika uchambuzi wako ulitumia neno SWARMING ila uchezaji ule ule kwa arsenal unatumia neno OVERLOADING.

Ilimradi united tuonekane hatuko level yenu tu.
 
😛 😛 😛 Yaani we jamaa na United hampatani kabisa. Kwenye kila story ya man united lazima utafute neno la ajabu kutushusha tu.
Nakumbuka game ya kwanza tulivyokuwa tunawabana kabla hamjafunga yale magoli yenu ya bahati ya kona kicks, katika uchambuzi wako ulitumia neno SWARMING ila uchezaji ule ule kwa arsenal unatumia neno OVERLOADING.

Ilimradi united tuonekane hatuko level yenu tu.
Sijawahi kutumia neno overload.

Swarming ni aina ya defense, kwa ninazozijua mimi kuoverload siyo aina ya defense. Hii style mliitumia sana kipindi cha Eriki Kichwa Ngumu
 
Hivi mnaamini Arsenal mtabeba ubingwa?! embu acheni masihara tangu lini mkawa serious kubeba ubingwa!!

Mara hii mmeshasahau nyie mmelaaniwa!!

Mkibeba ubingwa niitwe Chura nimekaa palee.
Labda wabebe ubingwa wa nafasi ya 2, ili Arsenyau abebe kombe labda tuziombe kamati za FA na Uefa waanzishe utaribu mpya wa kugawa makombe mawili kwenye ligi zao, iwe mshindi wa kwanza anapewa kombe na alishika nafasi ya pili pia awe na kombe lake.
Kiufupi Arsenyo kila msimu uwezo wao unaishia nafasi ya 2, yaani hawa ni sawa tu na ile style pendwa ya mbuzi kagoma.
 
😛 😛 😛 Yaani we jamaa na United hampatani kabisa. Kwenye kila story ya man united lazima utafute neno la ajabu kutushusha tu.
Nakumbuka game ya kwanza tulivyokuwa tunawabana kabla hamjafunga yale magoli yenu ya bahati ya kona kicks, katika uchambuzi wako ulitumia neno SWARMING ila uchezaji ule ule kwa arsenal unatumia neno OVERLOADING.

Ilimradi united tuonekane hatuko level yenu tu.
😀 😀 Swarming ni aina ya ukabaji ya kimtaani au timu zisizojua boli kwa kuutumia wachezaji wengi kumzonga mwenye mpira na kwenda kila mpira ulipo. Yaani unakuta wachezaji hata watano wamemzingira mwenye mpira na kila mpira utapo hamishwa nao wanahama nao, kama nyuki vile.

Overloading ni upangiliaji wa timu iwe katika ukabaji au ushambuliaji ambao unafanya timu iwe na mchezaji mmoja au zaidi dhidi ya wachezaji wa mpinzani. Mfano beki wa kushoto kuingia kati ili mido wawe watatu dhidi ya wawili wa mpinzani au kipa kutoka na kupokea pasi na kutoa kwenye defense yenye mabeki watatu na kuongeza kuwa wanne ili kukwepa press ya mpinzani yenye wachezaji watatu au pungufu ya hapo. Ni kama kutengeneza shambulizi halafu anayeshambulia awe na watu wengi kuliko anayelinda (2v1, 3v2, 5v3 nk). Yaani ni mipangilio siyo kuzonga na wachezaji kibao kama timu za mitaa ya Mwananyamala. Swarming ilikuwa style pendwa ya Baba Ubaya 7hag katika kutudhibiti sisi na ilimsaidia maana sisi hatujazoea boli la kimtaani la kombe la mbuzi.
 
Nyie Kima najua kabisa nyinyi ni wasindikizaji na lazima mtatuangusha.
Hivi mmeshavuta picha msimu huu makombe ya Uefa, Europa na Conference Leagues yote yakitua England tutakua tumeiheshimisha Epl kwa kiasi gani?View attachment 3308307
Arsenal: kiwanda cha washindi. Tuna export mabingwa kwenda timu zote Ulaya na duniani kwa ujumla, na sasa tumeamua kuanza kuchukua ubingwa wenyewe. Wapinzani watatukoma.
 
Arsenal: kiwanda cha washindi. Tuna export mabingwa kwenda timu zote Ulaya na duniani kwa ujumla, na sasa tumeamua kuanza kuchukua ubingwa wenyewe. Wapinzani watatukoma.
HENRY14 naona umeamua kuikamatia mikoba ya Masingeli ya kuendeleza false hopes humu, mimi nakukumbusha tu kila lilipokua linakuja suala la ubingwa Masingeli alikua analiongelea kwa overconfidence zaidi yako, ilifikia kipindi Masingeli aliwashawishi misukule yake humu kununua mpaka sare ya vijora vya kusherehekea ubingwa wa Epl 2023/2024
Kilichokuja kumkuta Masingeli hata kuingia kwenye hili jukwaa sasa hivi anaingia kwa kuibiaibia, maana kuna wananchi wenye hasira kali humu muda wote wamebeba vitu vyenye ncha kali wanamsubiria kwa hamu asogeze tu uso wake wale nae sahani moja.
Nahofia na wewe yasije yakakukuta tu kama yaliyokumkuta Masingeli, maana hili timu lenu kwa kweli sio la kulichukulia dhamana kabisa linapokuja suala la kubeba kombe.
Screenshot_20250113-083550.jpg
 
emoji1787.png
emoji1787.png
emoji1787.png
HENRY14 naona umeamua kuikamatia mikoba ya Masingeli ya kuendeleza false hopes humu, mimi nakukumbusha tu kila lilipokua linakuja suala la ubingwa Masingeli alikua analiongelea kwa overconfidence zaidi yako, ilifikia kipindi Masingeli aliwashawishi misukule yake humu kununua mpaka sare ya vijora vya kusherehekea ubingwa wa Epl 2023/2024
Kilichokuja kumkuta Masingeli hata kuingia kwenye hili jukwaa sasa hivi anaingia kwa kuibiaibia, maana kuna wananchi wenye hasira kali humu muda wote wamebeba vitu vyenye ncha kali wanamsubiria kwa hamu asogeze tu uso wake wale nae sahani moja.
Nahofia na wewe yasije yakakukuta tu kama yaliyokumkuta Masingeli, maana hili timu lenu kwa kweli sio la kulichukulia dhamana kabisa linapokuja suala la kubeba kombe. View attachment 3309079
Mikoba ya Hamisi kaichukua mkorea na yuko sahihi. Arsenal ya sasa si ile ya miaka 10 iliyopita. Sasa tunaandamwa na FA na PGMOL na majeruhi kedekede ila bado tunaupiga mwingi.
 
Msikose kutazama mtanange mkali Arsenal W vs Lyon W saa 8.30 mchans wa leo. Semi final UEFA
Kila la heri kwa wanawake wetu. Lyon ndiyo wanawake version ya Real Madrid ya wanaume kwenye UCL, yaani ni kama lao na UEFA wanawake wanaweza hata kulibadilisha hilo kombe jina liitwe UEFA LYON LEAGUE.

Na sasa wana kocha wetu wa zamani Joe Montemurro. Alivyokuwa Arsenal tulikuwa tishio balaa mpaka hata Chelsea walikuwa hawapendi kukutana na sisi. Kwa kifupi Lyon ni wamoto kinoma ila natumaini tutawapatia ushindani na hata kuwashinda.
 
Back
Top Bottom